HABARI

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

MATUKIO

MICHEZO

SIASA

TCAA Yavutia Viongozi wa Serikali Maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma


Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi, Prof. Godius W. Kahyarara akisaini kitabu katika banda la Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) kwenye maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayofanyika katika viwanja vya Chinangali Park, jijini Dodoma.
Meneja wa TCAA Kituo cha Dodoma Aswile Kamendu akitoa maelezo kwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi, Prof. Godius W. Kahyarara aliyefika katika banda la Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) kwenye maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayofanyika katika viwanja vya Chinangali Park, jijini Dodoma.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi, Prof. Godius W. Kahyarara akipokea zawadi kutoka kwa Meneja wa TCAA Kituo cha Dodoma Aswile Kamendu alipotembelea banda la Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) kwenye maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayofanyika katika viwanja vya Chinangali Park, jijini Dodoma.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi, Prof. Godius W. Kahyarara akizungumza jambo katika banda la Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) kwenye maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayofanyika katika viwanja vya Chinangali Park, jijini Dodoma.
Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Juma Mkomi akisaini kitabu katika banda la Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) kwenye maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayofanyika katika viwanja vya Chinangali Park, jijini Dodoma.

Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Juma Mkomi akiwa kwenye picha ya pamoja na Watumishi wa TCAA alipotembelea katika banda la Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) kwenye maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayofanyika katika viwanja vya Chinangali Park, jijini Dodoma.
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA), Dkt. Habibu J. Suluo akisaini kitabu katika banda la Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) kwenye maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayofanyika katika viwanja vya Chinangali Park, jijini Dodoma.

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA), Dkt. Habibu J. Suluo akizungumza jambo alipotembelea banda la Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) kwenye maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayofanyika katika viwanja vya Chinangali Park, jijini Dodoma.

Mkuu wa Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima (TEWW), Prof. Philipo Sanga akisaini kitabu katika banda la Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) kwenye maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayofanyika katika viwanja vya Chinangali Park, jijini Dodoma.

Afisa Rasilimali Watu TCAA Lucy Ngowo (wa pili kulia) akikabidhi zawadi kwa Mkuu wa Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima (TEWW), Prof. Philipo Sanga alipotembelea banda la Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) kwenye maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayofanyika katika viwanja vya Chinangali Park, jijini Dodoma.


Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi, Prof. Godius Kahyarara, Juni 22, 2026 alitembelea banda la Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) katika Maonesho ya Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma, yanayofanyika katika viwanja vya Chinangali Park, jijini Dodoma.

Akiwa katika banda hilo, Prof. Kahyarara alipokewa na Meneja wa TCAA Kituo cha Dodoma, Aswile Kamendu, ambaye alimueleza juhudi mbalimbali zinazotekelezwa na Mamlaka katika kuimarisha sekta ya usafiri wa anga nchini, ikiwemo maboresho ya miundombinu ya anga, kuimarisha usalama wa safari za anga pamoja na kuhimiza matumizi ya teknolojia za kisasa katika utoaji wa huduma.

Akizungumza mara baada ya kutembelea banda hilo, Prof. Kahyarara alisema: “Serikali inaendelea kuwekeza katika kuimarisha sekta ya usafiri wa anga kwa kuhakikisha miundombinu inaboreshwa, usalama unaimarishwa na teknolojia za kisasa zinatumika ili kuongeza ufanisi wa huduma. Hatua hizi ni muhimu katika kuchochea maendeleo ya uchumi na kuimarisha ushindani wa nchi yetu kikanda na kimataifa.”

Mbali na Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi, wageni wengine waliotembelea banda la TCAA ni pamoja na Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Juma Mkomi, Mkuu wa Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima (TEWW), Prof. Philipo Sanga, na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA), Dkt. Habibu J. Suluo, na kupata maelezo kuhusu majukumu ya Mamlaka, mafanikio yaliyopatikana pamoja na mikakati inayotekelezwa katika kuimarisha usalama, ufanisi na maendeleo ya sekta ya usafiri wa anga nchini.

Kupitia ushiriki wake katika maonesho hayo, TCAA inatumia fursa hiyo kuwahamasisha vijana na wadau wa sekta ya usafiri wa anga kuchangamkia fursa za mafunzo zinazotolewa na Chuo cha Usafiri wa Anga Tanzania (CATC), chuo kinachomilikiwa na TCAA. Mafunzo yanayotolewa chuoni hapo yanalenga kukabiliana na changamoto ya upungufu wa wataalamu wa ndani katika sekta ya usafiri wa anga kwa kuzalisha wataalamu wa kutosha na wenye viwango vinavyokubalika kimataifa.

Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma mwaka huu yanaongozwa na kaulimbiu isemayo “Kuchochea Uwajibikaji Jumuishi kwa Huduma Endelevu”, ikisisitiza umuhimu wa matumizi ya teknolojia katika kuboresha huduma kwa wananchi na kuimarisha uwajibikaji katika utumishi wa umma.

Wiki ya Utumishi wa Umma huadhimishwa kila mwaka kwa lengo la kutambua mchango wa watumishi wa umma katika maendeleo ya taifa, ambapo maadhimisho ya mwaka huu yanatarajiwa kufikia kilele chake Juni 23, 2026.



TCAA Yashiriki Wiki ya Utumishi wa Umma kwa Kutoa Elimu ya Usafiri wa Anga


Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) imeungana na Taasisi mbalimbali za umma kushiriki katika Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayofanyika katika viwanja vya Chinangali Park, jijini Dodoma kuanzia, Juni 16, 2026.

Katika maonesho hayo, TCAA inatoa elimu kwa wananchi kuhusu majukumu yake ya msingi, yakiwemo udhibiti wa shughuli zote za usafiri wa anga nchini. Hii inajumuisha pia usimamizi wa matumizi ya droni, ambalo ni eneo linalokua kwa kasi na kuhitaji ufuatiliaji wa karibu siyo tu kwa ajili ya usalama wa anga, bali pia kulinda faragha ya watu na kuepusha matumizi ya vifaa hivyo katika maeneo yasiyoruhusiwa kisheria, kama vile maeneo ya kijeshi, taasisi za serikali, na miundombinu nyeti.

Huduma nyingine zinazotolewa na TCAA ni pamoja na utoaji wa huduma za uongozaji ndege kwa ajili ya kuhakikisha usalama wa safari za anga ndani ya eneo la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Aidha, Mamlaka hiyo inatumia fursa hiyo kuwahamasisha vijana na wadau wa sekta ya usafiri wa anga kuchangamkia fursa za mafunzo zinazotolewa na Chuo cha Usafiri wa Anga Tanzania (CATC), kinachomilikiwa na TCAA. Mafunzo hayo yanalenga kuongeza idadi ya wataalamu wa ndani katika sekta muhimu ya usafiri wa anga.

Maadhimisho ya mwaka huu yanaongozwa na kaulimbiu: “Kuchochea uwajibikaji Jumuishi kwa Huduma Endelevu” ikisisitiza umuhimu wa matumizi ya teknolojia katika kuboresha huduma kwa wananchi na kuimarisha uwajibikaji katika utumishi wa umma.

Wiki ya Utumishi wa Umma huadhimishwa kila mwaka ili kutambua mchango wa watumishi wa umma katika maendeleo ya taifa. Maadhimisho ya mwaka huu yanatarajiwa kufikia kilele chake tarehe 23 Juni 2026.
Meneja wa TCAA Kituo cha Dodoma Aswile Kamendu (katikati) akitoa maelezo kwa Mkurugenzi wa Ufuatiliaji na Tathmini kutoka Wizara ya Uchukuzi Devota  Gabriel aliyefika katika banda la Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) kwenye maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayofanyika katika viwanja vya Chinangali Park, jijini Dodoma. 
Mkurugenzi wa Huduma za Usafiri kutoka Wizara ya Uchukuzi Biseko Chiganga  akisaini kitabu katika banda la Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) kwenye maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayofanyika katika viwanja vya Chinangali Park, jijini Dodoma. 
Afisa Rasilimali Watu TCAA Lucy Ngowo (wa pili kulia) akikabidhi zawadi kwa Mkurugenzi wa Huduma za Usafiri Wizara ya Uchukuzi ambaye pia ni Mjumbe wa Bodi Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA) Biseko Chiganga
Mkurugenzi wa Huduma za Usafiri kutoka Wizara ya Uchukuzi Biseko Chiganga akiwa kwenye picha pamoja na watumishi wa  Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) alipotembelea banda la Mamlaka hiyo kwenye maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayofanyika katika viwanja vya Chinangali Park, jijini Dodoma. 

Baadhi ya wafanyakazi wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) wakiendelea kutoa elimu katika Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yaliyofanyika kwenye Viwanja vya Chinangali jijini Dodoma.

