DKT. SHEIN AFUNGUA JENGO LA AFISI KUU YA UHAMIAJI ZANZIBAR

Ndugu wasomaji wetu tunaomba support yenu kwa kutangaza nasi hapa kwenye hii blog kwa bei nafuu ili tuweze kuendelea kutoa habari bila tatizo lolote. Wasiliana nasi kupitia namba +255713363965 / +255755274953. Tunashukuru kwa ushirikiano wenu.


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akisalimiana na Kamishna Mkuu wa Uhamiaji Tanzania Sylvester Ambokile Mwakinyule wakati alipowasili kulifungua Jengo la Afisi Kuu ya Uhamiaji Zanzibar leo liliopo Kilimani Mjini Zanzibar akimuwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akikata utepe kama ishara ya ufunguzi wa Jengo la Afisi Kuu ya Uhamiaji Zanzibar leo Kilimani Mjini Zanzibar akimuwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete (kutoka kushoto) Kamishna Mkuu wa UhamiajiTanzania Sylvester Ambokile Mwakinyule na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Perera A.Silima.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (katikati) akiangalia hatua za utengenezaji wa PassPort za Uraia wa Tanzania wakati alipotembelea sehemu mbali mbali baada ya kulifungua Jengo la Afisi Kuu ya Uhamiaji Zanzibar leo Kilimani Mjini Zanzibar akimuwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete (kushoto) Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Perera A.Silima na (kulia) Inspekta wa Uhamiaji Hassan Suleiman Ameir.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (wa pili kulia) akipata maelezo kutoka kwa Asistance Inspekta Khamis Ali Haji (katikati)wakati alipotembelea katika chumba cha kumbukumbu za picha kwa Wananchi walioomba Passpoti za Uraia baada ya kulifungua Jengo la Afisi Kuu ya Uhamiaji Zanzibar leo Kilimani Mjini Zanzibar akimuwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete. [Picha na Ikulu].

No comments

Powered by Blogger.