MH. MBOWE ATOA UFAFANUZI KUHUSU SUALA LA PICHA ZAKE AKIWA NA MKE WAKE KUSAMBAA MITANDAONI
Ndugu wasomaji wetu tunaomba support yenu kwa kutangaza nasi hapa kwenye hii blog kwa bei nafuu ili tuweze kuendelea kutoa habari bila tatizo lolote. Wasiliana nasi kupitia namba +255713363965 / +255755274953. Tunashukuru kwa ushirikiano wenu.
Mbowe Ameongea haya Kuhusu hizo kwa kusema "Kwanza mke wangu alikuwa anatimiza umri wa miaka 50 ya kuzaliwa,
vilevile firstborn wetu Dudley alikuwa amemaliza shahada yake ya kwanza
Chuo Kikuu cha Sussex, Uingereza, kwa mambo hayo mawili, tuliona ipo
haja ya kufanya sherehe, ukizingatia watoto wetu wengine wawili Nicole
na Denis walikuwa wamerejea nchini kwa sababu nao wanasoma nje ya nchi."
Siku hiyo ya tukio ilikuwa Jumapili, tulianza kwa kwenda kanisani
Azania Front tukatoa sadaka, baada ya hapo tulikwenda Serena Hotel
kwenye Ukumbi wa Kivukoni ambako chakula cha mchana kilikuwa
kimeandaliwa, tukajumuika na ndugu wengine pamoja na marafiki.
Haikuwa sherehe tu kusema labda nilikurupuka kumbusu mke wangu,
ilikuwa sherehe ya kifamilia, kumpongeza mke wangu na mtoto wetu,
alisema Mbowe.
Post a Comment