NI MIAKA SABA SASA TOKA MSANII WA REGGAE MAREHEMU LACKY DUBE KUFARIKI DUNIA TAREHE 18/10/2007, SOMA HAPA HISTORIA YAKE

Ndugu wasomaji wetu tunaomba support yenu kwa kutangaza nasi hapa kwenye hii blog kwa bei nafuu ili tuweze kuendelea kutoa habari bila tatizo lolote. Wasiliana nasi kupitia namba +255713363965 / +255755274953. Tunashukuru kwa ushirikiano wenu. 

Lucky Philip Dube  alizaliwa tarehe 3 Agosti 1964 na kufariki tarehe 18 Oktoba 2007 alikuwa mwanamuziki wa reggae kutoka Afrika Kusini. Alirekodi albamu 22 katika lugha ya KizuluKiingereza na Kiafrikaans katika kipindi cha miaka 25-na alikuwa mwanamuziki wa Reggae kutoka Afrika Kusini ambaye aliuza albamu nyingi kabisa.Dube aliuawa katika kitongoji cha Rosettenville huko Johannesburg jioni ya 18 Oktoba, mwaka 2007.

Maisha Yake ya Utotoni

Lucky Dube alizaliwa Ermelo, zamani lilikuwa eneo la Transvaal ya Mashariki, na sasa ni sehemu ya Mpumalanga, tarehe 3 Agosti 1964. Wazazi wake walitalikiana kabla ya yeye kuzaliwa na alilelewa na mamake, Sarah, ambaye alimpa jina hilo kwa sababu alichukulia kuzaliwa kwake kama bahati baada ya mimba nyingi kutoka.  Pamoja na ndugu zake wawili, Thandi na Patrick, kwa kipindi cha muda mrefu utotoni mwake Dube aliishi na nyanyake wakati mamake alihamishwa kufanya kazi sehemu nyingine. Kwenye mahojiano ya mwaka 1999 alimsimulia nyanyake kama "mpenzi wake wa dhati" ambaye "alizidisha vitu vingi kumkuza kuwa mtu wa kuwajibika aliye sasa." 

ENDELEA KUSOMA HISTORIA HII KWA KUBOFYA HAPA CHINI

Kuanza Uwanamuziki wake

Utotoni mwake Dube alilima lakini, alipokuwa mtu mzima, na kutambua kwamba hakuchuma pato la kumwezesha kulisha familia yake, alianza kuenda shuleni. Akiwa shuleni alijiunga na kwaya, pamoja na marafiki wengine, na kuunda kikundi chake cha kwanza cha waimbaji kilichoitwaThe Skyway Band. Alipokuwa shuleni aligundua kuhusu harakati za Rastafara. Akiwa na umri wa miaka 18 Dube alijiunga na bendi ya binamu yake, The Love Brothers, iliyoimba muziki wa pop kwa lugha ya Kizulu zilizojulikana kama mbaqanga huku akiyakimu maisha yake kwa kufanya kazi na kampuni ya Hole and Cooke kama mlinzi kwenye mnada wa magari huko Midrand. Bendi hiyo iliinga kwenye mkataba na kampuni ya Teal Record, chini ya Richard Siluma (Baadaye Teal iliunganishwa na Kampuni ya Gallo Record). Ingawa bado Dube alikuwa shuleni, bendi hiyo ilirekodi katika mji wa Johannesburg wakati alikuwa likizoni. Albamu waliotoa iliitwa kwa jima la Lucky Dube and the Supersoul. Albamu ya pili ilitolewa muda mchache baadaye, mara hii kando na kuimba Dube alitunga misitari. Ni wakati huu ambao alianza kujifunza Kiingereza.

