HABARI

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

MATUKIO

MICHEZO

SIASA

RAIS SAMIA APITA NYENDO ZA NYERERE URUSI







WAZIRI wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mahmoud Thabit Kombo, amesema ziara ya Rais Samia Suluhu Hassan nchini Urusi imefufua kumbukumbu za miaka 57 iliyopita wakati Rais wa Kwanza wa Tanzania, Hayati Mwalimu Julius Nyerere, alipofanya ziara ya kitaifa nchini humo mwaka 1969.Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Balozi Kombo amesema viongozi hao wawili wamekuwa na mwelekeo unaofanana katika maeneo matatu makuu ya uchumi, siasa za kimataifa na kuimarisha nafasi ya Tanzania katika jukwaa la Dunia.

Amesema kama ilivyokuwa kwa Mwalimu Nyerere mwaka 1969, Rais Samia pia amehutubia katika Jiji la St. Petersburg, ambalo wakati huo lilijulikana kama Leningrad, na kutumia jukwaa hilo kueleza fursa za uwekezaji, biashara na utalii zilizopo Tanzania.

Ameongeza kuwa viongozi hao wote wawili walitumia majukwaa ya kimataifa kueleza msimamo wa Tanzania kuhusu masuala ya dunia na kusisitiza umuhimu wa amani, ushirikiano na maendeleo ya pamoja.

Kwa mujibu wa Balozi Kombo, hatua ya Rais Samia kushiriki Jukwaa la Kimataifa la Uchumi la St. Petersburg (SPIEF) na kufanya mazungumzo na viongozi mbalimbali ni mwendelezo wa diplomasia ya kimkakati iliyoasisiwa na Mwalimu Nyerere, yenye lengo la kuimarisha ushawishi wa Tanzania na kufungua fursa zaidi za maendeleo.

TAZAMA HAPA RATIBA YA MICHEZO YOTE YA KOMBE LA DUNIA 2026



Makala : HOTUBA YA RAIS SAMIA URUSI NI USHINDI KIUCHUMI, KIJAMII NA KIDIPLOMASIA




Na Beda Msimbe-TBN, aliyekuwa Urusi
IJUMAA Juni 5, 2026 ilikuwa siku ya kihistoria na ya kipekee, wakati Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, alisipomama mbele ya viongozi wa dunia katika Jukwaa la Kimataifa la Uchumi (St. Petersburg International Economic Forum) na hoja nzito zenye mashiko, akibeba sauti ya Watanzania wote na kuweka wazi fursa zinazopatyikana Tanzania ikiwa na pamoja na mwelekeo mpya wa nchi katika kutengeneza uchumi wa kisasa.

Jukwaa hilo lilikuwa sehemu muhimu ya ziara ya Rais Samia ambayo haikuwa tu ya itifaki, bali ya kueleza milango wazi ya fursa za kiuchumi na kijamii.

Jinsi Rais Samia alivyopokewa na kukirimiwa nchini Urusi katika shughuli zoye zilizomhusu, ilionesha taswira ya urafiki wa dhati na cheko tupu kati yake na mwenyeji wake, Rais Vladimir Putin. Ziara hiyo ilirudisha historia, ikaweka wazi haja ya sasa baada ya ukombozi wa kisiasa kusaidiana kupatikana kwa ukombozi wa kiuchumi na ustawi wa jamii zote mbili.

Akiwa katika jukwaa la kiuchumi, akizungumza na washiriki hotuba ya Rais Samia iliwatafakarisha wahusika, kwani ilkijaa hoja za uchambuzi wa kina na haja ya dunia kubadilika

Rais Samia alifanya uchokozi wa fikira na moja ya uchokozi huo alisema bila kupepesa kuwa ifikapo mwaka 2050, mtu mmoja kati ya wanne duniani atakuwa Mwafrika; na takwimu hizo kutoka kwa Rais Samia Suluhu Hassan ziliambatana na swali: "Je, Afrika itastawi na kukuaa kwa masharti ya nani, na kwa modeli ya nani ya uchumi?"

