HABARI

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

MATUKIO

MICHEZO

SIASA

NBAA na BoT Wajadili Teknolojia katika Sekta ya Fedha



Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA), kwa kushirikiana na Benki Kuu ya Tanzania (BOT), imeandaa semina ya pamoja uliyowakutanisha wataalamu wa Uhasibu, Wakaguzi wa hesabu na wadau wa sekta ya fedha kutoka ndani na nje ya nchi iliyoanza tarehe 25 hadi 27, Mei, 2026.

Akifungua rasmi semina hiyo iliofanyika jijini Arusha, Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT) Emmanuel Tutuba, amewataka wataalamu wa fedha na Ukaguzi nchini kuhamasisha matumizi ya mifumo ya kidijitali katika miamala ya kifedha ili kupunguza matumizi ya fedha taslimu pamoja na vihatarishi vinavyoweza kujitokeza katika sekta ya fedha.

Tutuba amesema matumizi makubwa ya teknolojia katika huduma za kifedha yataisaidia Tanzania kudhibiti uvujaji wa fedha, kuongeza uwazi wa miamala na kuimarisha usalama wa mifumo ya kifedha nchini.

Ametoa wito huo katika semina ya pamoja ya wataalamu wa Uhasibu na Ukaguzi wa hesabu (NBAA) inayofanyika Jijini Arusha, akisisitiza umuhimu wa kusimamia masuala ya mabadiliko ya Tabianchi, mazingira, utawala bora pamoja na vihatarishi vinavyojitokeza kwenye sekta ya fedha kwa kuzingatia viwango vya kimataifa.

Aidha Tutuba amesema Tanzania imeendelea kuwa na uchumi himilivu licha ya changamoto za uchumi wa dunia, huku akibainisha kuwa usimamizi mzuri wa sekta ya fedha na utekelezaji wa mifumo endelevu vitasaidia Taifa kufikia dira ya uchumi wa trilioni moja.

Kwa Upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA) CPA Prof. Siasa Issa Mzenzi amesema miongoni mwa mambo watakaojadili na kujifunza ni Pamoja na matumizi ya TEHAMA katika masuala yote ya fedha kupitia.

Mafunzo hayo yaliyoandaliwa na NBAA na Benki Kuu ya Tanzania (BoT) yanalenga kuimarisha mfumo wa fedha endelevu kwa kutumia teknolojia sambamba na kuzingatia misingi ya mazingira, kijamii na utawala bora katika sekta ya fedha nchini.
Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BOT), Emmanuel Tutuba akizungumza wakati wa kufungua semina ya pamoja iliyoandaliwa na NBAA na BOT iliyofanyika jijini Arusha
Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA) CPA Prof. Siasa Issa Mzenzi akizungumza wakati wa ufunguzi wa semina ya pamoja iliyoandaliwa na NBAA na BOT iliyowakutanisha wataalamu wa Uhasibu, Wakaguzi wa hesabu na wadau wa sekta ya fedha kutoka ndani na nje ya nchi.
Baadhi ya wataalamu wa Uhasibu, Ukaguzi wa hesabu na wadau wa sekta ya fedha kutoka ndani na nje ya nchi wakifuatilia ufunguzi wa Semina ya pamoja iliyoandaliwa na NBAA na BOT
Picha za pamoja

Rais Samia ashiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali kuhusu Uvumbuzi wa Nishati ya Nyuklia barani Afrika (NEISA), Kigali nchini Rwanda


