Mwinyi awaangukia viongozi wa dini



RAIS mstaafu wa awamu ya pili, Alhaj Ali Hassani Mwinyi amewataka viongozi wa kidini nchini kuihami amani na utulivu inaotishiwa kuvurugwa na misukosuko ya kidini, kisiasa na kijamii  inayojitokeza katika maeneo mbalimbali yanchi.


Alhaj Mwinyi alisema hayo wakati maadhimisho ya sherehe za siku ya uzawa wa Mtume Mohamma (SWA), yalioandaliwa na Jumuiya ya Khoja Shia Ithnaasheri, kufanyika jijini Dar es Salaam leo.
Alisema nchi hivi sasa inapita kwenye misukosuko inayokana na vitendo hivyo na endapo viongozi wa kidini hawatakuwa makini katika kukemea waumini wao basi huenda nchi ikaingia kwenye matatizo ambayo hayana slahi kwa nchi.
Alhaj Mwinyi alisema mkiwa viongozi wadini mnalo jukumu la kila mmoja wenu kutumia elimu na fursa zilizopo kwa kuwatuliza vijana kutoingia katika vitendo vya uvunjifu wa amani kwa kisingizio cha dini.
“Tanzania inaongoza kwa kudumisha amani, utulivu na ustaarabu kwa miaka mingi kama ingekuwa wachezaji mpira tungesema sisi ni machampioni wa amani katika Bara la Afrika”alisema Alhaj Mwinyi.
Alisema ni wajibu wa Masheikh hao kusimamia na kulinda amani na utulivu uendelee kuwepo ili kila muumini aweze kufanya ibada, kwenda msikitini na kufanya shughuli nyingine za maendeleo kwa maslahi ya nchi.
Aliongeza kuwa hakuna haja ya kufikishana mahala kuwa kila mmoja anakuwa na wasiwasi wa maisha yake kitendo ambacho kinaenda kinyume na mafundisho ya Mtume Mohamad (SWA).
“Tanzania ni nchi kongwe na haikuanza leo pia ni sawa na gunia ambalo limekusanya watu wengi wa dini mbalimbali  na wasio na dini hivyo ni vema watu wakajenga ustaarabu wa kuvumiliana”alisema Alhaj Mwinyi.
Alhaj Mwinyi alisema wajibu wa Waislam ni kuhakikisha wanaishi kwa amani na watu wengine ambao hawajawaingilia na kutaka kuwafuta katika nchi hii.
Vilevile ieleweke wazi kuwa hakuna anaweza kumfuta mwenzake katika kile anachokiamini hivyo ni vema kila mtu akajifunza kumvumilia mwingine.
Alisema kubwa ni kla mmoja kujizuia kumuingilia mwingine kwenye dini yake, kazi hiyo hakuna mwingine wa kuifanya bali ni Masheikh hao.
Aliwaasa Masheikh hao kuacha kushabikia mambo madogo ambako ushabibiki ukiendekezwa iko siku unaweza kuvuruga amani ya nchi hii.

No comments

Powered by Blogger.