MWANAMKE ACHOMWA KISU MGONGONI AKIDAIWA KUCHUKUA MUME WA MTU MKOANI TABORA

 Mariamu Hussein akiwa na hali mbaya baada ya kuchomwa kisu mgongoni na kwenye paja wakati alipovamiwa na mwanamke mmoja ambaye inadaiwa kuwa Mariamu alikuwa na mahusiano ya kimapenzi na mume wa mwanamke huyo.Katika mkasa huo ilielezwa kuwa Mariamu akiwa nyumbani kwao ghafla alifika mwanamke huyo na kudai kuwa amekuja
kutekeleza mauaji kwa kile kilichofahamika kuwa amekuwa akivumilia kwa muda mrefu kuchukuliwa mume wake pasipo kuleta fujo yeyote jambo ambalo lilionesha unyonge wa hali ya juu kwa mwanamke huyo ambaye alifika nyumbani hapo na kucharuka kama Mbogo aliyejeruhiwa na kuanza kufanya unyama huo.

 ENDELEA KUSOMA HABARI HII KWA KUBOFYA HAPA CHINI

 Mwanamke aliyefanya unyama huo,alilazimika kukimbizwa Kituo Kikubwa cha Polisi Tabora,.Mariam akiwa hoi taabani huku damu ikiendelea kububujika kwenye jeraha kubwa la mgongoni.  Mpini wa kisu alichochomwa Mariamu ambapo inasadikiwa Mwanamke huyo baada ya kumpiga kisu cha mgongoni na kuingia,kilikatikia mgongoni na kumfanya Mariamu azidiwe na kupoteza fahamu

PICHA NA JUMA KAPIPI

No comments

Powered by Blogger.