UTAFITI: HIZI NDIZO DALILI ZINAZOONESHA KWAMBA MPENZI WAKO AMEANZA MAHUSIANO NA MTU MWINGINE


Mwaka 2012 ulifanyika utafiti Uliogundua kwamba asilimia 30 mpaka 50 (30%-50%) ya wanawake wangekubali kuwa na mwanaume mwingine endapo tu watathibitishiwa kwa asilimia mia moja (100%) kwamba wapenzi wao hawatajua! Utafiti ambao haukufanikiwa kwa upande wa wanaume ambao wengi wao hawakutaka kuwa wakweli! Ukweli ni kwamba hakuna kinacholeta aman moyoni kama uhusiano usio na udanganyifu!

Lakini suala linaloulizwa na watu wengi ni je, ntajuajuaje mpenzi wangu ananidanganya?  Usihofu Tumekuandalia ishara hizi muhimu kujua mpenzi wako anakudanganya.

ONYO: Usimuhukumu mtu kwa ishara moja tu na kufanya hitimisho kuwa ameanza mahusiano na mpenzi mwingine. Kumbuka dalili hizi kila moja ni onyo tu na tumia zaidi ya moja kugundua kama anakudanganya.

DALILI ZA WANAWAKE WADANGANYIFU
1.Anakuwa mkali kujibu maswali rahisi, Wakati mwingine hukuuliza kwanza wewe kabla ya kukujibu!
 Kisaikolojia hii huonesha ni akili ya kutaka kusema uongo. Mfano; umetoka wapi usiku huu? Jibu: kwan nini unaniuliza swali kama hilo? Au hujui kama leo ni birthday ya janet? Au pengine kwanini unanifuatilia siku hizi? Hiyo ni taa nyekundu.

ENDELEA KUSOMA MAKALA HII KWA KUBOFYA HAPA CHINI


2. Umuhimu wako anapungua kwake, Hujali zaidi Muonekano wake kuliko zamani, na hutumia muda mwingi kujiremba hasa anapotoka peke yake!
  Utagundua vile vitu alivyozoea kukuomba, kukuuliza, na kukushirikisha havipo tena. Unafikiri havipo tena? Hapana!  Vipo ila kuna mtu mwingine anayeulizwa au kushirikishwa kwenye masuala hayo. Inawezekana alikuwa akirudi nyumbani anakusimulia siku yake ilivyokuwa, changamoto nk lakini sasa ukimuuliza  siku yako iliendaje hugeukia pembeni na kujibu kwa jibu moja tu “nzuri” na kutumia muda wake mwingi kujiremba.

3.Kuna Rafiki mpya kajitokeza na Siku hizi na hataki tena kuwa karibu na ndugu/ rafiki zako
Mara chache anaweza kukutambulisha kwa rafiki huyu mpya, anaweza kusema ni mfanyakazi mwenzangu, mwanafunzi mwenzangu, au hata ni rafiki yangu tulipotezana muda mrefu!
 Cha ajabu ni kwamba, hupenda kumlinda na kusimama upande wake na kuwa mkali unapotaka kujua zaidi kuhusu rafiki huyu mgeni. Hatotaka pia ujue anakaa wapi, jina lake halisi nk!

4.Hapendi ujue ratiba yake, anataka ajue yako! Hataki umsindikize tena, anataka aende na rafiki zake! Neon “sisi” hubadilika na kuwa “mimi”
Hupendelea zaidi kukuuliza ratiba yako na kutokupa nafasi ya kuingilia ratiba yake. Hufanya hivi ili kujua atakuwa huru kiasi gani kufanya mambo yake. Na sehemu alipopenda kuweka neon sisi hubadilika na kuwa mbinafsi zaidi “mimi”. Hii hutokea hata anapozungumzia mambo yajayo.

5. Simu yake imekuwa kitu cha siri, na  huweka password (Haikuwa tabia yake)
Unapoona mpenzi wako kaanza kuwa mkali unapotaka kugusa simu yake, au hutoa sababu ya haraka akikuta tu umeshika simu yake (mfano hebu nipe mara moja nimpigie mama) hii sio dalili nzuri. Pia akitoka huchukua muda mrefu kupokea simu au kuacha ikate ndo akupigie, hii inawezekana anatafuta sehemu nzuri akae ndipo apokee simu hiyo ili usijue yuko wapi! Wakati mwingine hutoka na kwenda kuongelea mbali mnapokuwa pamoja, au hata kuacha simu nyumbani mnapotoka.

DALILI ZA WANAUME WADANGANYIFU

1.Haachi Simu yake muda wowote
Umeacha kuiona simu yake mezani akiwa hayupo? Kuna muda anaweza kuingia nayo mpka bafuni! Hutoa sababu kama “nasoma sana habari kutumia simu yangu” au kuna taarifa muhimu nataka kufuatilia siwezi acha simu yangu,hutoa sababu ya haraka akikuta tu umeshika simu yake (mfano hebu nipe mara moja nimpigie bosi nilikuta missed call yake) hii sio dalili nzuri.

2.Huwa Msiri na hataki ujue mambo yake huwa mkali sana unapoonesha kuumdadisi
Moja Ya Silaha za wanaume ni Kukutishia pale anapoona unaingia sana kwenye maisha yake binafsi. Huwa mkali sana unapomuuliza kuwa alikuwa wapi au kujua ratiba zake.

3.Kuna Rafiki mpya kajitokeza na pengine kutajwa mara kadhaa
Mara chache anaweza kukutambulisha kwa rafiki huyu mpya, anaweza kusema ni mfanyakazi mwenzangu, mwanafunzi mwenzangu, au hata ni rafiki yangu tulipotezana muda mrefu. Cha ajabu ni kwamba, hupenda kumlinda na kusimama upande wake na kuwa mkali unapotaka kujua zaidi kuhusu rafiki huyu mgeni. Hatotaka pia ujue anakaa wapi, jina lake halisi nk!

4.Safari zinaongezeka, na hataki muwe pamoja
Mpenzi wako kaongeza safari, pengine za kwenda mji  jirani kila weekend, au hataki kufuatana na wewe kama zamani, Hataki umsindikize stendi/airport au bandarini (pengine alikokuaga anaende sio anakokwenda) Huja amechoka na hataki kuwa karibu na wewe.

5.Anakutuhumu sana kwamba una mpenzi mwingine (Iwapo tu huna mpenzi mwingine)
Hii ni njia nyingine wanaume huitumia kujihami pale anapoona unaweza kumhisi anauhusiano na mpenzi mwingine. Hii humfanya mwanamke aogope kuzungumzia suala la udanganyifu kwenye uhusiano wao kwani akizungumzia tu, kibao kitageuka na kuanza kutuhumiwa yeye.

USHAURI
Hata hivyo, binadamu tunatofautiana hivyo usimuhukumu mtu kwa kuona ishara moja tu ambayo inaweza kutokana na mabadiliko mbalimbali ya kimaisha kama, maisha magumu, kazi, shule, magonjwa nk. Cha muhimu ni kuhakikisha  unatimiza wajibu wako kwa asilimia mia moja (100%) kwani pengine hii ndio sababu ya yeye kuwa na mpenzi wa nje. Pia ni jukumu lenu wote wawili kuonyesha. BAKI NJIA KUU MICHEPUO SIO DILI

NA  KUMI MUHIMU

No comments

Powered by Blogger.