Kuhamia rege

Baada ya kwa albamu yake ya tano ya Mbaqanga, Dave Segal (ambaye badaye alikuwa mhandisi wa sauti ya Dube) alimshauri aachane na jina la "Supersoul". Albamu zingine zot zilizofuata zilirekodiwa kama Lucky Dube. Wakati huu Dube alianza kugundua kwamba mashabiki walifurahishwa na baadhi ya nyimbo za rege alizoimba kwenye hadhara. Aliweza kuvutiwa na Jimmy Cliff na Peter Tosh,  alihisi kwamba ujumbe wa masuala ya kijamii na kisiasa uliohusishwa na rege ya kutoka Jamaica ingefaa kwa hadhira ya Afrika Kusini jamii ambayo ubaguzi wa rangi(usarangi) ulikuwa umekithiri. 
Aliamua kujaribu mtindo huu mpya wa muzikina katika mwaka wa 1984, alitoa albamu ndogo ya Rastas Never Die. Mauzo ya rekodi hiyo yalikuwa mabaya - idadi ilikuwa karibu 4000- ikilinganishwa na 30000 ambayo rekodi yake ya mbaqanga zingeuzwa. Serikali ilyoeneza usarangi (ubaguzi wa rangi), ikiwa na nia ya kukomesha haraki dhidi ya ubaguzi wa rangi, ilipiga marufuku albamu hiyo mwaka 1985. Hata hivyo, hakuvunjika moyo na aliendelea kuimba nyimbo za rege hadharani na akatoa albamu ya pili ya rege. Fikiria About The Children (1985). Ilifanikiwa kupata hali ya mauzo ya zaidi ya milioni na kumfanya Dube kuwa mwanamziki wa rege maarufu Afrika Kusini, mbali na kuvutia watu nje ya nyumbani kwao. 

Mafanikio muhimu na ya kibiashara

Dube aliendelea kutoa albamu zilizofanikiwa kibiashara. Mwaka 1989 alishinda tuzo nne za OKTV wimbo wa Prisoner, ulishinda nyingine na wimbo wa Captured Live ulishinda tuzo nyingine mwaka uliofuata na bado wimbo wa House Of Exile ulishinda tuzo mbili mwaka mmoja baadaye. Albamu yake ya mwaka 1993, Victims iliuza zaidi ya nakala milioni moja duniani kote. Mwaka 1995 alipata mkataba wa kurekodi duniani na na kampuni ya Motown. Albamu yake ya Trinity ilikuwa ya kwanza kutolewa na kampuni ya Tabu Records baada ya Motown  kujipatia kitambulisho hicho. 

Mwaka 1996 alitoa mkusanyiko albamu ya, Serious Reggae Business, ambayo ilimpelekea kuitwa "Mwanamziki wa Kiafrika mwenye mauzo bora zaidi" kwenye Tuzo la Wanamziki Duniani na "Msanii bora wa Mwaka" kwenye Tuzo la Wanamziki nchini. Albamu zake tatu zilizofuata zote zilishinda tuzo kwenye Tuzo la Wanamziki la Afrika Kusini.  Albamu yake ya hivi karibuni,Respect, ilipata nafasi ya kutolewa Ulaya na Kampuni ya Muziki ya Warner Musi.  Dube alizuru nchi nyingi, na kuimba kwenye jukwaa moja na wasanii kama vile Sinéad O'ConnorPeter Gabriel na Sting Alishiriki kwenye igizo la rege liitwalo Sunsplash mwaka 1991 (hali ya kipekee mwaka huo, alialikwa jukwaani tena na kuimba kwa muda wa dakika 25 akirudia) na onyesho la hadharani la 8 la mwaka 2005 mjini Johannesburg. 

Mbali na kuimba, wakati mwingine dube alikuwa muigizaji, alishiriki kwenye filamu za Voice In The Dark, Getting Lucky na Lucky Strikes Back

Kifo

Lucky Dube aliuawa katika kitongoji cha Rosettenville mjini Johannesburg tarehe 18 Oktoba 2007, muda mfupi baada kuwapeleka watoto wake wawili kati ya wote saba kando ya nyumba ya mjomba wao. |18 Oktoba 2007, muda mfupi baada kuwapeleka watoto wake wawili kati ya wote saba kando ya nyumba ya mjomba wao. Dube alikuwa akiendesha gari lake la aina ya Chrysler 300C ambayo kumbe ndiyo wauaji wake walikuwa wanataka. Duru za polisi zinaonyesha kuwa aliuawa kwa kupiga risasi na wezi wa magari. Wanaume watano wametiwa mbaroni kutokana na mauaji hayo Watu watatu wwalishitakiwa na kupatikana na hatia tarehe 31 Machi 2009; wawili walijaribu kutoroka lakini walishikwa. Watu hao walihukumiwa kifungo cha maisha.

Hiba

Tarehe 21 Oktoba 2008, Rykodisc alitoa albamu ya mkusanyiko kwa jina Retrospective, ambayo ilikuwa na nyimbo nyingi za kuvutia za Dube pamoja na traki nyingine ambazo hazikuwa zimetolea vilevile awali unreleased tracks katika Marekani. Albamu hiyo ilisifia muziki wa Dube na kuadhimisha mchango aliyotoa nchini Afrika ya Kusini



SOURCE: WIKIPEDIA

No comments

Powered by Blogger.