Dkt. Alberic Kacou awataka watanzania kuacha dhuluma dhidi ya wanawake
Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa nchini Dkt. Alberic Kacou akisoma hotuba yake wakati wa maadhimisho ya siku ya wanawake duniani yaliyofanyika chuo kikuu cha Dar es Salaam ukumbi wa Nkurumah.(Picha na Dewji Blog)
Afisa Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa Tanzania Hoyce Temu (wa kwanza kulia) akiwa na baadhi ya wafanyakazi wenzake wa Mashirika mbalimbali ya Umoja wa Mataifa nchini waliojumuika katika sherehe za kuadhimisha siku ya wamawake duniani iliyofanyika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam katika Ukumbi wa Nkurumah.
Mwakilishi
wa UN Women Tanzania Bi. Anna Collins-Falk akizungumzia wakati wa
sherehe za maadhimisho ya siku ya wanawake duniani ambapo amesema
shirika litahakikisha linafanya kazi kwa ukaribu na serikali ya Tanzania
katika kutetea Haki za Wanawake.
Balozi wa
Ireland nchini Tanzania Mh. Fionnala Gilsenan aktioa neno la Shukrani
kwa wadau, wanafunzi na wafanyakazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa
waliohudhuria sherehe hizo.
Wajumbe wa
Chama cha Vijana wa Umoja wa Mataifa (YUNA) wakiongozwa na Jokate
Mwegelo(wa tatu kushoto)wakijadiliana na kutoa maoni juu ya adha
wanazokabiliana nazo wanawake wakati wa maadhimisho ya siku ya Wanawake
Duniani yaliyofanyika katika chuo kikuu cha Dar es Salaam.
Baadhi ya wakuu wa mashirika mbalimbali ya Umoja wa Mataifa waliohudhuria maadhimisho hayo.
Mratibu
Mkazi wa Umoja wa Mataifa nchini Dkt. Alberic Kacou (katikati) akiteta
jambo na Mwakilishi wa UN Women Tanzania Bi. Anna Collins-Falk wakati wa
maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani.
Mmoja wa
wadau wa masuala ya Haki za Wanawake akichangia maoni wakati wa sherehe
hizo zilizowakutanisha wanafunzi wa vyuo vikuu mbalimbali vya jijini Dar
katika Ukumbi wa Nkurumah wa Chuo kikuu cha Dar es Salaam.
Picha juu
na chini Baadhi ya wanafunzi wa vyuo mbalimbali jijini Dar na wadau wa
masuala ya Haki za Wanawake waliohudhuria sherehe hizo.
Baadhi ya
Wanfunzi wa vyuo mbalimbali wakijisajili kwenye chama cha vijana cha
Umoja wa Mataifa (YUNA) wakati wa sherehe za maadhimisho ya siku ya
wanawake duniani yaliyofanyika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ukumbi wa
Nkurumah.
It’s a womens Day take care of us…….lol……Wajumbe wa YUNA Tanzania.
Wananchi
wa Tanzania na watu wote duniani kwa ujumla wametakiwa kuwa na mikakati
endelevu itakayohakikisha inatokomeza uhalifu na dhuluma wanazofanyiwa
wanawake yakiwemo matendo ya kubakwa, kupigwa, kunyanyaswa, kunyimwa
haki na mengine ya aina hiyo.
Akizungumza
wakati akifungua mdahalo juu ya matatizo yanayowakumba wanawake wakati
wa Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani uliofanyika katika ukumbi wa
Nkurumah wa Chuo Kikuu cha Dar Es Salaam, Mratibu Mkazi wa Umoja wa
Mataifa Dkt. Alberic Kacou amesema wakati umefika sasa kwa dunia
kuonyesha kumjali mwanamke kwani katika utekelezaji wa shughuli nyingi
za kimaendeleo, uchumi na kijamii mwanamke anahusika.
Ametolea
mfano nchini Tanzania takwimu za mwaka 2010 zinaonyesha zaidi ya
theluthi moja ya wanawake wote sawa na asilimia 39 wamewahi kukumbana
shambulio la kimwili mpaka kufikia miaka 15.
Dkt kacou
ameongeza kuwa theluthi mija ya wanawake sawa na asilimia 33 wameshapata
mateso ya kufanyiwa vurugu katika kipindi cha miezi 12 iliyopita.
Amesema
siku hii ya Wanawake duniani inasherehekewa rasmi kwa sababu kwanza
tunatambua kuwa maendeleo, michakato na ustawi kunahitaji ushiriki hai
wa kiusawa na kuhusishwa kwa wanawake, pili kwa sababu tunakubali kuwa
Amani na Usalama wa Kimataifa unaweza tu kufikiwa kuwa kuwashirikisha
wanawake.
Katika
mdahalo huo washiriki mbali mbali walipata fursa ya kutaza filamu mbili
tofauti zinazoonyesha matatizo yanayowapata wanawake na baada ya hapo
walijadiliana na kutoa maoni na mapendekezo kadhaa.
Kauli mbiu ya Siku ya Wanawake Duniani kwa mwaka 2013 ni “ Uelewa wa Masuala ya Jinsia Katika Jamii; Ongeza Kasi
Post a Comment