GARI LILOLOBEBA MITIHANI LACHOMWA MOTO, POLISI AJERUHIWA VIBAYA NCHINI KENYA

Ndugu wasomaji wetu tunaomba support yenu kwa kutangaza nasi hapa kwenye hii blog kwa bei nafuu ili tuweze kuendelea kutoa habari bila tatizo lolote. Wasiliana nasi kupitia namba +255713363965 / +255755274953. Tunashukuru kwa ushirikiano wenu. 


AFISA wa polisi alijeruhiwa vibaya na wenzake 7 wakatoroka waliposhambuliwa wakisindikiza gari lililobeba karatasi za mtihani wa KCSE katika Kaunti ya Turkana.

Maafisa hao 8 walikuwa wakisindikiza gari hilo kupeleka karatasi za mtihani shule ya mseto ya Kapendo waliposhambuliwa na watu wasiojulikana.


Baada ya maafisa hao kutoroka, wavamizi waliteketeza gari hilo. Kulingana na mwakilishi wa wanawake wa kaunti ya Turkana Bi Joyce Emanikor, gari hilo lilishambuliwa eneo la Kasarani kati ya vituo vya biashara vya Lomelo na Kapedo.


“Hatukuamini tulipopokea habari hizo tukisherehekea sikukuu ya Mashujaa Dei katika Lokori. Tulipata habari hizo muda mfupi kabla ya mkuu wa wilaya kusoma hotuba ya Rais Uhuru Kenyatta,”  akasema Bi Emanikor.

ENDELEA KUSOMA HABARI HII KWA KUBOFYA HAPA CHINI
Aliongeza kuwa kuna hali ya taharuki katika eneo hilo lililo karibu na mpaka wa Kaunti ya  Baringo akisema matokeo yatakuwa mabaya kwa sababu ya ukosefu wa usalama eneo hilo.


“Wanakijiji wanalazimika kukaa ndani ya nyumba. Kila gari linashambuliwa na shughuli zimeathirika na uhaba wa chakula unatarajiwa eneo hili,” akasema.


Kisa hicho kinajiri siku moja baada ya shule nne karibu na mpaka huo kufungwa kwa muda usiojulikana kufuatia mashambulizi ya mara kwa mara.


Mwalimu mkuu wa shule ya msingi ya Kapedo Bw Joseph Emoit Ekorukou kwa wakati huu amelazwa katika hospitali ya  St Lukes mjini Eldoret baada ya kujeruhiwa kwenye shambulizi Ijumaa iliyopita. Shambulio hilo lilifanya walimu kulalamika. 

Walimu Kususia kazi

29 wa shule ya upili mseto ya  Kapedo, shule ya msingi ya wasichana  ya Kapedo, shule ya msingi ya Lomelo  na shule ya msingi ya mseto ya  Kapedo waliamua kususia kazi hadi hali ya usalama irejeshwe eneo hilo.


Watahiniwa wote 25 kwa sasa wamewekwa chini ya ulinzi mkali wa maafisa wa GSU. Mkurugenzi wa Elimu wa kaunti hiyo Dkt   Nichodemus Anyang aliwasiliana na Baraza la Mitihani nchini  na kusema wanajadili uwezekano wa kutuma karatasi kwa ndege au kuhamishia watahiniwa eneo salama huko Lokori.


Mwalimu Mkuu wa shule hiyo Daniel Namunwa alisema watahiniwa hao wameshtusha na tukio hilo.

No comments

Powered by Blogger.