SOMA HAPA UJUE SIRI YA KUISHI MAISHA MAREFU


WATAFITI wa nchini Israel walibaini kuwa, mtu anayekunywa chai mara kwa mara ana uwezo wa kuishi muda mrefu tofauti na yule asiyependa chai.

Aghalabu maisha ya mwanadamu yeyote yule yapo mikononi mwa muumba wake, ambaye hujua lini muda wa kuishi wa kiumbe wake utakwisha. Lakini mtindo wa maisha yetu usiojali kanuni za afya, umeonyesha kuwa ndicho chanzo cha watu wengi kuishi maisha mafupi.

Kiwango cha maisha ya binadamu sasa kinapunguzwa kutokana na mabadiliko ya tabianchi, mtindo wa maisha na mazingira, lakini wanasayansi na wataalamu wa afya wamekuja na mbinu ambazo zinatajwa kusaidia kuongeza miaka yako ya kuishi.

KUNYWA CHAI; Watafiti wa nchini Israel walibaini kuwa, mtu anayekunywa chai mara kwa mara ana uwezo wa kuishi muda mrefu tofauti na yule asiyependa chai.

Chai, hasa ya kijani (green tea) ina ondoa sumu iitwayo ‘polyphenols’ ambayo husaidia mwili wako kupambana na magonjwa ya moyo. Wataalamu hao wanasema, chai iliyochemka vizuri au pakiti ya majani ya chai kukorogwa vyema katika majimoto, yafaa zaidi. Kwa kifupi, chai ikolee majani.

ENDELEA KUSOMA ,MAKALA HII KWA KUBOFYA HAPA CHINI

KUSIMAMA KWA MGUU MMOJA KILA ASUBUHI; Inaweza kuonekana kuwa ni jambo la ajabu, lakini wanasayansi wamebaini kuwa kusimama kwa mguu mmoja asubuhi kunasaidia kuimarisha misuli ya mgongo, nyonga na tumbo na kuupa uwiano uti wa mgongo.


Mtaalamu wa viungo anasema, zoezi hili jepesi likifanywa kila siku, linatoa manufaa ya muda mrefu na linakukinga kuvunjika mifupa kwa urahisi hasa unapoanza kuzeeka. Tafuta marafiki sita unaowaamini Kuwa na marafiki wazuri na familia ambayo unaiamini ni siri moja kubwa ya kuishi miaka 100.

Utafiti uliofanywa na kitengo cha Maisha na Mazingira katika Chuo Kikuu cha Australia, ulionyesha kuwa kupata watu wa kukupa msaada na kukufariji wakati wa huzuni kunasaidia kuongeza umri wa kuishi kwa kuzalisha kemikali ya ‘furaha’ inayofahamika kama dopamine na oxtocyin ambavyo huusaidia ubongo.

Mwanasaikolojia wa Chuo Kikuu cha Dodoma, anasema unapokuwa na tatizo, kisha ukalihifadhi moyoni, unaunda uchungu ambao unakuathiri. Anasema, mwili wa mtu unaathiriwa kutokana na tabia au matendo ya moyoni, unapohifadhi tatizo bila kupata ushauri unakuza tatizo hilo.

“Marafiki au hata ndugu wa kumweleza tatizo lako ni muhimu, wanaweza kukupoza,” anasema

USISHIBE SANA; Wakazi wa kisiwa cha Okinawa, nchini Japan, wanaongoza kwa kuwa na kiasi kidogo cha watu wenye unene uliopitiliza (obesity) na wanasifika kwa kuwa na idadi kubwa ya watu wanaoishi zaidi ya miaka 100. Siri yao kubwa ni kuwa hawali wakashiba kwa zaidi ya asilimia 80.


Watafiti wa Marekani pia, wamebaini kuwa, binadamu wanaweza kuishi miaka mingi zaidi iwapo chakula wanachokula kinapunguzwa kwa robo tatu. Ina maana kwamba kula kidogo kunaufanya mwili wako usiwe na kazi kubwa ya kumeng’enya, hivyo kuupa nafasi ya kuwajibika na kazi nyingine.

Mtaalamu wa chakula na lishe, anasema, mtu hatakiwi kula akashiba bali anatakiwa aache njaa kwa mbali ili kutoa nafasi ya maji na mmengenyo kuchukua nafasi.

LALA KWA MUDA MREFU; Ukosefu wa usingizi unakuweka katika hatari kubwa ya kupata maradhi ya msongo wa mawazo na moyo. Kupata makunyanzi na mwili kuchoka.


