HOSPITALI YA AMI YA JIJINI DAR YAFUNGWA

Ndugu wasomaji wetu tunaomba support yenu kwa kutangaza nasi hapa kwenye hii blog kwa bei nafuu ili tuweze kuendelea kutoa habari bila tatizo lolote. Wasiliana nasi kupitia namba +255713363965 / +255755274953. Tunashukuru kwa ushirikiano wenu.


Meneja Biashara wa Kampuni ya Udalali ya Mem, Elieza Mbwambo (kulia), akimkabidhi funguo Meneja wa Kampuni ya Navtej Bains, Zulfiqar Hassanali, baada ya kampuni hiyo kuwaondoa wapangaji Hospitali ya Ami waliokuwa na deni la sh. bilioni 3.2. Makabidhiano hayo yalifanyika nje ya jengo hilo Masaki jijini Dar es Salaam, leo. (Picha na Francis Dande)


HOSPITALI maarufu kwa kutibu vigogo wa serikali, African Medical Investment (AMI), hatimaye imefutwa rasmi baada ya jengo la hospitali hiyo kukabidhiwa kwa mmiliki wa jengo hilo kwa nguvu ya mahakama.

Nao wafanyakazi wa hospitali hiyo, ambayo iko Masaki wilayani Kinondoni, wamesema hawajui hatima yao, baada viongozi wao kuzima simu zao.

Hali hiyo ilitokana na mri ya Mahakama Kuu kuagiza mali za hospitali hiyo zikamatwe na jengo la hospitali hilo lirejeshwe kwa mmiliki wake kutokana na kushindwa kulipa kodi ya pango ya sh. bilioni 3.2 kwa zaidi ya miezi 26.

Akizungumza na wandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Meneja wa Biashara Kampuni ya Madalali (MEM), Elieza Mbwambo, alisema, kazi yao ilikuwa ni kukamata mali na kukabidhi jengo, masuala ya kudai fedha ni jukumu la mmiliki.


Alisema kuwa walifikia hatua hiyo baada ya uongozi wa hospitali hiyo kutii amri ya mahakama ya kuwaondoa wagonjwa wote na kwamba mali walizokamata wataziuza.

“Wiki mbili zilizopita tulikuwa hapa kukamata mali na tuliwapa taarifa wagonjwa wote waliokuwa hapa waondoke na leo tunashukuru wagonjwa wote wameondoka na leo tunamkabidhi jengo mwenye mali,”alisema Mbwambo.

Mbwambo, alisema vifaa vyote vilivyokamatwa vitauzwa, hata hivyo, fursa itatolewa kwanza kwa mmiliki wa jengo hilo.

Akizungumza kwa niaba ya Kampuni ya Navtej Singh ambao ndiyo wa jengo hilo, Zulfiqar Hassanali, alisema baada ya kukabidhiwa jengo lao, wanatarajia kufungua hospitali kama mwanzo kwa vile eneo hilo la Msasani halina huduma hiyo zaidi hapo.

“Bado hatujampata mtu kwa sababu baada ya kutokea tukio hilo kuna watu wengi wamejitokeza kuomba jengo hili kwa kuendesha shughuli hizi,”alisema Hassanali.

No comments

Powered by Blogger.