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza katika Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali kuhusu Uvumbuzi wa Nishati ya Nyuklia barani Afrika (NEISA), Kigali nchini Rwanda tarehe 19 Mei, 2026. Mkutano huo wa Kimataifa unawakutanisha pia wataalamu wa nishati, wawekezaji na mashirika ya kimataifa, ambapo utajadili matumizi ya nishati ya nyuklia kwa maendeleo ya Bara la Afrika. Mkutano huo pia unalenga kujadili namna bora ya kuongeza upatikanaji wa nishati ya umeme Afrika, kupunguza uchafuzi wa mazingira, kusaidia maendeleo ya viwanda, kukuza ubunifu wa teknolojia za nishati ya nyuklia pamoja na kuvutia wawekezaji katika miradi ya nishati tarehe, 19 Mei, 2026.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha ya pamoja na Viongozi mbalimbali walioshiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali kuhusu Uvumbuzi wa Nishati ya Nyuklia barani Afrika (NEISA), Kigali nchini Rwanda tarehe 19 Mei, 2026. Mkutano huo wa Kimataifa unawakutanisha pia wataalamu wa nishati, wawekezaji na mashirika ya kimataifa, ambapo utajadili matumizi ya nishati ya nyuklia kwa maendeleo ya Bara la Afrika. Mkutano huo pia unalenga kujadili namna bora ya kuongeza upatikanaji wa nishati ya umeme Afrika, kupunguza uchafuzi wa mazingira, kusaidia maendeleo ya viwanda, kukuza ubunifu wa teknolojia za nishati ya nyuklia pamoja na kuvutia wawekezaji katika miradi ya nishati, tarehe 19 Mei, 2026.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akitembelea maonyesho wakati wa Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali kuhusu Uvumbuzi wa Nishati ya Nyuklia barani Afrika (NEISA), Kigali nchini Rwanda tarehe 19 Mei, 2026. Mkutano huo wa Kimataifa unawakutanisha pia wataalamu wa nishati, wawekezaji na mashirika ya kimataifa, ambapo utajadili matumizi ya nishati ya nyuklia kwa maendeleo ya Bara la Afrika. Mkutano huo pia unalenga kujadili namna bora ya kuongeza upatikanaji wa nishati ya umeme Afrika, kupunguza uchafuzi wa mazingira, kusaidia maendeleo ya viwanda, kukuza ubunifu wa teknolojia za nishati ya nyuklia pamoja na kuvutia wawekezaji katika miradi ya nishati, tarehe 19 Mei, 2026.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan pamoja na Viongozi mbalimbali wakishiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali kuhusu Uvumbuzi wa Nishati ya Nyuklia barani Afrika (NEISA), Kigali nchini Rwanda tarehe 19 Mei, 2026. Mkutano huo wa Kimataifa unawakutanisha pia wataalamu wa nishati, wawekezaji na mashirika ya kimataifa, ambapo utajadili matumizi ya nishati ya nyuklia kwa maendeleo ya Bara la Afrika. Mkutano huo pia unalenga kujadili namna bora ya kuongeza upatikanaji wa nishati ya umeme Afrika, kupunguza uchafuzi wa mazingira, kusaidia maendeleo ya viwanda, kukuza ubunifu wa teknolojia za nishati ya nyuklia pamoja na kuvutia wawekezaji katika miradi ya nishati.

Rais Dkt. Samia Aelekea Rwanda Kushiriki Mkutano wa Nishati ya Nyuklia Afrika




Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiagana na viongozi mbalimbali kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) Jijini Dar es Salaam kabla ya kuondoka nchini, kuelekea Kigali, Rwanda kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali kuhusu Uvumbuzi wa Nishati ya Nyuklia barani Afrika (NEISA) tarehe 19 Mei, 2026. Mkutano huo wa Kimataifa unawakutanisha pia wataalamu wa nishati, wawekezaji na mashirika ya kimataifa, ambapo utajadili matumizi ya nishati ya nyuklia kwa maendeleo ya Bara la Afrika. Mkutano huo pia unalenga kujadili namna bora ya kuongeza upatikanaji wa nishati ya umeme Afrika, kupunguza uchafuzi wa mazingira, kusaidia maendeleo ya viwanda, kukuza ubunifu wa teknolojia za nishati ya nyuklia pamoja na kuvutia wawekezaji katika miradi ya nishati.

Baraza la Mawaziri la EAC kukutana kwa Dharura jijini Arusha


Maandalizi ya Mkutano wa 60 wa Dharura wa Baraza la Mawaziri la Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), unaotarajiwa kufanyika tarehe 22 Mei 2026, yameanza rasmi kupitia vikao vya ngazi ya wataalamu vinavyoendelea kuanzia tarehe 18 hadi 20 Mei 2026 katika Makao Makuu ya Jumuiya hiyo jijini Arusha.

Kikao hicho cha wataalamu kimepokea na kujadilia taarifa ya Kamati ya Fedha na Utawala kuhusu masuala ya fedha ya Jumuiya, na rasimu ya bajeti ya Sekretarieti ya EAC pamoja na taasisi zake kwa mwaka wa fedha 2026/2027. Mapendekezo yatakayopitishwa katika ngazi hiyo yatawasilishwa kwa Makatibu Wakuu watakaokutana tarehe 21 Mei, 2026 kabla ya kuwasilishwa katika Mkutano wa Baraza la Mawaziri utakaofanyika tarehe 22 Mei, 2026.

