HABARI

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

MATUKIO

MICHEZO

SIASA

WATUMISHI WA TCAA WASHIRIKI MAADHIMISHO YA MEI MOSI

Wafanyakazi wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) wameungana na wafanyakazi wengine duniani kushiriki katika Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani (Mei Mosi), ambayo kwa mwaka huu yameadhimishwa kitaifa katika Mkoa wa Singida, yakiongozwa na Mgeni Rasmi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Maadhimisho hayo yamebeba kauli mbiu isemayo “Uchaguzi Mkuu 2025 utuletee viongozi wanaojali haki na maslahi ya wafanyakazi, sote tushiriki,” ikisisitiza umuhimu wa ushiriki wa wafanyakazi katika mchakato wa uchaguzi kwa ajili ya mustakabali bora wa haki zao.

Katika kilele cha sherehe hizo, Mhe. Rais Dkt. Samia ametangaza habari njema kwa wafanyakazi wote nchini kwa kutangaza ongezeko la kima cha chini cha mshahara kwa asilimia 35, hatua inayolenga kuboresha maisha ya mfanyakazi na kutambua mchango wao katika ujenzi wa taifa.

Aidha, Maadhimisho ya Mei Mosi yameendelea kufanyika katika maeneo mbalimbali nchini, ambapo Visiwani Zanzibar yaliongozwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, yakibeba kauli mbiu “Wafanyakazi tufanye kazi kwa bidii na nidhamu, tudai haki zetu kwa mujibu wa sheria na tushiriki katika Uchaguzi Mkuu kwa amani.”

Kwa upande wa Mkoa wa Dar es Salaam, maadhimisho hayo yamefanyika kwa mafanikio makubwa yakiongozwa na Mkuu wa Mkoa huo, Mhe. Albert Chalamila.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akiwa na Makamu wa Rais Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango, Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa, Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Mhe. Dkt. Doto Mashaka Biteko, Spika wa Bunge Mhe. Dkt. Tulia Ackson pamoja na Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi (TUCTA) Tumaini Nyamhokya wakiimba Wimbo wa Mshikamano (Solidarity Forever) kwenye Maadhimisho ya Siku wa Wafanyakazi Duniani Mei Mosi ambapo Kitaifa Sherehe hizo zimefanyika katika uwanja wa Bombadia Mkoani Singida tarehe 01 Mei, 2025.
Baadhi ya Watumishi wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) wakipita mbele ya Jukwaa Kuu huku wakiwa na bango lenye ujumbe kuhusiana Wafanyakazi wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani yaliyofanyika uwanja wa Bombadia Mkoani Singida tarehe 01 Mei, 2025.
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi akipokea zawadi kutoka kwa Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi TCAA Bi. Mtumwa Ameir alipotembelea banda la Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) kwenye Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani yaliyofanyika Kizimkazi, Unguja.
Baadhi ya Watumishi wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) Zanzibar wakiwa kwenye maandamano ya Siku ya Wafanyakazi Duniani yaliyofanyika Kizimkazi, Unguja.
Gari lililobeba ujumbe wa TCAA katika maadhimisho ya Mei Mosi Kizimkazi  Kusini Unguja, Zanzibar. Gari hilo lilionyesha namna Wafanyakazi wa TCAA wanavyotoa huduma za Uongozaji ndege wakiwa kazini.
Baadhi ya Watumishi wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) Dar es Salaam wakiwa katika maandamano wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani yaliyofanyika katika Viwanja vya Tanganyika Packers Kawe wilaya ya Kinondoni jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya Watumishi wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) Dar es Salaam wakipita mbele ya Jukwaa Kuu huku wakiwa na bango lenye ujumbe kuhusiana Wafanyakazi wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani yaliyofanyika katika Viwanja vya Tanganyika Packers Kawe wilaya ya Kinondoni jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya Watumishi wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) Dar es Salaam wakiwa kwenye picha ya pamoja wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani yaliyofanyika katika Viwanja vya Tanganyika Packers Kawe wilaya ya Kinondoni jijini Dar es Salaam.

MAKAMU WA PILI WA RAIS ZANZIBAR ATEMBELEA BANDA LA TCAA KATIKA MAONESHO YA MEI MOSI KIZIMKAZI, UNGUJA


 Katika kuadhimisha Maonesho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani (Mei Mosi), Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Mheshimiwa Hemed Suleiman Abdulla, ametembelea banda la Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA).

Akiwa banda la TCAA , Mheshimiwa Hemed alipata maelezo kuhusu huduma na majukumu ya TCAA pamoja na miradi inayoitekeleza kutoka kwa Meneja wa Kituo cha TCAA katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume(AAKIA), Bw. Mohamed Ali Mohamed.

