UPDATES: BABA WA WEMA SEPETU AFARIKI DUNIA LEO

Taarifa iliyotufikia asubuhi hii,inaeleza kuwa Balozi Issac Abraham  Sepetu ambaye pia ni Baba mzazi wa Miss Tanzania 2006,Wema Sepetu.Amefariki Dunia asubuhi ya leo kwenye Hospitali ya TMJ Mikocheni jijini Dar es Salaam.

Taarifa za awali zinasema kuwa,Balozi Sepetu alikuwa amelazwa katika hospital ya TMJ alikokuwa akitibiwa ugonjwa wa Kisukari na kiharusi uliokuwa ukimsumbua.

Hadi Mauti yanamkuta,Balozi Isaac Sepetu alikuwa ni Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya Uwekezaji wa Vitega Uchumi Zanzibar.

Tunaungana na Waombolezaji wote wa Msiba huu na Mwenyezi Mungu Mwingi wa Rehma na Mwenye Kurehemu,Aiweke Mahala Pema Peponi Roho ya Marehemu Balozi Isaac Abraham Sepetu.

UONGOZI WA MTANDAO WA PAMOJA UNATOA POLE KWA FAMILIA, NDUGU NA JAMAA KWA KIPINDI HIKI KIGUMU


No comments

Powered by Blogger.