KESI YA LADY JAYDEE YAHAIRISHWA TENA MPAKA AGOSTI 2, 2013
Lady Jaydee (kulia) akiwa na Prof. Jay (kushoto) pamoja na Gadna (kwa nyuma) wakiwa wanatoka mahakamani leo
Lady Jayde akiwa anatoka nje ya mahakama
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kinondoni, leo imeiaharisha kesi inayomkabili msanii wa kizazi kipya nchini, Judith Wambura 'Lady Jaydee' a.k.a Annaconda dhidi ya uongozi wa Clouds Media Group hadi Agosti 2, mwaka huu.
Endelea kusoma habari hii kwa kubofya hapa
Kesi hiyo ya madai iliyopo mbele ya Hakimu
Athumani Nyamlani, leo ililetwa kwa ajili ya kusikilizwa lakini ilishindikana
kutokana na wakili anayemtetea, Jaydee kutotokea mahakamani hapo na kumtuma
mwakilishi wake.
Ilidaiwa mahakamani hapo kuwa wakili huyo wa
Jaydee, amekwenda katika Mahakama Kuu kuhudhuria kesi nyingine na hivyo
kushindwa kufika mahakamani hapo kuendelea na kesi hiyo na hivyo kuahirishwa
hadi Agosti 2, mwaka huu.
Kesi hiyo ya madai ilipelekwa mahakamani hapo na
Mkurugenzi wa Utafiti na Maendeleo wa Kampuni ya Clouds Media kwa madai ya
kuukashifu uongozi huo.
Kwa mujibu wa mdai huyo, ambaye ni uongozi wa
Clouds Media ulidai kuwa mdaiwa huyo ambaye ni Lady Jaydee aliandika maneno ya
kuukashifu uongozi huo kupitia blogu yake.
Post a Comment