Katika maelezo yake, Bw. Mohamed pia alimueleza Mheshiwa Hemed namna TCAA inavyosimamia usalama wa safari za anga, kuratibu huduma za Uongozaji ndege, pamoja na kuendeleza teknolojia za kisasa kuhakikisha kunakuwa na ufanisi na maendeleo ya sekta ya usafiri wa anga nchini na visiwa vya Zanzibar kwa ujumla.

Mheshimiwa Hemed alipongeza jitihada za TCAA katika kuimarisha huduma za usafiri wa anga na kuhimiza mamlaka hiyo kuendelea kuboresha huduma kwa maslahi ya taifa na wananchi.

Maonesho hayo ya Mei Mosi yanazileta pamoja taasisi mbalimbali za serikali na sekta binafsi kuonesha huduma na mafanikio yao katika kuunga mkono maendeleo ya kitaifa.

Meneja wa Kituo cha TCAA katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume(AAKIA), Bw. Mohamed Ali Mohamed akitoa maelezo kwa Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Mheshimiwa Hemed Suleiman Abdulla kuhusu kazi mbalimbali zinazofanywa na mamlaka hiyo kwenye maonesho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani (Mei Mosi)


Katibu Mkuu Uchukuzi atembelea Banda la TCAA


Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania(TCAA) inashiriki katika Maonesho ya 73 ya Baraza la Kimataifa la Viwanja vya Ndege (ACI Africa) na imepata fursa ya kutembelewa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi Prof. Godius Kahyarara.

Maonyesho hayo yanafanyika katika viwanja vya Mount Meru Hotel, yanayofanyika sambamba na Mkutano wa 73 wa Baraza la Kimataifa la Viwanja vya Ndege – ACI Kanda ya Afrika.

Akiwa bandani, Prof. Kahyarara alipokelewa na Mkurugenzi Mkuu wa TCAA, Bw. Salim Msangi, ambaye alimueleza juhudi mbalimbali zinazofanywa na Mamlaka hiyo katika kuimarisha sekta ya usafiri wa anga nchini, ikiwemo maboresho ya miundombinu, usalama wa safari za anga, na kuhimiza matumizi ya teknolojia za kisasa.

Maonesho hayo yanawaleta pamoja wadau kutoka sekta ya viwanja vya ndege ndani na nje ya Afrika, kwa lengo la kubadilishana uzoefu na kuonesha maendeleo ya huduma za usafiri wa anga.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi, Prof. Godius W. Kahyarara akipata maelezo kutoka kwa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA), Bw. Salim Msangi wakati wa ufunguzi wa Maonesho ya 73 ya Baraza la Kimataifa la Viwanja vya Ndege (ACI Africa) yanayofanyika jijini Arusha.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi, Prof. Godius W. Kahyarara akizungumza jambo katika banda la Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) wakati wa ufunguzi wa Maonesho ya 73 ya Baraza la Kimataifa la Viwanja vya Ndege (ACI Africa) yanayofanyika jijini Arusha. Wa kwanza kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA), Bw. Salim Msangi.
Mkufunzi Mkuu wa kitengo cha Uongozaji Ndege kutoka Chuo cha Usafiri wa Anga (CATC) , Godlove Longole akitoa maelezo kwa baadhi ya wadau wa Usafiri wa anga waliofika katika Banda la Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) wakati wa ufunguzi wa Maonesho ya 73 ya Baraza la Kimataifa la Viwanja vya Ndege (ACI Africa) yanayofanyika jijini Arusha.
Kaimu Meneja wa Mawasiliano TCAA, Ally Changwila(kushoto) akitoa maelezo kuhusu kazi zinazofanywa na Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) wakati wa ufunguzi wa Maonesho ya 73 ya Baraza la Kimataifa la Viwanja vya Ndege (ACI Africa) yanayofanyika jijini Arusha.

KATIBU MKUU UCHUKUZI AZINDUA MAONESHO YA 73 YA ACI AFRICA, ATEMBELEA BANDA LA TAA


Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi, Prof. Godius W. Kahyarara akikata utepe kuashiria uzinduzi wa wa Maonesho ya 73 ya Baraza la Kimataifa la Viwanja vya Ndege (ACI Africa) yanayofanyika jijini Arusha.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi, Prof. Godius W. Kahyarara akipata maelezo kutoka kwa Meneja Mipango, Usanifu na Uthamini kutoka Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA) Mhandisi Diana Munubi baada ya kutembelea Bando la Mamlaka hiyo wakati wa ufunguzi wa Maonesho ya 73 ya Baraza la Kimataifa la Viwanja vya Ndege (ACI Africa) yanayofanyika jijini Arusha.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi, Prof. Godius W. Kahyarara akisaini kitabu mara baada ya kutembelea banda la Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA) wakati wa uzinduzi wa Maonesho ya 73 ya Baraza la Kimataifa la Viwanja vya Ndege (ACI Africa) yanayofanyika jijini Arusha.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi, Prof. Godius Kahyarara akipokea zawadi kutoka kwa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Abdul Mombokaleo mara baada ya kutembelea banda la TAA wakati wa ufunguzi wa Maonesho ya 73 ya Baraza la Kimataifa la Viwanja vya Ndege (ACI Africa) yanayofanyika jijini Arusha.