Swali hilo lenye mantiki kubwa liliulizwa kwa shauku kubwa kutokana na siasa za kijiopiti ambazo zimekuwa zikiyumbisha ushirika wa kawaida na kujazwa na masharti ya kuangushana na kudhibitiana katika mfumo ambao unamlazimisha maskini asiendelee au kuchaguliwa patna wa kuzungumza naye.

Katika misingi mikubwa ya kufikiri kilojiki Rais Samia alikuwa anaitafadhalisha dunia sio kuistiri Afrika bali kutambua ukweli na kuiacha Afrika ijiamulie mambo yake yenyewe.

Mathalani Afrika kwa sasa ina Ajenda 2063 na soko la AfCFTA, lakini kuna mataifa yanayoendelea kuingilia kati kila mara na kuwatenganisha waafrika ili wajifikirie wanahitaji masaada katika utatuzi wa kero zinazowakabili.

Rais Putin aliunga mkono hoja hiyo, jambo lililoleta miguno ya ridhaa na vigelegele ukumbini.Kuna mambo mengi yanayopaswa kufanywa na Waafrika wenyewe yenye manufaa makubwa kwa binadamu

Mambo yaliyoguswa
Katika hotuba yake na ziara hiyoik ya Urusi Rais Samia amegusa mambo mengi. Hapa tunaweza kuangazia maeneo makubwa yaliyoguswa na jinsi makubaliano yalivyomalizika ikiwa ni mafanikio makubwa kwa Tanzania.

Ikumbukwe kwamba ndani ya ziara ya Rais Samia ambapo pia aliambatana na wafanyabiashara inakumbusha ulimwengu kuhusu mizizi imara ya kidiplomasia kati ya Tanzania na Urusi. Kuna historia ndefu ya mahusiano kuanzia miaka ya uhuru,kwani siku mbili baada ya Tanzania bara kupata uhuru, Urusi ilituma salamu vivyo hivyo kwenye mapinduzi matukufu ya Zanzibar.

Mbele ya wawekezaji, Rais Samia alibainisha kuwa uchumi wa Tanzania unakua kwa kasi ya takribani 6%, ukiwa miongoni mwa chumi zinazochangamka zaidi Afrika.

Alitangaza Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, inayolenga kumfikisha kila Mtanzania kwenye kipato cha wastani cha dola $7,000$ huku akielezea fursa za uwekezaji na biashara nchini Tanzania

Hotuba yake hiyo iliyopigiwa makofi mara kwa mara iliwavutia matajiri wa Kirusi, ambapo sekta binafsi ya Urusi ilikiri kuwa Tanzania ni soko salama na lenye utulivu wa kisiasa unaoruhusu ukuaji wa mitaji.

Lakini hayo yamesemwa wakati pia Rais akieleza kuwapo kwa Mapinduzi makubwa ya Miundombinu (Reli na Bandari). Rais Samia ambaye katika mkutano huo pamoja na ule wa pembeni ambapo wafanyabiashara wa Tanzania walipata nafasi ya kuzungumza na wenzao wa Urusi, alieleza kwa kina ujenzi wa Reli ya Kisasa (SGR) inayounganisha Bandari ya Dar es Salaam na nchi za Rwanda, Burundi, na DRC na faida yake kwa wakazi wa eneo hili.

Pia alitaja mpango wa miaka mitano (2026–2031) wa kupanua reli hiyo hadi Musoma, na kuunganisha ukanda wa kusini kuelekea Malawi na Msumbiji. Urusi ikiwa na uzoefu mkubwa wa teknolojia ya reli na usafirishaji, ilionesha nia ya kutoa utaalamu wa kihandisi na mitambo ili kuharakisha uunganishaji wa reli hizo za kikanda.