Vilevile, mkutano huo wa siku tano kuanzia tarehe 18 hadi 22 Mei, 2026 unalenga kuweka mikakati ya pamoja ya utekelezaji wa maelekezo na maamuzi yaliyotolewa na Mkutano wa 25 wa Wakuu wa Nchi za EAC, hususan katika maeneo ya mipango na fedha

Baraza la Mawaziri la EAC ni chombo kikuu cha maamuzi na kusimamia shughuli za Jumuiya, katika hatua hii ya maandalizi ya bajeti, Baraza hilo lina jukumu la kupokea, kuchambua, kufanya marekebisho na kuidhinisha makadirio ya mapato na matumizi ya Sekretarieti ya EAC kabla ya kuwasilishwa katika Bunge la Afrika Mashariki (EALA) kwa ajili ya kujadiliwa na kupitishwa rasmi.

Ujumbe wa Tanzania katika mkutano huo unajumuisha wajumbe kutoka Wizara ya Fedha, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora pamoja na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, ukionaongozwa na Mkurugenzi wa Sera na Mipango kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Justin Kisoka.






Rais Samia Akutana na Mkurugenzi wa Miradi Benki ya Dunia Afrika


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye mazungumzo na aliyekuwa Mkurugenzi Mkazi wa Benki ya Dunia anayesimamia nchi za Malawi, Tanzania, Zambia na Zimbabwe, Bw. Nathan Belete, Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 18 Mei, 2026. Bw. Belete ambaye kwa sasa ni Mkurugenzi wa Miradi wa Benki ya Dunia Kanda ya Afrika, alifika Ikulu kwa ajili ya kumuaga Mhe. Rais Dkt. Samia mara baada ya kuhudumu katika nafasi yake ya awali kwa kipindi cha miaka minne. Pia aliambatana na mrithi wake Mkurugenzi Mkazi wa Benki hiyo anayesimamia nchi za Malawi, Tanzania, Zambia na Zimbabwe Bw. Firas Raad.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na aliyekuwa Mkurugenzi Mkazi wa Benki ya Dunia anayesimamia nchi za Malawi, Tanzania, Zambia na Zimbabwe, Bw. Nathan Belete ambaye kwa sasa ni Mkurugenzi wa Miradi ya Benki hiyo, Kanda ya Afrika, Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 18 Mei, 2026.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na aliyekuwa Mkurugenzi Mkazi wa Benki ya Dunia anayesimamia nchi za Malawi, Tanzania, Zambia na Zimbabwe, Bw. Nathan Belete ambaye kwa sasa ni Mkurugenzi wa Miradi wa Benki hiyo, Kanda ya Afrika, pamoja na Mkurugenzi Mkazi wa Benki ya Dunia anayesimamia nchi za Malawi, Tanzania, Zambia na Zimbabwe Bw. Firas Raad mara baada ya mazungumzo yao, Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 18 Mei, 2026.

NBAA Yatoa Mafunzo kwa Watumishi wa NAOT


Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA) imetoa mafunzo maalumu kwa watumishi 101 wa Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi (NAOT) kwa lengo la kuimarisha ujuzi wa kitaaluma, kuongeza ufanisi katika utendaji kazi pamoja na kuendana na mabadiliko ya kimataifa katika Taaluma ya Uhasibu na Ukaguzi.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo, Mkurugenzi Mtendaji wa NBAA, CPA Prof. Siasa Issa Mzenzi ameishukuru NAOT kwa kuendelea kushirikiana na NBAA katika kuwawezesha Wahasibu na Wakaguzi kupitia mafunzo mbalimbali ya kitaaluma, hususan mafunzo maalumu yaliyoandaliwa kwa watumishi wa ofisi hiyo.

Prof. Mzenzi amesema tangu alipoanza rasmi majukumu yake tarehe 30 Machi mwaka huu, amepokea salamu nyingi za pongezi kutoka kwa wadau mbalimbali wa Taaluma ya Uhasibu na Ukaguzi, jambo ambalo limempa hamasa ya kuendelea kuisukuma mbele Taaluma hiyo kupitia kaulimbiu ya “Moving the Profession Forward”.

Aidha, amempongeza aliyekuwa Mkurugenzi Mtendaji wa NBAA, CPA Pius A. Maneno, kwa mchango wake mkubwa wa zaidi ya miaka 20 katika kuimarisha Taaluma ya Uhasibu na Ukaguzi nchini. Amesema mafanikio mengi yanayoonekana leo katika Taaluma hiyo yametokana na uongozi na juhudi zake katika kipindi chote cha utumishi wake.

