Ecobank Tanzania imeendelea kutoa elimu kwa wananchi kuhusu huduma mbalimbali za kifedha kupitia ushiriki wake katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Sabasaba yanayoendelea katika Viwanja vya Julius Nyerere, Dar es Salaam, ambapo banda lake linapatikana katika Kijiji cha Bima kinachosimamiwa na Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania (TIRA).
Akizungumza katika maonesho hayo, mwakilishi wa Ecobank amesema benki hiyo inatoa huduma mbalimbali za kifedha zinazolenga kukidhi mahitaji ya watu binafsi, wafanyabiashara na taasisi, huku ikiwapa wateja suluhisho la huduma za benki kwa urahisi na ufanisi.
Ameeleza kuwa miongoni mwa huduma zinazotolewa ni "Saving Account", ambayo haina makato ya kila mwezi na humruhusu mteja kuweka na kutoa fedha wakati wowote kulingana na mahitaji yake.
Aidha, amesema Ecobank inatoa "Current Account", inayomwezesha mteja kupata huduma ya "Overdraft", inayomruhusu kutumia fedha zinazozidi salio lililopo kwenye akaunti kwa muda wa hadi siku 14, kwa kuzingatia masharti ya benki.
Vilevile, benki hiyo inatoa mikopo ya muda mfupi na muda mrefu kwa makundi mbalimbali yakiwemo watumishi wa umma, wafanyabiashara na watu binafsi, pamoja na mikopo ya ujenzi na ununuzi wa nyumba.
Mbali na huduma za benki, Ecobank pia inatoa huduma mbalimbali za bima zikiwemo bima ya nyumba, magari na afya, kwa kushirikiana na wadau wake wa sekta ya bima, ikiwa ni sehemu ya kuwapatia wateja huduma za kifedha zilizounganishwa katika eneo moja.
Ecobank imewahimiza wananchi wanaotembelea Maonesho ya Sabasaba kutembelea banda lake lililopo Kijiji cha Bima (TIRA) ili kupata elimu zaidi kuhusu huduma za benki na bima, kufungua akaunti, kupata ushauri wa kifedha na kufahamu fursa mbalimbali zinazotolewa na benki hiyo.
Mkuu wa kitengo cha Wateja Binafsi na Biashara kutoka Ecobank Tanzania, Joyce Ndyetabura akimsikiliza mfanyakazi wa Ecobank Tanzania walipokuwa wanatoa huduma katika maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Sabasaba yanayoendelea jijini Dar es Salaam ambapo banda lake linapatikana katika Kijiji cha Bima kinachosimamiwa na Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania (TIRA).
Watumishi wa Ecobank Tanzania wakitoa elimu katika maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Sabasaba yanayoendelea jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa Kitengo cha Biashara kwa Wateja Wakubwa (Commercial Banking) Joyce Ndyetabura akiwa kwenye picha ya pamamo na watumishi wa Ecobank Tanzania katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Sabasaba yanayoendelea katika Viwanja vya Julius Nyerere, Dar es Salaam, ambapo banda lake linapatikana katika Kijiji cha Bima kinachosimamiwa na Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania (TIRA).











.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)