Suala la kuwepo kwa maboresho ya uwekezaji na mifumo ya saa 24 kulileta msisimko mkubwa. Rais alieleza jinsi uwekezaji ulivyopaa kutoka dola bilioni 3 (2021) hadi dola bilioni 12 (2025) kutokana na mfumo wa usajili wa kampuni unaochukua hadi saa 24 tu. Ni kutokana na kutambulika kwa ukweli huu Taasisi za uwekezaji za Tanzania (TIC) na zile za Urusi zilisaini mikataba ya ushirikiano. Hatua hii ilifungwa kwa cheko na bashasha, kwani urasimu sasa umepigwa marufuku rasmi.

Aidha Miradi ya Eneo Maalum la Kiuchumi la Bagamoyo na Bandari ya Kimataifa ya Mizigo ya Mangapwani (Zanzibar) ilipewa kipaumbele cha juu na makampuni makubwa ya Urusi yanayohusika na masuala ya meli na usafirishaji wa baharini. Wao walikubali kutuma timu za wataalamu nchini Tanzania kufanya upembuzi yakinifu wa namna ya kuwekeza kwenye bandari hizo.

Kwenye Sekta ya Madini Rais Samia alizungumzia haja ya Tanzania ambayo ni Kuongeza Thamani Ndani ya Nchi.Tanzania ikiwa na utajiri wa dhahabu, uranium, nickel, graphite, helium, na madini adimu.

"Hatutaki tena kuuza malighafi pekee, tunataka viwanda vya usindikaji hapa nchini."alisema Rais Samia. Urusi, ikiwa ni mbabe wa madini, ilimalizia haja ya Tanzania kwa kukubali kujenga viwanda (Industrial Parks) nchini Tanzania ili kuchenjua na kuongeza thamani ya madini kabla hayajasafirishwa kwenda nje.

Katikia ziara hii Rais Samia alielezea na kudhihirisha ni kwa namna gani Tanzania iko tayari kwa biashara, ubunifu, na ushirikiano wa kufanikisha kila hatua itakayochangia ustawi wa wananchi wake.

Wakati Rais Samia akimaliza hotuba yake kwenye jukwaa hilo la St Petersburg kwa kutoa shukrani za dhati kwa Rais Vladimir Putin kwa ukarimu wake, viongozi hao wawili walionesha tabasamu la furaha, ikiwa ni ishara ya kukubalika kwa hoja za Tanzania na mwanzo mpya wa dhahabu katika uhusiano wa mataifa haya mawili.

RAIS SAMIA: MANENO BASI, SASA NI UTEKELEZAJI


Na Beda Msimbe,TBN, Moscow
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan amesema wakati umefika kwa Tanzania na Urusi kutekeleza makubaliano na kuacha maneno katika kufanikisha makubaliano yanayokuza biashara na uwekezaji.

Amesema kwamba uwekezaji Tanzania unalipa hasa katika mikakatik ambayo imelenga kutekeleza Dira ya maendeleo ya 2050.

Alisema kwamba milango ya Tanzania ipo wazi kuona kwamba makubaliano ya ujenzi wa viwanda vya dawa, viua dud una uwekezaji kwimngine unfanyuiwa kazi kwa manjufaa ya pande zote mbili.

Alisema ikiwa sehemu ya kurahisha utekelezaji wa mikataba ya uwekezaji kuanzia Julai 2 mwaka huu Shirika la Ndege (ATCL) litaanza safari za moja kwa moja kutoka Dar es Salaam, Moscow na Zanzibar.

Aidha ni matarajio ya Rais Samia kwamba Shirika la Ndege la Urusi la Azur pia litanza safari hizo.

Akizungumza na wafanyabiashara juu ya nafasi ya wananchi wa pande zote mbili kunufaika na uhusiano huo, Rais Samia alizungumzia kuhusu uwekezaji wa Urusi nchini Tanzania na kuwaita wafanyabuashara na wawekezaji katika nishati, madini, dawa za binadamu, viwatilifu na kilimo na kusema mabadiliko makubwa yanatakiwa kufanywa ili kupunguza urari wa biashara.

Alisema kwamba ujazo wa sasa biashara hauakisi ukweli kuwa kuna nafasi kubwa ya kuwapo kwa maendeleo ya ushirikiano hasa katika n yajna ambazo ni za kimkakati zinazolenga kuihudumia Dira ya Taifa ya Maendeleo ya 2050.

