MAREHEMU MZEE GURUMO AZIKWA KIJIJI CHA MASAKI ALIKOZALIWA
Muigizaji wa filamu, Jacob Stephen na mwenzake Dude wakisaidia kuubeba mwili wa Mzee Gurumo
Maelfu ya wananchi na watu mbalimbali maarufu wamejitokeza kwenye
mazishi ya muimbaji mkongwe wa muziki nchini, Mzee Muhidin Gurumo
yanayofanyika katika kijiji cha Masaki wilayani Kisarawe, Pwani. Kwa
mujibu wa makamu wa rais wa shirikisho la muziki Tanzania, Samwel
Brighton, ushiriki kwenye mazishi huo ni mkubwa ambapo mkuu wa wilaya
hiyo amewasaidia kwa kiasi kikubwa katika kuweka mambo sawa.
“Ushiriki kwa upande wa dansi watu wote walikuwepo
kwasababu kama unavyojua huyu ni baba wa muziki huo na wa maigizo
tulikuwa nao wengi tu lakini kwa upande wa kizazi kipya kusema ukweli
kwa macho yangu sidhani kama nimeona zaidi ya wasanii 10, sijajua tatizo
ni nini lakini ushiriki wao ni mdogo kwakweli,” Brighton amekiambia
kipindi cha Power Jams cha East Africa Radio.
ENDELEA KUTIZAMA TUKIO HILI KWA KUBOFYA HAPA CHINI
Wananchi wakimzika Mzee Gurumo katika kijiji cha Masaki, Kisarawe
Mzee
Gurumo alifariki Jumapili baada ya kulazwa kwenye hospitali ya taifa ya
Muhimbili jijini Dar es Salaam. Amewahi kuimba na bendi mbalimbali
zikiwemo Kilwa Jazz Band, Nuta Jazz Band, Mlimana Park, Safari Sound na
baadaye Msondo Ngoma.
Profesa Jay ni miongoni mwa wasanii waliohudhuria mazishi hayo
KAMA UNATAKA KUSOMA HISTORI YAKE BOFYA HAPA
Post a Comment