NBAA YATEMBELEA BAOBA INSTITUTE OF TANZANIA


Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA) imeendelea na jitihada zake za kuhamasisha na kuendeleza Taaluma ya Uhasibu nchini kwa kutembelea Baobab Institute of Tanzania iliyopo Mapinga, Wilaya ya Bagamoyo mkoani Pwani, kwa lengo la kuwajengea wanafunzi uelewa kuhusu majukumu ya Bodi pamoja na fursa mbalimbali zilizopo katika Taaluma ya Uhasibu na Ukaguzi wa hesabu.

Ziara hiyo iliyofanyika Juni 12, 2026, ni sehemu ya programu endelevu ya NBAA ya kutoa elimu kwa wanafunzi wa vyuo, Taasisi za elimu na shule za sekondari nchini, ikiwa na lengo la kuongeza uelewa kuhusu shughuli za Bodi, kuhamasisha vijana kujiunga na Taaluma ya Uhasibu na kuwaandaa kwa fursa zinazopatikana katika soko la ajira.

Katika ziara hiyo, maafisa wa NBAA walikutana na wanafunzi pamoja na walimu wa Baobab Institute of Tanzania, Taasisi inayotoa kozi mbalimbali zikiwemo Uhasibu na Fedha. Wanafunzi walipata fursa ya kujifunza kwa undani kuhusu majukumu ya NBAA katika kusimamia, kudhibiti na kuendeleza Taaluma ya Uhasibu na Ukaguzi wa hesabu nchini.

Akizungumza na wanafunzi hao, maafisa wa NBAA walisisitiza umuhimu wa Taaluma ya Uhasibu katika kukuza uchumi wa taifa na kuimarisha uwajibikaji katika Taasisi za umma na binafsi. Waliwahimiza wanafunzi kujenga msingi imara wa taaluma zao kwa kuzingatia maadili, weledi na kujituma katika masomo yao.

Aidha, wanafunzi walipatiwa elimu kuhusu njia mbalimbali za kufikia sifa za kitaaluma za uhasibu, taratibu za usajili wa wahasibu na wakaguzi wa hesabu pamoja na fursa za ajira na maendeleo ya taaluma zinazoratibiwa na NBAA.

Ziara hiyo pia ilitoa fursa kwa wanafunzi kuuliza maswali mbalimbali kuhusu taaluma ya Uhasibu, mahitaji ya soko la ajira, matumizi ya teknolojia katika taaluma hiyo na hatua za kufuata ili kufikia hadhi ya mtaalamu wa Uhasibu. Wataalamu wa NBAA walijibu maswali hayo na kuwahimiza wanafunzi kuendana na mabadiliko ya teknolojia ili kuongeza ushindani wao katika soko la ajira.

Kwa upande wake, uongozi wa Baobab Institute of Tanzania umeishukuru NBAA kwa kutembelea Taasisi hiyo na kutoa elimu yenye manufaa kwa wanafunzi, ukieleza kuwa ziara hiyo imeongeza hamasa, maarifa na uelewa wa wanafunzi kuhusu taaluma ya uhasibu na mchango wake katika maendeleo ya taifa.

NBAA imeeleza kuwa itaendelea kutekeleza programu za uelimishaji kwa vijana katika taasisi mbalimbali za elimu nchini ili kuhakikisha wanapata taarifa sahihi kuhusu taaluma ya Uhasibu na fursa zinazopatikana, sambamba na kuchangia upatikanaji wa wataalamu wenye sifa na weledi unaohitajika katika maendeleo ya uchumi wa Tanzania.

Picha ya pamoja kati ya Watumishi wa NBAA pamoja na wakufunzi wa Baobab Institute of Tanzania.
Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano na Mawasiliano wa NBAA, Magreth Kageya akitoa ufafanuzi kuhusu kazi zinazofanywa na Bodi hiyo wakati wa mafunzo kwa wanachuo wa Baobab Institute of Tanzania.
Mfanyakazi wa Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA), Sawa Ngendabanka akizungumzia kuhusu usajili, madaraja mbalimbali ya mitihani ya Taaluma ya Uhasibu na jinsi ya kufanya mitihani hiyo.












Baadhi ya wanachuo pamoja na walimu wa Baobab Institute of Tanzania wakifuatilia mada zilizokuwa zinatolewa na wafanyakazi wa NBAA walipotembelea Taasisi hiyo.