Naye Waziri wa Maendeleo ya Kiuchumi wa Urusi, Maxim Reshetnikov amesema kwamba amefurahishwa na juhudi za kuifungua Tanzania zinazofanywa na Rais Samia Suluhu Hassan.

Alisema juhudi hizo zinazaa matunda na kwamba Urusi ipo tayari kushirikiana na Tanzania katika miradi yake ya kimkakati.

Anasema taifa hilo litaendelea kufungua fursa mbalimbali kwa kuwekeza nchini Tanzania katika kilimo na teknolojia na viwanda

“Tanzania ni lango la mashariki ya kati tupo tayari kuwapatia teknolojia na utaalamu wetu na tupo tayari kushiriki katika kuanzisha viwanda mbalimbali vya dawa na mbolea” alisisitiza waziri huyo akishukuru kwa namna ambavyo wafanyabiashara wa Tanzania walivyofika kwa wingi baada ya mkutano wa Arusha, kushiriki katika ukamilishaji wa mambo mbalimbali.

Aidha mmoja wa wafanyabiashara wa Kitanzania akizungumza baada ya kukamilika kwa kongamano hilo, Dhruv Jog, amesema kualikwa kwa wafanyabiashara katika safari ya Rais na kushiriki kongamano hilo inaonesha ni kwa namna gani sekta binafsi inathaminiwa katika kubadili maisha ya Watanzania.

Alisema kitendo hic ho kinasaidia kuifungua jumuiya ya sekta binafsi katika daraja jingine. Alisema kufanikiwa kufungua soko la Urusi kutawezesha watanzania kufanya biashara na nchi takribani 15 zinazofanya ukanda wa Urusi hivyo kuleta kipato zaidi.

Katika ziara hii ya kihistoria ikifanywa kwa mara ya pili katika historia ya uhusiano wa Tanzania na Urusi, ya kwanza ilikuwa ni miaka ya 1960 iliyofanywa na baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere, Rais Samia anaendeleza kampeni kubwa ya kuhakikisha Tanzania inanufaika pia kiuchumi na uhusiano mzuri na mataifa mbalimbali.

Akiwa hapa Rais Samia alifanya mazungumzo na Rais Vladmir Putin katika lengo la kuimarisha uhusiano wa kidiplomasia, kisiasa, kiuchumi na kihistoria baina ya Tanzania na Urusi

Pia Rais Samia ameiweka Tanzania katika ramani ya uwekezaji kwa hotuba yake aliyoitoa katika mkutano mkubwa wa uwekezaji jijini St Petersburg.

TANZANIA YASHIRIKI MKUTANO WA AFIAAR PORT LOUIS, MAURITIUS


Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA) imeshiriki katika Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Jukwaa la Wasimamizi wa Taaluma ya Ukaguzi Afrika (African Forum of Independent Accounting and Auditing Regulators (AFIAAR) wa mwaka 2026, unaofanyika mjini Port Louis, Mauritius kuanzia tarehe 2 hadi 5 Juni 2026.

Katika Mkutano huo, Mkurugenzi Mtendaji wa NBAA, CPA Prof. Siasa Mzenzi, alichaguliwa kuwa Makamu Mwenyekiti wa AFIAAR. Pamoja na Mkurugenzi Mtendaji, NBAA imewakilishwa na CPA Pius Maneno, Mkurugenzi Mtendaji Mstaafu wa NBAA na Makamu Mwenyekiti anayemaliza muda wake wa jukwaa hilo; CPA Winnington Makaka, Mkuu wa Sehemu ya Ubora wa Ukaguzi (AQR); pamoja na Magreth Kageya, Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano na Mawasiliano cha NBAA.

