Baadhi ya ndugu, jamaa na marafiki wakiwasili nyumbani kwa Marehemu SAJUKI Tabata Bima jijini Dar es Salaam leo.
Mke wa marehemu Wastara aliyefunikwa kanga ilikuwa ni vigumu kuamini
kama mumewe kipenzi hatamuona tena alikuwa akilia muda wote na
kufarijiwa na ndugu wa karibu nyumbani kwao Tabata Bima jijini Dar.
kushoto ni mama wa marehemu Bi. Zaitun
|
Msanii wa filamu Tea na mdau wa filamu nchini Zamaradi wa Clouds Fm na kipindi cha Take One cha Clouds Tv |
|
Wasanii wakiomboleza kushoto ni Monalisa |
|
Dokii akiingia msibani |
|
Bibi wa Marehemu akiiingia nyumbani |
|
Sebuleni wanandugu wakiwa wanaomboleza |
|
Aha we acha tu, anaovyoonekana kusema Yusuph Mlela |
|
Wasanii hawa ndio walikuwa kwenye filamu ya mwisho ya merehemu ambayo haikutoka inaitwa Mwanasheria |
|
Wastara yani ilikuwa ni vigumu kuvumilia na kujikuta akilia muda wote kushoto ni mama wa marehemu aitwae Zaitun |
|
Sehemu ya mbele ya nyumba ya marehemu |
|
Viti na mahema vikiletwa kwa ajili ya waombolezaji |
Wasanii wakiwa wamejitokeza katika msiba wa mwenzao.
Watu waliojitokeza msibani huku wengine wakiwa wamekaa kwenye mitaro
Watu wakiwa msibani huku wakijadili mambo mbali mbali. Msiba wa
Marehemu Juma Kilowoko 'Sajuki' umewagusa wengi na kuleta simanzi.
Marehemu Juma Kilowoko anatarajiwa kuzikwa ijumaa saa 5 katika makaburi ya Kisutu jijini Dar es Salaam
SALAMU ZA RAMBIRAMBI KWA FAMILIA
Waziri wa Habari, Vijana , Utamaduni na Michezo Dkt. Fenella
Mukangaraamewatumia salamu za rambirambi, ndugu, jamaa na wasanii wote
nchini kufuatia kifo cha msanii Juma Kilowoko (SAJUKI) kilichotokea
usiku wa kuamkia tarehe 02/01/2013 katika Hospitali ya Taifa Muhimbili.
Taarifa iliyotolewa leo, jijini Dar es salaam ,Wizara ya Habari, Vijana
na Utamauni na Michezo imepokea kwa masikitiko na huzuni kubwa taarifa
za kifo cha msanii huyo na kuongeza kuwa kifo hicho ni pigo katika
tasnia ya filamu hapa nchini.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo Kifo chake ni pengo kubwa kwa Serikali, wadau
wa tasnia ya filamu na michezo ya kuigiza nchini kwa ujumla.“Nimepokea
kwa masikitiko makubwa taarifa ya kifo cha SAJUKI sina maneno ya
kuelezea masikitiko na huzuni nilinayo , kwani kifo chake ni pigo katika
tasnia ya filamu za michezo ya kuigiza” alisema Dkt Mukangara.
Dkt. Mukungara amewataka ndugu, jamii na wasanii wote kuwa wavumilivu na
watumilivu wakati wote wa msiba na kumuombea marehemu makao mema kwa
Mwenyezi Mungu.
Juma Kilowoko (SAJUKI)ni mzaliwa wa mkoa wa Ruvuma. Sajuki alianza
kujihusisha na masuala ya maigizo alipojiunga na kikundi cha Kaole na
baadaye filamu. Filamu alizocheza ni pamoja na Revenge ya Kampuni ya
RJ.
Mwaka 2008 aliamua kuanza kutengeneza kazi zake mwenyewe ambapo filamu
yake ya kwanza iitwayo Two Brothers kwa kushirikiana na Shija
Deogratious ilitoka. Sajuki baadaye aliamua kuanzisha kampuni yake
iitwayo WAJEY Production Company ambapo alitengeneza filamu nyingi
zikiwemo Mboni Yangu, Round, Briefcase , Kijacho, Kozopata, Mchanga na
Keni, 077( Zero Seven Seven).nk
Sajuki alifanikiwa kucheza michezo ya kuigiza na filamu na wasanii wengi
wenye majina hapa nchini. Sajuki amebobea katika Uigizaji, Utayarishaji
na Uongozaji wa filamu.
Sajuki alianza kuugua mwaka 2010 na hali ilizidi kudhoofu mwaka
2011,ambapo alikwenda kutibiwa nchini India. Wadau wengi wa tasnia ya
filamu walifanikiwa kutoa michango mbalimbali iliyomwezesha Sajuki
kupata matibabu yake. Alirudi na kuonekana kapata nafuu kidogo jambo
ambalo lilileta matumaini na furaha kwa watanzania; aliporejea tu
aliweza kutoa filamu iitwayo Kivuli huku filamu nyingine ikiwa katika
hatua ya utengenezaji.
Aidha hali yake ilibadilika jambo lililolazimu alazwe katika hospitali
ya Taifa ya Muhimbili hadi umauti ulipomkuta usiku wa kuamkia tarehe
02/01/2013
Mungu ailaze roho ya Marehemu mahali pema peponi. AMEN.
Picha na www.elimuboratanzania.blogspot.com
Post a Comment