HABARI

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

MATUKIO

MICHEZO

SIASA

TAZAMA HAPA RATIBA YA MICHEZO YOTE YA KOMBE LA DUNIA 2026



TANZANIA YASHIRIKI MKUTANO WA AFIAAR PORT LOUIS, MAURITIUS


Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA) imeshiriki katika Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Jukwaa la Wasimamizi wa Taaluma ya Ukaguzi Afrika (African Forum of Independent Accounting and Auditing Regulators (AFIAAR) wa mwaka 2026, unaofanyika mjini Port Louis, Mauritius kuanzia tarehe 2 hadi 5 Juni 2026.

Katika Mkutano huo, Mkurugenzi Mtendaji wa NBAA, CPA Prof. Siasa Mzenzi, alichaguliwa kuwa Makamu Mwenyekiti wa AFIAAR. Pamoja na Mkurugenzi Mtendaji, NBAA imewakilishwa na CPA Pius Maneno, Mkurugenzi Mtendaji Mstaafu wa NBAA na Makamu Mwenyekiti anayemaliza muda wake wa jukwaa hilo; CPA Winnington Makaka, Mkuu wa Sehemu ya Ubora wa Ukaguzi (AQR); pamoja na Magreth Kageya, Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano na Mawasiliano cha NBAA.

Lengo la mkutano huo ni kuwakutanisha wasimamizi wa taaluma ya Uhasibu na Ukaguzi barani Afrika ili kujadili masuala mbalimbali yanayohusu taaluma hiyo, hususan hali ya ubora wa ukaguzi. Majadiliano hayo yanalenga kuimarisha ubora wa taarifa za ukaguzi wa makampuni, jambo litakalosaidia kukuza uchumi wa Afrika kwa kuongeza imani ya wawekezaji kupitia taarifa sahihi na za kuaminika za kifedha.

Akizungumza katika mkutano huo, Mkurugenzi Mtendaji wa NBAA na Makamu Mwenyekiti wa AFIAAR, CPA Prof. Siasa Mzenzi, alisema: “Mkutano huu ni muhimu kwa taasisi yetu na Tanzania kwa ujumla, kwani umetupatia fursa ya kujifunza na kubadilishana uzoefu kuhusu mbinu bora za usimamizi wa taaluma ya ukaguzi. Maarifa haya yatasaidia kuboresha ubora wa huduma za ukaguzi nchini na hivyo kuongeza uaminifu wa taarifa za kifedha zinazotolewa na taasisi na makampuni mbalimbali.”

Mkutano wa AFIAAR unawakutanisha wadau mbalimbali wa usimamizi wa taaluma ya ukaguzi kutoka nchi mbalimbali za Afrika kwa lengo la kuimarisha ushirikiano, kubadilishana uzoefu na kujadili mikakati ya kuendeleza ubora wa ukaguzi barani humo.










NBAA na BoT Wajadili Teknolojia katika Sekta ya Fedha



Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA), kwa kushirikiana na Benki Kuu ya Tanzania (BOT), imeandaa semina ya pamoja uliyowakutanisha wataalamu wa Uhasibu, Wakaguzi wa hesabu na wadau wa sekta ya fedha kutoka ndani na nje ya nchi iliyoanza tarehe 25 hadi 27, Mei, 2026.

Akifungua rasmi semina hiyo iliofanyika jijini Arusha, Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT) Emmanuel Tutuba, amewataka wataalamu wa fedha na Ukaguzi nchini kuhamasisha matumizi ya mifumo ya kidijitali katika miamala ya kifedha ili kupunguza matumizi ya fedha taslimu pamoja na vihatarishi vinavyoweza kujitokeza katika sekta ya fedha.

Tutuba amesema matumizi makubwa ya teknolojia katika huduma za kifedha yataisaidia Tanzania kudhibiti uvujaji wa fedha, kuongeza uwazi wa miamala na kuimarisha usalama wa mifumo ya kifedha nchini.

Ametoa wito huo katika semina ya pamoja ya wataalamu wa Uhasibu na Ukaguzi wa hesabu (NBAA) inayofanyika Jijini Arusha, akisisitiza umuhimu wa kusimamia masuala ya mabadiliko ya Tabianchi, mazingira, utawala bora pamoja na vihatarishi vinavyojitokeza kwenye sekta ya fedha kwa kuzingatia viwango vya kimataifa.

