MH.HAMAD RASHID AWAASA WANAFUNZI KUJIUNGA NA MFUKO WA PENSHENI WA PSPF ILI KUPATA MIKOPO YA ELIMU NA MIKOPO YA KUANZIA MAISHA

Ndugu wasomaji wetu tunaomba support yenu kwa kutangaza nasi hapa kwenye hii blog kwa bei nafuu ili tuweze kuendelea kutoa habari bila tatizo lolote. Wasiliana nasi kupitia namba +255713363965 / +255755274953. Tunashukuru kwa ushirikiano wenu.


Mgeni rasmi Hamad Rashid ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Wawi kupitia CUF akizunguza na wanafunzi walioudhuria kwenye siku ya Career Day iliyofanyika kwenye viwanja vya chuo cha Biashara (CBE) jijini Dar es Salaam
Rais wa Serikali ya Wanafunzi Katika Chuo cha Biashara,(CBE),Ramadhani S Kirungi akiwakaribisha wageni mbalimbali katika siku ya "CAREER DAY" iliyofanyika katika viwanja vya Chuo hicho Jijini Dar es salaam
Afisa wa PSPF Hadji Jamadary akiwa anafafanua na kuelezea  kuhusu na uchangiaji wa hiari wa PSS kwa wanafunzi wa Chuo Cha Biashara (CBE) jijini Dar es salaam
Maseko Kodalo Afisa wa Mfuko wa pensheni Wa PSPF akiwa anatoa maelekezo ya kujiunga na mfuko huo kwa mpango wa lazima, Mikopo ya Elimu na mikopo ya kuanzia maisha.
Mgeni rasmi Mh. Hamad Rashid ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Wawi kupitia CUF akitolewa ufafanuzi kufusu kazi za mfuko wa PSPF na Afisa wa PSPF Hadji Jamadary (wa pili kutoka Kushoto)
Mbunge wa Jimbo la Wawi kupitia CUF, Mh. Hamad Rashid akiwa ndani ya banda la PSPF ambao walikuwa wadhamini wakuu katika Career Day
Mgeni rasmi Mh. Hamad Rashid ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Wawi kupitia CUF akipata ufafanuzi kutoka kwa wanafunzi wa Chuo kikuu cha biashara (CBE) wa kozi mbalimbali kuhusu kazi zao na maendeleo ya masomo yao.
Afisa wa PSPF Hadji Jamadary akitoa ufafanuzi kwa mmoja wa wanafunzi waliotembelea banda la mfuko wa PSPF.

Wanafunzi wakiwa kwenye banda la Mfuko wa PSPF wakipatiwa elemu kuhusu mikopo ya kuanzia maisha na fao la elimu.
Afisa wa  mfuko wa Pesheni (PSPF) Abdallah Ahamed akitoa maelekezo kwa mmoja wa wanachuo waliotembelea kwenye banda la PSPF
Wanafunzi wa Chuo cha Biashara (CBE) jijini dar es Salaam wakijaza fomu za kujiunga na mfuko wa PSPF
Baadhi ya washiriki ya washiriki wa Cereer Day
Baadhi ya wanafunzi walioweza kutembelea banda la PSPF na kuweza kulimishwa juu ya fao la elimuna mikopo ya kuanzia maisha wakitizama mtandao wa Mfuko huo kwa njia ya simu
Mgeni Rasmi na PSPF wakiwa kwenye picha ya pamoja na Baadhi ya viongozi wa Chuo cha Biashara (CBE)  jijini Dar 


Mbunge wa Jimbo la Wawi kupitia CUF Mh.Hamad Rashid ameupongeza mfuko wa pensheni wa PSPF kwa kuwa wadhamini katika Career Day ya Chuo cha biashara (CBE) iliyofanyika katika viwanja vya chuo hicho  siku ya ijumaa ambapo mbunge huyo aliweza kuwa mgeni rasmi wa tukio hilo na kuwapa hongera PSPF kwa kitendo cha kuweza kuwa pamoja na wanafunzi kwa ajiri ya kuwaandaa kuwa washiriki wazuri katika uchangiaji wa mafao mbalimbali na kuweza kupata mikopo ya elimu na ile ya kuanzia maishi

Rais wa Serikali ya Wanafunzi Katika Chuo cha Biashara,(CBE) Bw.Ramadhani S Kirungi amewashukuru wanafunzi wote walio weza kushiriki katika sherehe hizo kwani ni za kwanza toka chuo hicho kianze yapata miaka hamsini (50) hazijawahi fanyika lakini katika uongozi wake amepata bahati ya kuweza kuifanya siku hiyo, pia amewapongeza wanafunzi wa kozi mbalimbali walio weza kufanya maonesho katika viwanja vya chuo hicho kwaajiri ya kuwaonesha wahudhuriaji ufasaha wa masomo yao.

Pia Mfuko wa Pensheni wa  PSPF kupitia Maafisa wao walio weza kujitoa kwa ajiri ya kuwapa elimu ya jinsi na namna ya kujiunga na mfuko huo hususani katika fao la elimu na fao la kuanzia maisha ambapo ni mfuko mojawapo wenye manufaa makubwa kuliko mifuko mingine unaoweza kutoa huduma kulingana na mahitaji wa watanzania pasipo na ubaguzi wala upendeleo

Maseko Kodalo Ambaye ni Afisa wa Mfuko wa pensheni Wa PSPF yeye aliweza kutoa rai kwa wanafunzi wote na wananchi wote waweze kujiunga na mfuko huo ili kuweza kupata mafanikio, alitoa mifano michache ambayo inawezekana ukaimudu pindi unapo jiunga na mfuko huo ambapo kwa mwanafunzi alitaja kuwa unaweza kupata mikopo na kujiwekea akiba ili kuweza kukusaidia katika masomo, vilevile kuna mikopo ya kuanzia maisha  ambayo itakuwezesha kupata nyumba ambazo wamezijenga kwa ajiri ya mtanzania aweze kununua au kukopeshwa na baadae kuweza kurejesha mkopo huo wanyumba, pia aliongeza kwa kusema nyumba zote zimewekewa bima endapo tatizo lolote likitokea basi nyumba hizo zitakuwa salama .

No comments

Powered by Blogger.