Mabadiliko kidogo tu ya kitabia yanaweza kuleta mapinduzi makubwa katika afya yako. Wanaopata usingizi wa kutosha si rahisi kupatwa na kiharusi au shinikizo la damu.

PIGA MSWAKI


Maradhi ya fizi, ni maradhi yaliyopata umaarufu duniani. Dk James Russel wa kituo cha tiba cha Hope, anasema, meno na fizi ni chanzo cha magonjwa mengi ambayo wengi hudhani hayahusiani na afya ya kinywa. Maradhi ya fizi yanatajwa kuwa chanzo cha saratani za aina fulani, maradhi ya moyo, ubongo na hata kisukari.

KUWA MAKINI
Utafiti uliofanywa na Mwanasaikolojia wa nchini Marekani, Dk Howard Friedman unasema kuwa, umakini wa mtu ni kigezo cha urefu wa maisha yake. Watu ambao wapo makini na maamuzi, matumizi ya fedha na ambao wanapenda kuweka kila kitu sawa na kufanya mambo yao kwa uangalifu, wanaweza kuishi kwa muda mrefu.


KWA NINI? Dk Kitila Mkumbo, Mwanasaikolojia wa Chuo Kikuu Kishiriki cha Elimu (DUCE) anasema, unapokuwa makini unafanya uamuzi mzuri ambayo hupunguza kiwango cha kuishi maisha hatarishi.

“Umakini unamsaidia mtu kuepuka tabia hatarishi kwa mfano ngono zembe, kuvuta sigara, mambo ambayo yanahatarisha afya,” anasema.

Anasema, mtu anayepangilia mambo yake na kuwa makini kwa mfano kutumia kinga wakati wa tendo la ndoa kunakuepusha na maambukizi ya maradhi mbalimbali.

USIWEKE MATUNDA KWENYE JOKOFU Unaweza kufikiri kuwa, kuyaweka matunda katika jokofu, unayafanya yadumu kwa muda mrefu, lakini tafiti zinaonyesha kuwa, matunda yaliyopoozwa kwa baridi ya jokofu, yanapungukiwa vitamini muhimu kuliko matunda yanayowekwa katika hali ya kawaida.


Kwa mfano, nyanya na pilili ni vyema kuwekwa katika bakuli kuliko katika jokofu. Matunda mengi yanasaidia kuondoa sumu mwilini hivyo lishe zake zikibaki bila kuharibiwa, husaidia kujenga moyo imara na kupunguza kiwango aina fulani za saratani.

KUFANYA TENDO LA NDOA ANGALAU MARA MBILI KWA WIKI
Utafiti mkubwa na uliothibitishwa wa Welsh na wenzake wa Hospitali ya Royal Edinburgh, Uingereza ulibaini kuwa wale wanaofanya mapenzi mara moja kwa mwezi wapo katika hatari ya kufa mapema, ukilinganisha na wale wanaofanya mapenzi mara mbili kwa wiki.

Welsh anasema, tendo la ndoa linapunguza msongo wa mawazo na kumfanya mtu apate usingizi mzuri. Msongo wa mawazo unasababisha maradhi ya moyo na kisukari. Dk Mkumbo anasema, tendo la ndoa ni jambo la afya na husaidia katika kupunguza msongo wa mawazo na kuupa mwili uchangamfu. Hata hivyo Dk Mkumbo anasema hajawahi kusikia idadi ya siku za kufanya mapenzi kama ni mara moja au mbili kwa wiki, bali anaamini kitendo chenyewe kina umuhimu wake kiafya.

Kwa nini Wajapan wanaishi maisha marefu? Inaelezwa kuwa Wajapan ni taifa linaloongoza kwa kuwa na watu wanaoishi muda mrefu kuliko mataifa mengine. Takwimu za Shirika la Afya Duniani zinaeleza kuwa, raia wa Japan wanaishi maisha marefu zaidi. Kwa mfano, mwanaume mzee kuliko wote aliyevunja rekodi ni Jiroemon Kimura, kutoka Kyotango, Kyotto, Japan aliyefariki dunia akiwa na umri wa miaka 116. Siri yao kubwa ni kula chakula chenye afya ikiwemo samaki badala ya nyama nyekundu.


Hawanywi maziwa, au bidhaa zozote za ng’ombe. Nafaka jamii ya soya ambazo zinasaidia kuondoa maradhi ya moyo. Wanakunywa chai kwa wingi, hasa ya kijani, wanakula kiasi kidogo cha chakula, hawatumii magari mara kwa mara na wanatumia vyoo vya kuchuchumaa badala ya vya kukaa.

No comments

Powered by Blogger.