HABARI

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

MATUKIO

MICHEZO

SIASA

MREMBO JULITHA KABETE AAHIDI MAKUBWA MISS AFRIKA

Ndugu wasomaji wetu tunaomba support yenu kwa kutangaza nasi hapa kwenye hii blog kwa bei nafuu ili tuweze kuendelea kutoa habari bila tatizo lolote. Wasiliana nasi kupitia namba +255713363965 / +255755274953. Tunashukuru kwa ushirikiano wenu.


MWAKILISHI wa Tanzania katika mashindano ya Miss Afrika, Julitha Kabete ameondoka leo kuelekea nchini Nigeria katika fainali ya michuano hiyo inayofanyika Novemba 26 mwaka huu huku akiwaahidi watanzania kwua  ataipeperusha vyema bendera ya Tanzania .

Akizungumza kabla ya kuondoka kwenye  Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Kabete amesema kuwa lengo lake ni kuwa mmoja wa wawakilishi bora katika shindano hilo na kuitangaza vyema nchini  pamoja na kurudi taji hilo na kwa kupitia kampuni ya Millen Magese Group chini ya Mkurugenzi wake ,Happiness 'Millen' Magese ameshukuru kwa kuingia nae mkataba ili aweze kushiriki michuano hiyo na kufanya Kazi nyingine za urembo. 

"Mimi kama mwakilishi wa Tanzania nitahalikisha anafanya vizuri katika shindano hilo, ambalo nimepata nafasi ya kuwa mpeperusha bendera wa nchini yangu Tanzania " amesema. Kabete alikabidhiwa bendera ya taifa na Waziri wa Habari Sanaa Utamaduni na Michezo, Nape Nnauye ambaye alimshihi kwenda kujituma zaidi kwani wana imani na uwezo wake na pia ni moja ya warembo watakaowakilisha vyema nchi yetu na kurudi na taji hilo.

“Lengo la Serikali ni kuhakikisha washiriki wa shindano la Miss Tanzania wanapata fursa nyingine si tu akishapatikana mshinda wengine wanaachwa, hivyo tunaamini mrembo huyo anavigezo vyote na atakwenda kufanya vizuri,” amesema Nape.

Shindano hilo litafanyika nchini humo katika jimbo la Cross River, mji wa Calabar,ambapo Gavana wa jimbo hilo la Cross River Profesa Ben Ayade, atatoa zawadi ya gari na zaidi ya sh.million 52 ya Tanzania hiyo itakuwa kwa ushindi wa kwanza, mshindi wa pili atapata zawadi ya Sh.milioni 32 na ushindi wa Tatu ni Sh.million 22. 

Shindano hilo la Miss Afrika 2016 ambalo limebeba kauli
mbiu ya Kutunza, Kujali na Kuthamini Uchumi wenye kutoa kipaumbele kwa Mazingira kama nyenzo kwa ajili ya Maendeleo endelevu.
Julietha alichaguliwa katika shindano lililoendeshwa na kampuni ya Millen Magese (MMG), inayoshughulika na kusaka vipaji vya warembo pamoja na 
Mmratibu wa MMG, Matukio Chuma, amesema kuwa wanamitindo kutoka kwenye shindano hilo wameweza kuendelea kufanya vizuri kupitia Swahili Fashion Week.

Taasisi hiyo imekuwa ikifanya shughuli zake ndani na nje ya bara la Afrika, ikiwemo nchini Marekani, Millen Magese amekuwa Kinara, Balozi wa kuheshimika na aliye mfano ndani na nje ya Bara la Afrika. mwisho

DIANA EDWARD NDIYE LETE RAHA MISS KINONDONI 2016

Ndugu wasomaji wetu tunaomba support yenu kwa kutangaza nasi hapa kwenye hii blog kwa bei nafuu ili tuweze kuendelea kutoa habari bila tatizo lolote. Wasiliana nasi kupitia namba +255713363965 / +255755274953. Tunashukuru kwa ushirikiano wenu.


 Malkia wa Kinondoni 2016 Diana Edward ndiye huyu hapa.
 Lete Raha Miss Kinondoni 2016, Diana Edward (katikati), akipunga mkono baada ya kutangazwa kuwa mshindi Dar es Salaam jana. Kulia ni  mshindi wa pili Regina Ndimbo na kushoto ni mshindi wa tatu, Sia Pius.
 Warembo hao wakiserebuka wakati wakijitambulisha.
 Wadau wakifuatilia kwa karibu shindano hilo. 
 Washiriki wa shindano hilo wakiwa katika vazi la ubunifu. Kutoka kushoto ni Catherine Liston, Hafsa Mahamoud na Mariana Charles.

 Washiriki hao waliofanikiwa kuingia 10 bora.
 Washiriki waliofanikiwa kuingia tano bora. Kutoka kulia ni Hafsa Mahamoud, Diana Edward ambaye ndiye Miss Kinondoni 2016. Regina Ndimbo, Sia Pius na Jackline Kimambo.

Majaji wa shindano hilo wakiwa kazini.

Mgeni rasmi wa shindano hilo, Gift Msuya (kulia), akiwa katika picha ya pamoja na washindi wa shindano hilo.

 Hapa ni sebene kwa kwenda mbele.
 Wakina mama wakimtuza mwanamuziki Christian Bella wakati akiimba wimbo wa Nani kama mama.

Mgeni rasmi wa shindano hilo, Katibu Tawala wa Wilaya ya Kinondoni, Gift Msuya (katikati), akikabidhi zawadi.

Na Dotto Mwaibale

KAMATI ya maandalizi ya shindano la Lete Raha Miss Kinondoni  2016 imemtangaza Diana Edward  kuwa mlimbwende wa wilaya hiyo baada ya kuibuka mshindi katika shindano lililofanyika Hoteli ya Denfrances iliyopo Sinza jijini Dar es Salaam jana.

Edward aliibuka mshindi baada ya kuwabwaga washiriki wenzake 20 waliokuwa wakiwania taji hilo ambapo nafasi ya pili ilichukuliwa na Regina Ndimbo huku ya tatu ikichukuliwa na Sia Pius ambapo Happyness Munisi akishinda nafasi ya utanashati.

Akizungumza wakati wa mchakato wa kutoa zawadi Mratibu wa shindano hilo, Rhamat George alisema asilimia 10 ya mapato yaliyopatikana katika shindano hilo yatakwenda Wilaya ya Kinondoni kwa ajili ya kusaidia ujenzi wa madarasa ikiwa ni kumuunga mkono Rais Dk. John Magufuli ya kuhakikisha kila mwanafunzi anapata elimu bure katika mazingira bora.

Katika shindano hilo washindi waliofanikiwa kuingia tano bora wataingia moja kwa moja katika kinyang'anyiro cha kumsaka mlimbwende wa Tanzania.

Shindano hilo lilidhaminiwa na Kampuni ya Mabibo Beer Wines and Spirits Ltd kupitia bia ya Windhoek Lager na Draught pamoja na Gazeti la Lete Raha na wadhamini wengine.

Katibu Tawala wa Wilaya ya Kinondoni, Gift  Msuya alisema Serikali itaendelea kuunga mkono mashindano hayo ambayo yamekuwa yakitoa ajira na kuibua vipaji vya watoto wa kike.

Shindano hilo lilipambwa na burudani kutoka kwa mwanamuziki wa muziki wa dansi Christian Bella na kundi la sanaa la Kampuni ya Mabibo Beer Wines and Spirits Ltd.

(Imeandaliwa na mtandao wa www.habari za jamii.com)