Picha ya pamoja kati ya Watumishi wa NBAA, wakufunzi pamoja na wanachuo wa Baobab Institute of Tanzania.

MAFUNZO KWA WAFANYAKAZI WA TCAA YAWEKA MKAZO KATIKA UTENDAJI, USHIRIKISHWAJI WA WADAU NA MAENDELEO YA SEKTA YA ANGA


Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA), Dkt. Jabiri K. Bakari, amewataka watumishi wa Mamlaka hiyo kuendana na mabadiliko kwa kujenga utamaduni wa kupanga, kubuni, kushirikiana na kuwahusisha wadau katika utekelezaji wa majukumu yao, akieleza kuwa hatua hiyo ni muhimu katika kuimarisha utendaji wa taasisi na kuchochea maendeleo endelevu ya sekta ya usafiri wa anga nchini.

Dkt. Bakari alitoa rai hiyo wakati wa mafunzo maalum ya siku nne yaliyofanyika katika Chuo cha Uongozi cha Mwalimu Julius Nyerere, Kibaha, kuanzia Juni 5 hadi 8, yaliyowakutanisha viongozi na wawakilishi wa watumishi wa TCAA kutoka vituo mbalimbali nchini.

Mafunzo hayo yalitoa fursa kwa washiriki kutafakari utendaji wa Mamlaka, kujadili vipaumbele vya kimkakati na kubaini njia bora za kuimarisha utoaji wa huduma pamoja na ufanisi wa taasisi kwa ujumla.

Sehemu ya kwanza ya mafunzo ilijikita katika maendeleo binafsi na ujenzi wa timu kupitia programu iliyoendeshwa na Peak Performance. Kupitia shughuli mbalimbali za ndani na nje ya darasa, washiriki walishiriki mazoezi yaliyolenga kuimarisha mshikamano, kujenga kuaminiana, kuboresha mawasiliano na kuhamasisha mabadiliko chanya ya fikra na mtazamo.

Washiriki walihamasishwa kutafakari upya namna wanavyotekeleza majukumu yao, kujenga nidhamu binafsi, kuzingatia afya na ustawi wa mwili pamoja na kuendeleza tabia zinazochangia mafanikio ya mtu mmoja mmoja na taasisi kwa ujumla. Mafunzo hayo pia yalisisitiza umuhimu wa kujitambua, uwajibikaji na kuwa na mtazamo chanya katika kufanikisha malengo ya pamoja.

Moja ya matokeo muhimu ya mafunzo hayo ilikuwa kuandaliwa kwa waraka wa pamoja wa kujenga timu (Team Building Charter) unaoakisi maadili, matarajio na dhamira ya pamoja iliyojengwa wakati wa mafunzo hayo. Waraka huo unatarajiwa kuwa mwongozo wa kuimarisha utamaduni wa taasisi, kukuza ushirikiano na uwajibikaji, pamoja na kusaidia juhudi za Mamlaka katika kufikia ubora wa utendaji na utoaji huduma.

Katika kipindi chote cha mafunzo, washiriki pia walijadili masuala mbalimbali ya kimkakati ikiwemo utendaji wa Mamlaka, mipango ya bajeti, michakato ya kazi, ushirikishwaji wa wadau na fursa za kuboresha utoaji wa huduma. Majadiliano hayo yalitoa nafasi kwa viongozi na watumishi kutathmini changamoto zilizopo, kubaini fursa na kujadiliana kuhusu suluhisho zitakazosaidia kuimarisha ufanisi wa Mamlaka.

Akizungumza wakati wa mafunzo hayo, Dkt. Bakari alisisitiza umuhimu wa kuondokana na utamaduni wa kushughulikia matatizo baada ya kutokea na badala yake kujenga utamaduni wa kupanga, kufanya tafiti na kufanya maamuzi kwa kuzingatia taarifa sahihi na ushahidi.

Aliwataka watumishi kutumia tafiti, takwimu na taarifa za wakati halisi katika kuelewa mwenendo wa sekta na kufanya maamuzi yatakayosaidia kuimarisha huduma na kuongeza ufanisi wa utekelezaji wa majukumu ya Mamlaka.

Mkurugenzi Mkuu huyo pia alisisitiza umuhimu wa kuzingatia dhana ya “Know Your Customer” (KYC) kwa kuwafahamu kwa kina wadau wa sekta ya anga, kuelewa mahitaji yao na kujenga mahusiano mazuri yatakayowezesha utoaji wa huduma bora zaidi.