Katika hatua nyingine, Prof. Mzenzi amesisitiza umuhimu wa kuendelea kuimarisha ushirikiano kati ya NBAA na NAOT katika maeneo mbalimbali ikiwemo mafunzo, utawala bora pamoja na matumizi ya Viwango vya Kimataifa vya Uhasibu wa Sekta ya Umma (IPSAS).

Amesema Tanzania imeendelea kuwa mfano bora barani Afrika katika utekelezaji wa viwango vya IPSAS, huku nchi nyingi za Afrika zikiiangalia Tanzania kama kitovu cha kujifunza uzoefu na mafanikio katika utekelezaji wa viwango hivyo. Ameeleza kuwa mafanikio hayo yametokana na juhudi kubwa zinazofanywa na NAOT katika kuhakikisha Taasisi za umma zinaandaa taarifa za fedha zinazokidhi viwango vya kimataifa.

Sambamba na hilo, amewataka Wahasibu na Wakaguzi kujiandaa na mabadiliko mapya ya Taaluma, hususan katika eneo la Sustainability Reporting, akisema kuwa mfumo huo sasa ni sehemu muhimu ya taarifa za kifedha duniani. Ameongeza kuwa Serikali kupitia Wizara ya Fedha tayari imeanza kutoa mwongozo na ramani ya utekelezaji wa mfumo huo nchini.

Naye mwakilishi wa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Charles E. Kichere, amesema faida kubwa ya mafunzo hayo ni ushirikiano uliopo kati ya NBAA na NAOT katika kuandaa muundo wa mafunzo unaoendana na hali halisi pamoja na changamoto zinazojitokeza katika utekelezaji wa majukumu ya Ukaguzi wa hesabu za Serikali.

“Tumekuwa na muundo maalumu wa ratiba ya mafunzo haya ili kuhakikisha yanakuwa yenye tija na yanakidhi mahitaji halisi ya washiriki. Kabla ya kuanza rasmi kwa mafunzo, tulipata fursa ya kushirikiana kwa karibu katika kuandaa mada mbalimbali, jambo lililowezesha kuwepo kwa majadiliano yanayoakisi mazingira halisi ya kazi pamoja na changamoto zinazokabili Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Serikali,” amesema.

Aidha, amesema ushirikiano huo umewezesha NBAA kutoa nafasi kwa wakufunzi wa ndani pamoja na wakufunzi kutoka NAOT kushiriki katika kuendesha mafunzo hayo, hatua ambayo imeongeza ubora wa mafunzo na kuimarisha ushirikiano wa kitaaluma kati ya Taasisi hizo mbili.

Vilevile, amewapongeza watumishi wa NAOT kwa ushiriki wao mzuri katika mafunzo hayo, akieleza kuwa ushiriki huo ni ishara ya dhamira ya kuendelea kujifunza na kuongeza ufanisi katika utendaji wa kazi.

Mafunzo hayo yanatarajiwa kuongeza ujuzi wa kitaaluma kwa washiriki na kuimarisha uwezo wao katika kutekeleza majukumu ya Ukaguzi na usimamizi wa fedha za umma kwa ufanisi zaidi.
Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA), CPA Prof. Siasa Issa Mzenzi akizungumza na watumishi wa Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi (NAOT) alipokuwa anafungua mafunzo ya siku mbili yaliyofanyika katika Ukumbi wa Hoteli ya APC, Bunju jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa Huduma za Utafiti, Viwango na Uhasibu wa NBAA, CPA Angyelile Tende akizungumza kuhusu namna wanavyoshirikiana na Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi (NAOT) katika utoaji wa Mafunzo kwa watumishi wao wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya Siku mbili yaliyofanyika katika Ukumbi wa Hoteli ya APC, Bunju jijini Dar es Salaam.

Mkufunzi wa Mafunzo hayo, CPA. Dkt. Neema Kiure Mssusa akiendelea kutoa mada kwa watumishi wa Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi (NAOT)
Watumishi wa Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi (NAOT) wakifuatilia hotuba ya mgeni rasmi Mkurugenzi Mtendaji wa NBAA, CPA Prof. Siasa Issa Mzenzi wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya Siku mbili kwa watumishi hao.
Mkurugenzi Mtendaji wa NBAA, CPA Prof. Siasa Issa Mzenzi akiwa kwenye picha ya pamoja na Watumishi wa Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi (NAOT), watoa mada pamoja na baadhi ya watumishi wa NBAA.