BUNGE LAPITISHA MUSWADA, SASA WAANDISHI KUFUNGWA JELA IKIWA...

Ndugu wasomaji wetu tunaomba support yenu kwa kutangaza nasi hapa kwenye hii blog kwa bei nafuu ili tuweze kuendelea kutoa habari bila tatizo lolote. Wasiliana nasi kupitia namba +255713363965 / +255755274953. Tunashukuru kwa ushirikiano wenu.


Mbunge wa Muhambwe, Felix Mkosamali akichangia mjadala katika kikao cha Bunge, mjini Dodoma. Picha na Anthony Siame 

Mvutano mkali uliibuka jana bungeni wakati Bunge lilipokaa kama kamati kupitisha Muswada wa Takwimu wa mwaka 2013, baada ya wabunge kuupinga. Muswada huo una kipengele kinachotoa adhabu ya kifungo cha miaka mitatu jela na faini isiyopungua Sh10 milioni kwa mtu au chombo cha habari kitakachofanya makosa ya kutoa takwimu zisizokuwa sahihi.
Wabunge hao waliufananisha muswada huo na miswada miwili ya habari ya mwaka 2015 ambayo itawasilishwa bungeni Jumanne chini ya hati ya dharura kwa usiri uliopo na mpango wa kuiwasilisha bila wadau kushirikishwa.
Awali, muswada wa Takwimu uliwasilishwa kwenye mkutano wa 17 wa Bunge uliofanyika Novemba mwaka jana na wabunge wakapinga vifungu vinavyobana waandishi wa habari kuhusu eneo la takwimu, ndipo Serikali ilipoamua kuutoa kwa maelezo kuwa inakwenda kuurekebisha hadi ilipourejesha jana na ukapitishwa kwa mbinde.
ENDELEA KUSOMA HABARI HII KWA KUBOFYA HAPA CHINI
Jana, Bunge lilipokaa kama kamati kupitisha muswada huo, Mbunge wa Ubungo (Chadema), John Mnyika alihoji juu ya kifungu hicho kinachotoa adhabu kali na Serikali kujibu kuwa imeshakifanyia marekebisho.
Hata hivyo, Mnyika hakukubaliana na maelezo hayo, bali alisema kifungu hicho hakijafanyiwa marekebisho yoyote na Serikali na adhabu bado inaendelea kuwa kali.
Mnyika aliungwa mkono na mbunge wa Viti Maalumu (CCM), Ester Bulaya aliyehoji, “Iweje Serikali iweke kinga kwa mtumishi wa Serikali anayetoa taarifa zisizo sahihi lakini ikaacha kuweka kwa mwandishi anayepewa taarifa hizo zisizo sahihi na ofisa huyo wa Serikali?”
Maelezo ya Bulaya yalimfanya Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), George Masaju kusimama na kusema kwa kifupi kuwa “mwandishi atakwenda kujieleza mahakamani au polisi.”
Ilivyokuwa mwaka jana
Kabla ya kuondolewa bungeni Novemba 2014 muswada huo pamoja na mambo mengine, ulikuwa ukipendekeza faini ya Sh10 milioni au kifungo cha mwaka mmoja jela au vyote kwa chombo cha habari kitakachotoa taarifa za kitakwimu za uongo au zenye upotoshaji.
 “Mtu yeyote, kwa kujifanya anatimiza majukumu yake, iwapo anapata au anaomba kupatiwa taarifa ambayo haijaidhinishwa kuipata na kuichapisha au kuisambaza atakuwa amefanya kosa ambalo adhabu yake ni kifungo kisichopungua miezi 12 au faini isiyopungua shilingi milioni mbili au vyote kwa pamoja,” ilisema ibara ya 37 (d) cha muswada huo.
Muswada huo pia ulikuwa ukiainisha kwamba takwimu rasmi ni zile ambazo zimetolewa na kuidhinishwa na taasisi zilizoelezwa kwenye ibara hiyo ya 20 na ndizo pekee zinazoweza kutumika kama ushahidi kwenye kesi.


Adhabu kali pia zimependekezwa kwenye muswada huo kwa vyombo vya habari ambavyo vitatoa taarifa za takwimu zitakazosababisha watu wasishiriki kwenye shughuli zilizoandaliwa na Serikali zinazohusiana na masuala ya takwimu.
Muswada huo unapendekeza pia adhabu kali kwa watu ambao watakataa kutoa ushirikiano kwa watu waliotumwa kufanya kazi za ukusanyaji taarifa kama vile sensa na adhabu iliyopendekezwa ni faini isiyopungua Sh5 milioni, kifungo kisichopungua miezi 12 au vyote kwa pamoja.
Miswada yapita
Miswada mingine iliyopitishwa na Bunge jana ni muswada wa Usimamizi wa Kodi wa Mwaka 2014, wa Sheria ya Marekebisho ya Uhamiaji wa mwaka 2014 na Wakala wa Usimamizi wa Kodi wa mwaka 2014
CHANZO: MWANANCHI

No comments

Powered by Blogger.