Aidha Tutuba amesema Tanzania imeendelea kuwa na uchumi himilivu licha ya changamoto za uchumi wa dunia, huku akibainisha kuwa usimamizi mzuri wa sekta ya fedha na utekelezaji wa mifumo endelevu vitasaidia Taifa kufikia dira ya uchumi wa trilioni moja.

Kwa Upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA) CPA Prof. Siasa Issa Mzenzi amesema miongoni mwa mambo watakaojadili na kujifunza ni Pamoja na matumizi ya TEHAMA katika masuala yote ya fedha kupitia.

Mafunzo hayo yaliyoandaliwa na NBAA na Benki Kuu ya Tanzania (BoT) yanalenga kuimarisha mfumo wa fedha endelevu kwa kutumia teknolojia sambamba na kuzingatia misingi ya mazingira, kijamii na utawala bora katika sekta ya fedha nchini.
Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BOT), Emmanuel Tutuba akizungumza wakati wa kufungua semina ya pamoja iliyoandaliwa na NBAA na BOT iliyofanyika jijini Arusha
Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA) CPA Prof. Siasa Issa Mzenzi akizungumza wakati wa ufunguzi wa semina ya pamoja iliyoandaliwa na NBAA na BOT iliyowakutanisha wataalamu wa Uhasibu, Wakaguzi wa hesabu na wadau wa sekta ya fedha kutoka ndani na nje ya nchi.
Baadhi ya wataalamu wa Uhasibu, Ukaguzi wa hesabu na wadau wa sekta ya fedha kutoka ndani na nje ya nchi wakifuatilia ufunguzi wa Semina ya pamoja iliyoandaliwa na NBAA na BOT
Picha za pamoja

Rais Samia ashiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali kuhusu Uvumbuzi wa Nishati ya Nyuklia barani Afrika (NEISA), Kigali nchini Rwanda


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza katika Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali kuhusu Uvumbuzi wa Nishati ya Nyuklia barani Afrika (NEISA), Kigali nchini Rwanda tarehe 19 Mei, 2026. Mkutano huo wa Kimataifa unawakutanisha pia wataalamu wa nishati, wawekezaji na mashirika ya kimataifa, ambapo utajadili matumizi ya nishati ya nyuklia kwa maendeleo ya Bara la Afrika. Mkutano huo pia unalenga kujadili namna bora ya kuongeza upatikanaji wa nishati ya umeme Afrika, kupunguza uchafuzi wa mazingira, kusaidia maendeleo ya viwanda, kukuza ubunifu wa teknolojia za nishati ya nyuklia pamoja na kuvutia wawekezaji katika miradi ya nishati tarehe, 19 Mei, 2026.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha ya pamoja na Viongozi mbalimbali walioshiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali kuhusu Uvumbuzi wa Nishati ya Nyuklia barani Afrika (NEISA), Kigali nchini Rwanda tarehe 19 Mei, 2026. Mkutano huo wa Kimataifa unawakutanisha pia wataalamu wa nishati, wawekezaji na mashirika ya kimataifa, ambapo utajadili matumizi ya nishati ya nyuklia kwa maendeleo ya Bara la Afrika. Mkutano huo pia unalenga kujadili namna bora ya kuongeza upatikanaji wa nishati ya umeme Afrika, kupunguza uchafuzi wa mazingira, kusaidia maendeleo ya viwanda, kukuza ubunifu wa teknolojia za nishati ya nyuklia pamoja na kuvutia wawekezaji katika miradi ya nishati, tarehe 19 Mei, 2026.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akitembelea maonyesho wakati wa Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali kuhusu Uvumbuzi wa Nishati ya Nyuklia barani Afrika (NEISA), Kigali nchini Rwanda tarehe 19 Mei, 2026. Mkutano huo wa Kimataifa unawakutanisha pia wataalamu wa nishati, wawekezaji na mashirika ya kimataifa, ambapo utajadili matumizi ya nishati ya nyuklia kwa maendeleo ya Bara la Afrika. Mkutano huo pia unalenga kujadili namna bora ya kuongeza upatikanaji wa nishati ya umeme Afrika, kupunguza uchafuzi wa mazingira, kusaidia maendeleo ya viwanda, kukuza ubunifu wa teknolojia za nishati ya nyuklia pamoja na kuvutia wawekezaji katika miradi ya nishati, tarehe 19 Mei, 2026.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan pamoja na Viongozi mbalimbali wakishiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali kuhusu Uvumbuzi wa Nishati ya Nyuklia barani Afrika (NEISA), Kigali nchini Rwanda tarehe 19 Mei, 2026. Mkutano huo wa Kimataifa unawakutanisha pia wataalamu wa nishati, wawekezaji na mashirika ya kimataifa, ambapo utajadili matumizi ya nishati ya nyuklia kwa maendeleo ya Bara la Afrika. Mkutano huo pia unalenga kujadili namna bora ya kuongeza upatikanaji wa nishati ya umeme Afrika, kupunguza uchafuzi wa mazingira, kusaidia maendeleo ya viwanda, kukuza ubunifu wa teknolojia za nishati ya nyuklia pamoja na kuvutia wawekezaji katika miradi ya nishati.

