MSIKITI WA HINDU ULIOPO MTAA WA KIBASILA JIJINI DAR WATEKETEA KWA MOTO

 Kikosi cha zima moto kikifanya juhudi za kuzima moto huo.
MSIKITI wa madhehebu ya Wahindu uliopo maeneo ya Mtaa wa Kibasila karibu na shule ya Olimpia jijini Dar es Salaam, umeteketea kwa moto leo asubuhi ambapo baadhi ya mali zimeungua na mtu mmoja kukimbizwa hospitali kutokana na mshituko.

 Sehemu ya chumba cha msikiti kilichoungua.
Akizungumza na mtandao huu, shuhuda mmoja alisema moto huo umesababishwa na hitilafu ya umeme iliyoanzia kwenye mashine ya luku ambapo baadhi ya waumini walikuwa wakijiandaa  kuupamba msikiti huo.

ENDELEA KUTIZAMA TUKIO HILI KWA KUBOFYA HAPA CHINI


 Wananchi wakiwa katika eneo la tukio wakisaidia kuokoa baadhi ya mali zilizopo ndani ya msikiti.
 Gari la kikosi cha zima moto likiwa eneo la tukio kuuzima moto.
Baadhi ya waumini wakiwa eneo la tukio.
Baadhi ya mali zilizookolewa.

NA GPL

No comments

Powered by Blogger.