UNCDF na Washirika wake Waja na Mkakati Mpya Kukabili Mabadiliko ya Tabianchi


Mfuko wa Maendeleo ya Mitaji wa Umoja wa Mataifa (UNCDF) pamoja na washirika wake wa maendeleo wameandaa warsha ya kitaifa ya siku tatu yenye lengo la kuimarisha ushirikiano wa wadau na kuongeza uelewa na uwezo wa jinsi kuainisha vipaumbele vya kukabiliana na mabadiliko ya Tabianchi katika Awamu ya Pili ya utekelezaji wa program ya LoCAL nchini Tanzania.

Washirika wa maendeleo wa UNCDF ni Ubalozi wa Norway nchini Tanzania, Ubalozi wa Ubelgiji nchini Tanzania, Umoja wa Ulaya, na Ubalozi wa Ireland nchini Tanzania.

Akizungumza kwemye warsha hiyo Mratibu wa mradi wa Mabadiliko ya tabianchi wa UNCDF- LoCAL, Aine Mushi amesema lengo la warsha hiyo ni kuimarisha uelewa na uwezo wa kukabiliana na mabadiliko ya Tabianchi na uhimilivu kwa mendeleo endelevu nchini Tanzania.

Pia amesema warsha hii imewakutanisha wadau mbalimbali wanaoshughulika na jitihada mbali mbali za kuweza kupambana na athari za mabadiliko ya Tabianchi zikiwemo taasisi za Serikali, washirika wa maendeleo, Mamlaka za Serikali za Mitaa (LGA), washauri waelekezi na taasisi za elimu ya juu za utafiti ambapo washiriki 80 wamehudhuria warsha hiyo.

“Tunawajengea uwezo kuhusu mpango wa LoCAL kama jukwaa la kuendeleza harakati za kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi na uwezo wa kupanga vipaumbele na kuingiza vifungu kwenye bajeti ya Mamlaka za Serikali za Mitaa ili kujenga uhimilivu wa mabdiliko ya tabianchi kwa wananchi kwa kutumia mbinu shirikishi na zinazozingatia usawa wa kijinsia.” Alisema Mushi
Afisa Misitu Mkuu kutoka Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Ofisi ya Rais - TAMISEMI) Rogacian Lukoa akizungumza kuhusu namna serikali ilivyojipanga kushirikiana na wadau wa maendeleo ili kuweza kukabiliana na mabadiriko ya Tabianchi.
Mshauri wa Kanda wa Mrasi wa LoCAL - UNCDF Jenifer Bukokhe Wakhungu akizungumza kuhusus namna shirika hilo lilivojipanga kuendelea kutoa mafunzo mbalimbali ili kuongeza uwezo wa serikali , halmashauri na vijiji kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi hapa nchini.
Afisa Mazingira Mkuu kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais(VPO) Mhandisi Mwanasha Rajabu Tumbo akitoa salamu za ofisi hiyo wakati wa warsha ya kitaifa kwa lengo la kuimarisha ushirikiano wa wadau na kuongeza uelewa na uwezo wa jinsi kuainisha vipaumbele vya kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi katika Awamu ya Pili ya utekelezaji wa program ya LoCAL nchini Tanzania.
Mkuu wa Ushirikiano na Maendeleo kutoka Ubalozi wa Ubeligiji nchini Tanzania Fanny Heylen akizungumzia ushirikiano wa Ubalozi huo na Mfuko wa Maendeleo ya Mitaji wa Umoja wa Mataifa(UNCDF).
Mshauri Mwandamizi wa Kilimo, Mabadiliko ya Tabianchi, na Utafiti kutoka Ubalozi wa Norway, Bw. Yassin Mkwizu akitoa salamu za ubalozi huo kwa wadau mbalimbali kwenye warsha iliyoandaliwa na Mfuko wa Maendeleo ya Mitaji wa Umoja wa Mataifa(UNCDF) pamoja na washirika wake.
Mratibu wa mradi wa Mabadiliko ya Tabianchi wa UNCDF- LoCAL, Aine Mushi akiwasirisha mada kwa wadau mbalimbali kutoka taasisi za Serikali, washirika wa maendeleo, Mamlaka za Serikali za Mitaa (LGA), washauri waelekezi na taasisi za elimu ya juu za utafiti wakati wa warsha hiyo.

Baadhi ya wadau mbalimbali kutoka taasisi za Serikali, washirika wa maendeleo, Mamlaka za Serikali za Mitaa (LGA), washauri waelekezi na taasisi za elimu ya juu za utafiti wakifuatilia mada kwenye warsha hiyo.
Picha za pamoja