Lengo la mkutano huo ni kuwakutanisha wasimamizi wa taaluma ya Uhasibu na Ukaguzi barani Afrika ili kujadili masuala mbalimbali yanayohusu taaluma hiyo, hususan hali ya ubora wa ukaguzi. Majadiliano hayo yanalenga kuimarisha ubora wa taarifa za ukaguzi wa makampuni, jambo litakalosaidia kukuza uchumi wa Afrika kwa kuongeza imani ya wawekezaji kupitia taarifa sahihi na za kuaminika za kifedha.

Akizungumza katika mkutano huo, Mkurugenzi Mtendaji wa NBAA na Makamu Mwenyekiti wa AFIAAR, CPA Prof. Siasa Mzenzi, alisema: “Mkutano huu ni muhimu kwa taasisi yetu na Tanzania kwa ujumla, kwani umetupatia fursa ya kujifunza na kubadilishana uzoefu kuhusu mbinu bora za usimamizi wa taaluma ya ukaguzi. Maarifa haya yatasaidia kuboresha ubora wa huduma za ukaguzi nchini na hivyo kuongeza uaminifu wa taarifa za kifedha zinazotolewa na taasisi na makampuni mbalimbali.”

Mkutano wa AFIAAR unawakutanisha wadau mbalimbali wa usimamizi wa taaluma ya ukaguzi kutoka nchi mbalimbali za Afrika kwa lengo la kuimarisha ushirikiano, kubadilishana uzoefu na kujadili mikakati ya kuendeleza ubora wa ukaguzi barani humo.










NBAA na BoT Wajadili Teknolojia katika Sekta ya Fedha



Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA), kwa kushirikiana na Benki Kuu ya Tanzania (BOT), imeandaa semina ya pamoja uliyowakutanisha wataalamu wa Uhasibu, Wakaguzi wa hesabu na wadau wa sekta ya fedha kutoka ndani na nje ya nchi iliyoanza tarehe 25 hadi 27, Mei, 2026.

Akifungua rasmi semina hiyo iliofanyika jijini Arusha, Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT) Emmanuel Tutuba, amewataka wataalamu wa fedha na Ukaguzi nchini kuhamasisha matumizi ya mifumo ya kidijitali katika miamala ya kifedha ili kupunguza matumizi ya fedha taslimu pamoja na vihatarishi vinavyoweza kujitokeza katika sekta ya fedha.

Tutuba amesema matumizi makubwa ya teknolojia katika huduma za kifedha yataisaidia Tanzania kudhibiti uvujaji wa fedha, kuongeza uwazi wa miamala na kuimarisha usalama wa mifumo ya kifedha nchini.

Ametoa wito huo katika semina ya pamoja ya wataalamu wa Uhasibu na Ukaguzi wa hesabu (NBAA) inayofanyika Jijini Arusha, akisisitiza umuhimu wa kusimamia masuala ya mabadiliko ya Tabianchi, mazingira, utawala bora pamoja na vihatarishi vinavyojitokeza kwenye sekta ya fedha kwa kuzingatia viwango vya kimataifa.

Aidha Tutuba amesema Tanzania imeendelea kuwa na uchumi himilivu licha ya changamoto za uchumi wa dunia, huku akibainisha kuwa usimamizi mzuri wa sekta ya fedha na utekelezaji wa mifumo endelevu vitasaidia Taifa kufikia dira ya uchumi wa trilioni moja.

Kwa Upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA) CPA Prof. Siasa Issa Mzenzi amesema miongoni mwa mambo watakaojadili na kujifunza ni Pamoja na matumizi ya TEHAMA katika masuala yote ya fedha kupitia.

Mafunzo hayo yaliyoandaliwa na NBAA na Benki Kuu ya Tanzania (BoT) yanalenga kuimarisha mfumo wa fedha endelevu kwa kutumia teknolojia sambamba na kuzingatia misingi ya mazingira, kijamii na utawala bora katika sekta ya fedha nchini.
Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BOT), Emmanuel Tutuba akizungumza wakati wa kufungua semina ya pamoja iliyoandaliwa na NBAA na BOT iliyofanyika jijini Arusha
Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA) CPA Prof. Siasa Issa Mzenzi akizungumza wakati wa ufunguzi wa semina ya pamoja iliyoandaliwa na NBAA na BOT iliyowakutanisha wataalamu wa Uhasibu, Wakaguzi wa hesabu na wadau wa sekta ya fedha kutoka ndani na nje ya nchi.
Baadhi ya wataalamu wa Uhasibu, Ukaguzi wa hesabu na wadau wa sekta ya fedha kutoka ndani na nje ya nchi wakifuatilia ufunguzi wa Semina ya pamoja iliyoandaliwa na NBAA na BOT
Picha za pamoja

