MWENYEKI WA WAFANYABIASHARA AACHIWA KWA DHAMANA

Ndugu wasomaji wetu tunaomba support yenu kwa kutangaza nasi hapa kwenye hii blog kwa bei nafuu ili tuweze kuendelea kutoa habari bila tatizo lolote. Wasiliana nasi kupitia namba +255713363965 / +255755274953. Tunashukuru kwa ushirikiano wenu.


Mwenyekiti wa Jumuiya ya wafanyabiashara Bwana Jonson Minja akiwa na baadhi ya Wafanyabiashara wakifurahia jambo walipokuwa wakipiga Picha ya Pamoja hivi karibuni mjini Dodoma, huku wafanyabiashara hao wakiwa wamevaa furana zenye ujumbe wa MINJA KWANZA BIASHARA BAADAE.(Picha na maktaba yetu)

 Mwenyekiti wa Jumuia ya wafanyabiasha nchini Tanzania Bwana Jonson Minja ameachiwa kwa dhamana na Mahakama ya Hakimu mkazi Mkoa wa Dodoma baada ya wafanyabiashara kuweka mgomo ambao ulikuwa haujafahamika ukomo wake mara moja ambapo suala hilo hapo jana bungeni mjini Dodoma liliibua mjadala miongoni mwa wabunge wakitaka serikali kukaa na kuangalia namna yakuweza kumaliza mgogoro uliopo kwa kupatiwa dhamana kwa mwenyekiti huyo na ili waweze kukaa meza moja na kumaliza tofauti zilizopo.
Hata hivyo moja ya mambo ambayo Mwenyekiti huyo anakabiliwa nayo ni pamoja na mashtaka mawili ya kuwachochea wafanyabiashara mkoani Dodoma kutenda kosa na kuwakataza wafanyabiashara nchini wasitumie mashine za kieletroniki za kukusanya kodi za EFDS ambavyo vyote ni makosa ya jinai.Endelea kufuatilia taarifa zetu kufahamu.

No comments

Powered by Blogger.