Rais Dkt. Samia Aelekea Rwanda Kushiriki Mkutano wa Nishati ya Nyuklia Afrika




Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiagana na viongozi mbalimbali kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) Jijini Dar es Salaam kabla ya kuondoka nchini, kuelekea Kigali, Rwanda kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali kuhusu Uvumbuzi wa Nishati ya Nyuklia barani Afrika (NEISA) tarehe 19 Mei, 2026. Mkutano huo wa Kimataifa unawakutanisha pia wataalamu wa nishati, wawekezaji na mashirika ya kimataifa, ambapo utajadili matumizi ya nishati ya nyuklia kwa maendeleo ya Bara la Afrika. Mkutano huo pia unalenga kujadili namna bora ya kuongeza upatikanaji wa nishati ya umeme Afrika, kupunguza uchafuzi wa mazingira, kusaidia maendeleo ya viwanda, kukuza ubunifu wa teknolojia za nishati ya nyuklia pamoja na kuvutia wawekezaji katika miradi ya nishati.

Baraza la Mawaziri la EAC kukutana kwa Dharura jijini Arusha


Maandalizi ya Mkutano wa 60 wa Dharura wa Baraza la Mawaziri la Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), unaotarajiwa kufanyika tarehe 22 Mei 2026, yameanza rasmi kupitia vikao vya ngazi ya wataalamu vinavyoendelea kuanzia tarehe 18 hadi 20 Mei 2026 katika Makao Makuu ya Jumuiya hiyo jijini Arusha.

Kikao hicho cha wataalamu kimepokea na kujadilia taarifa ya Kamati ya Fedha na Utawala kuhusu masuala ya fedha ya Jumuiya, na rasimu ya bajeti ya Sekretarieti ya EAC pamoja na taasisi zake kwa mwaka wa fedha 2026/2027. Mapendekezo yatakayopitishwa katika ngazi hiyo yatawasilishwa kwa Makatibu Wakuu watakaokutana tarehe 21 Mei, 2026 kabla ya kuwasilishwa katika Mkutano wa Baraza la Mawaziri utakaofanyika tarehe 22 Mei, 2026.

Vilevile, mkutano huo wa siku tano kuanzia tarehe 18 hadi 22 Mei, 2026 unalenga kuweka mikakati ya pamoja ya utekelezaji wa maelekezo na maamuzi yaliyotolewa na Mkutano wa 25 wa Wakuu wa Nchi za EAC, hususan katika maeneo ya mipango na fedha

Baraza la Mawaziri la EAC ni chombo kikuu cha maamuzi na kusimamia shughuli za Jumuiya, katika hatua hii ya maandalizi ya bajeti, Baraza hilo lina jukumu la kupokea, kuchambua, kufanya marekebisho na kuidhinisha makadirio ya mapato na matumizi ya Sekretarieti ya EAC kabla ya kuwasilishwa katika Bunge la Afrika Mashariki (EALA) kwa ajili ya kujadiliwa na kupitishwa rasmi.

Ujumbe wa Tanzania katika mkutano huo unajumuisha wajumbe kutoka Wizara ya Fedha, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora pamoja na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, ukionaongozwa na Mkurugenzi wa Sera na Mipango kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Justin Kisoka.