Rais Samia ashiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali kuhusu Uvumbuzi wa Nishati ya Nyuklia barani Afrika (NEISA), Kigali nchini Rwanda


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza katika Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali kuhusu Uvumbuzi wa Nishati ya Nyuklia barani Afrika (NEISA), Kigali nchini Rwanda tarehe 19 Mei, 2026. Mkutano huo wa Kimataifa unawakutanisha pia wataalamu wa nishati, wawekezaji na mashirika ya kimataifa, ambapo utajadili matumizi ya nishati ya nyuklia kwa maendeleo ya Bara la Afrika. Mkutano huo pia unalenga kujadili namna bora ya kuongeza upatikanaji wa nishati ya umeme Afrika, kupunguza uchafuzi wa mazingira, kusaidia maendeleo ya viwanda, kukuza ubunifu wa teknolojia za nishati ya nyuklia pamoja na kuvutia wawekezaji katika miradi ya nishati tarehe, 19 Mei, 2026.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha ya pamoja na Viongozi mbalimbali walioshiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali kuhusu Uvumbuzi wa Nishati ya Nyuklia barani Afrika (NEISA), Kigali nchini Rwanda tarehe 19 Mei, 2026. Mkutano huo wa Kimataifa unawakutanisha pia wataalamu wa nishati, wawekezaji na mashirika ya kimataifa, ambapo utajadili matumizi ya nishati ya nyuklia kwa maendeleo ya Bara la Afrika. Mkutano huo pia unalenga kujadili namna bora ya kuongeza upatikanaji wa nishati ya umeme Afrika, kupunguza uchafuzi wa mazingira, kusaidia maendeleo ya viwanda, kukuza ubunifu wa teknolojia za nishati ya nyuklia pamoja na kuvutia wawekezaji katika miradi ya nishati, tarehe 19 Mei, 2026.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akitembelea maonyesho wakati wa Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali kuhusu Uvumbuzi wa Nishati ya Nyuklia barani Afrika (NEISA), Kigali nchini Rwanda tarehe 19 Mei, 2026. Mkutano huo wa Kimataifa unawakutanisha pia wataalamu wa nishati, wawekezaji na mashirika ya kimataifa, ambapo utajadili matumizi ya nishati ya nyuklia kwa maendeleo ya Bara la Afrika. Mkutano huo pia unalenga kujadili namna bora ya kuongeza upatikanaji wa nishati ya umeme Afrika, kupunguza uchafuzi wa mazingira, kusaidia maendeleo ya viwanda, kukuza ubunifu wa teknolojia za nishati ya nyuklia pamoja na kuvutia wawekezaji katika miradi ya nishati, tarehe 19 Mei, 2026.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan pamoja na Viongozi mbalimbali wakishiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali kuhusu Uvumbuzi wa Nishati ya Nyuklia barani Afrika (NEISA), Kigali nchini Rwanda tarehe 19 Mei, 2026. Mkutano huo wa Kimataifa unawakutanisha pia wataalamu wa nishati, wawekezaji na mashirika ya kimataifa, ambapo utajadili matumizi ya nishati ya nyuklia kwa maendeleo ya Bara la Afrika. Mkutano huo pia unalenga kujadili namna bora ya kuongeza upatikanaji wa nishati ya umeme Afrika, kupunguza uchafuzi wa mazingira, kusaidia maendeleo ya viwanda, kukuza ubunifu wa teknolojia za nishati ya nyuklia pamoja na kuvutia wawekezaji katika miradi ya nishati.