NAIBU WAZIRI WA MAJI MH AMOS MAKALLA AZINDUA MRADI MKUBWA WA MAJI KIJIJI CHA MKONGO NAKAWALE

Ndugu wasomaji wetu tunaomba support yenu kwa kutangaza nasi hapa kwenye hii blog kwa bei nafuu ili tuweze kuendelea kutoa habari bila tatizo lolote. Wasiliana nasi kupitia namba +255713363965 / +255755274953. Tunashukuru kwa ushirikiano wenu.


Naibu Waziri wa Maji Mh. Amos Makalla akisalimiana na watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo, kushoto kwake ni Mkuu wa Wilaya ya Namtumbo Bi. Agnes Hokororo.
Naibu Waziri wa Maji Mh. Amos Makalla akisalimia watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo mara baada ya kuwasili Namtumbo kukagua na kuzindua miradi ya maji wilayani Namtumbo. Kushoto kwa Naibu Waziri ni Mkuu wa Wilaya Bi. Agnes Hokororo.


Naibu Waziri wa Maji, Mh Amos Makalla amefanya ziara ya kikazi wilaya ya Namtumbo pamoja na mambo mengine amezindua mradi mkubwa Maji kijiji cha Mkongo Nakawale ambao watu zaidi ya 4000 wanapata Maji safi.


Aidha amekagua mradi wa Maji Milonji na ametoa agizo hadi kufikia tarehe 12 mei mwaka huu mkandarasi awe amekamilisha kuchimba kisima kingine baada kisima cha awali kuwa na Maji machache.
Pia Mh Makalla amemwagiza Katibu mkuu wizara ya Maji kuunda kikosi kazi cha watalaam kwenda Namtumbo kufuatilia matumizi ya Fedha kwa miradi ya Maji wilaya ya Namtumbo.

Naibu waziri wa Maji Mh. Amos Makalla akifungua maji katika moja ya vituo vya kuchotea maji bara baada ya uzinduzi wa mradi wa maji katika kijiji cha Nakawale kilichopo Namtumbo mkoani Ruvuma.
Naibu Waziri wa Maji Mh. Amos Makalla akiwa na Mbunge wa Namtumbo Mh. Vitta Kawawa wakiashiria kuzinduliwa kwa mradi wa maji wa kijiji cha Nakawale.

No comments

Powered by Blogger.