“Lazima tuwafahamu wateja na wadau wetu, tuelewe changamoto zao na mazingira wanayofanyia kazi. Uelewa mzuri wa wadau wetu utatuwezesha kufanya maamuzi sahihi, kuboresha utoaji wa huduma na kuchangia kwa ufanisi maendeleo ya sekta ya usafiri wa anga,” alisema.

Dkt. Bakari alisisitiza pia umuhimu wa kujenga na kuendeleza mahusiano imara na wadau mbalimbali wa sekta ya anga, akieleza kuwa ushirikiano, kuaminiana na mawasiliano endelevu ni nguzo muhimu katika kuhakikisha sekta hiyo inaendelea kukua kwa usalama, ufanisi na ushindani.

Aidha, aliwataka watumishi kufuatilia kwa karibu mwenendo wa sekta, kufanya tafiti na kutumia taarifa mbalimbali katika kuelewa changamoto na mahitaji ya wadau ili kusaidia kufanya maamuzi yenye tija kwa maendeleo ya sekta.

Kwa upande mwingine, Dkt. Bakari alisisitiza umuhimu wa afya na ustawi wa watumishi, akibainisha kuwa taasisi yenye watumishi wenye afya njema, ari ya kazi na mtazamo chanya ndiyo yenye uwezo mkubwa wa kufanikisha malengo yake. Aliwahimiza watumishi kuzingatia afya zao za mwili na akili ili kuwa na nguvu na uthabiti wa kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi.

Mafunzo hayo yalihitimishwa kwa washiriki kubaini suluhisho za changamoto mbalimbali za kiutendaji na kuthibitisha upya dhamira yao ya kuimarisha ushirikiano, ubunifu, ushirikishwaji wa wadau na utoaji wa huduma bora.

Majadiliano yaliyofanyika yanaakisi dira ya TCAA ya kujenga taasisi yenye utendaji wa hali ya juu inayoweza kuendelea kuisimamia na kuiendeleza sekta ya usafiri wa anga kwa usalama, ufanisi na kwa kuzingatia mahitaji ya wadau wake.

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA), Dkt. Jabiri K. Bakari akizungumza wakati wa mafunzo maalum ya siku nne ya kuimarisha utendaji wa taasisi na kuchochea maendeleo endelevu ya sekta ya usafiri wa anga nchini yaliyofanyika katika Chuo cha Uongozi cha Mwalimu Julius Nyerere, Kibaha mkoani Pwani.
Baadhi ya watumishi wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) wakiwa kwenye mafunzo ya  kuimarisha utendaji wa Taasisi hiyo.

RAIS SAMIA APITA NYENDO ZA NYERERE URUSI







WAZIRI wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mahmoud Thabit Kombo, amesema ziara ya Rais Samia Suluhu Hassan nchini Urusi imefufua kumbukumbu za miaka 57 iliyopita wakati Rais wa Kwanza wa Tanzania, Hayati Mwalimu Julius Nyerere, alipofanya ziara ya kitaifa nchini humo mwaka 1969.Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Balozi Kombo amesema viongozi hao wawili wamekuwa na mwelekeo unaofanana katika maeneo matatu makuu ya uchumi, siasa za kimataifa na kuimarisha nafasi ya Tanzania katika jukwaa la Dunia.

Amesema kama ilivyokuwa kwa Mwalimu Nyerere mwaka 1969, Rais Samia pia amehutubia katika Jiji la St. Petersburg, ambalo wakati huo lilijulikana kama Leningrad, na kutumia jukwaa hilo kueleza fursa za uwekezaji, biashara na utalii zilizopo Tanzania.

Ameongeza kuwa viongozi hao wote wawili walitumia majukwaa ya kimataifa kueleza msimamo wa Tanzania kuhusu masuala ya dunia na kusisitiza umuhimu wa amani, ushirikiano na maendeleo ya pamoja.

Kwa mujibu wa Balozi Kombo, hatua ya Rais Samia kushiriki Jukwaa la Kimataifa la Uchumi la St. Petersburg (SPIEF) na kufanya mazungumzo na viongozi mbalimbali ni mwendelezo wa diplomasia ya kimkakati iliyoasisiwa na Mwalimu Nyerere, yenye lengo la kuimarisha ushawishi wa Tanzania na kufungua fursa zaidi za maendeleo.

TAZAMA HAPA RATIBA YA MICHEZO YOTE YA KOMBE LA DUNIA 2026