KUHUSU RAY C KUZUSHIWA KIFO
Kuna watu wengi wamekuwa wakiuliza kuhusu hali ya RayC, kuna mtu ambaye
kwa sababu ambazo hazijulikana aliaanza kuzusha taarifa ya kifo cha RayC
jana mchana, blog hii ilipigiwa simu kadhaa ambazo zimeendelea mpaka
leo kuulizia ukweli kuhusu taarifa hiyo. TAARIFA HIYO NI UWONGO MTUPU.
Moja ya watu walioweka kwenye ukurasa wake wa Facebook taarifa hii ni
mwanafunzi aliyeko Urusi aitwaye Musa, na alipojaribu kuhojiwa kuhusu
hilo aliishia kujibu kwa matusi. Katika wiki hii ya majonzi katika
tasnia ya sanaa pia msanii mwingine alizushiwa kifo na kulazimisha blog
hii kuwasiliana na viongozi wa tasnia ya msanii husika kuulizia kuhusu
hili, pia hilo lilikuja julikana kuwa ni uwongo. Swali ni mtu wa namna
gani unaweza kuzua kuwa binadamu mwenzio amefariki wakati unajua ni
uwongo mtupu?
Miezi kadhaa iliyopita blog hii ilitumiwa sms , tena na
mwandishi mwenye heshima kuwa mwanamuziki fulani aliyekua nje ya nchi
amefariki na kuwa eti amezikwa Magomeni tayari, ililazimika kumpigia
simu mwanamuziki mwenyewe ambaye bahati nzuri alipokea simu mwenyewe
akiwa mzima wa afya. Chonde ndugu zangu tabia hii chafu lazima ikome.
Hapa nawaunganisha kusikia sauti ya mama yake RayC akiongea kuhusu uzushi huo
Hapa nawaunganisha kusikia sauti ya mama yake RayC akiongea kuhusu uzushi huo
CHANZO: http://musicintanzania.blogspot.com
Post a Comment