BASI LA SUPER FEO LILILOKUWA LINATOKEA MBEYA KWENDA SONGEA LIMETUMBUKIA MTONI ENEO LA PIPELINE INYARA LEO ASUBUHI
Ndugu wasomaji wetu tunaomba support yenu kwa kutangaza nasi hapa kwenye hii blog kwa bei nafuu ili tuweze kuendelea kutoa habari bila tatizo lolote. Wasiliana nasi kupitia namba +255713363965 / +255755274953. Tunashukuru kwa ushirikiano wenu.
Mpaka Basi la Super Feo
l inapata ajali lilikuwa na abiria 20 na basi hilo linauwezo wa kubeba abiria
53. Chanzo
cha ajali ni dereva wa basi alitaka kuovatake roli bila ya uangalifu na kakutana
na roli akakimblia kulia zaidi ndipo ikapinduka mara tatu na kufikia kwenye
kalvatina kutumbukia mtoni.
Majeruhi wametajwa kwa majina ambao ni Patriki Mwimbila
ambaye ni dereva msaidizi wa basi na amevunjika
mguu majeruhi wengine ni Sakeni Mwandaneg, Fatuma Nyambi na Feliciana Mwalongo hawa wote wamelazwa hospitali ya mkoa
Mbeya. Waliofariki katika ajali hii ni watatu ambao ni Anastazia Ngonyani, Robett Leyman kutoka Marekani pamoja na mwanaume mmoja hajafahamika jina lake. Abiria kumi na tatu wako salama, dereva wa basi anaitwa Shafii Ngaiyo ametoroka baada ya ajali hiyo kutokea.
HABARI NA JOSEPH MWAISANGO
Post a Comment