DKT. MAGUFULI AKAGUA UJENZI WA DARAJA LA KIGAMBONI-KUKAMILIKA MWEZI WA TISA MWAKA HUU

Ndugu wasomaji wetu tunaomba support yenu kwa kutangaza nasi hapa kwenye hii blog kwa bei nafuu ili tuweze kuendelea kutoa habari bila tatizo lolote. Wasiliana nasi kupitia namba +255713363965 / +255755274953. Tunashukuru kwa ushirikiano wenu.


 Waziri wa Ujenzi Dkt. John Pombe Magufuli (wakwanza kulia) akifanya ukaguzi katika mradi wa ujenzi wa Daraja la Kigamboni. Katikati ni Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Mfuko wa Hifadhii ya Jamii (NSSF), Dkt. Ramadhan Dau. Mradi wa Ujenzi wa Daraja hilo umefikia Asilimia 85, na unatarajiwa kukamilika mwezi wa tisa mwaka huu.
 Taswira ya mbele ya Daraja la Kigamboni ambalo linatajajiwa kumamilika mwezi wa Tisa. 
 Kazi za Ujenzi wa Daraja la Kigamboni ukiendelea kwa kasi
 Waziri wa Ujenzi Dkt. John Magufuli akikagua moja ya nguzo za barabara za juu flyovers katika maingilio ya Daraja la Kigamboni. Katika eneo hilo kutajengwa barabara za juu ili kuruhusu magari kupita kwa urahisi wakati wa kuingia na kutoka katika daraja hilo.
 Waziri wa Ujenzi Dkt. John Magufuli akiwa ameambatana na Watendaji mbalimbali wa Wizara ya Ujenzi pamoja na NSSF wakifanya  ukaguzi wa ghafla katika mradi wa ujenzi wa  daraja la Kigamboni.
 Meneja Mradi wa Ujenzi Daraja la Kigamboni kutoka NSSF, Karim Mataka wakwanza kulia akitoa maelezo ya Ujenzi wa Daraja la Kigamboni.
 Waziri wa Ujenzi Dkt. John Magufuli (wapili kulia) akikagua eneo la barabara za kuingia katika Daraja la Kigamboni.
 Sehemu ya barabara za Maingilio ya Daraja la Kigamboni zikiwa katika hatua za mwisho kukamilika.
Sehemu ya Katikati ya Daraja la  Kigamboni kama inavyoonekana. Picha zote kwa Hisani ya Kitengo cha Mawasiliano Wizara ya Ujenzi

No comments

Powered by Blogger.