HABARI

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

MATUKIO

MICHEZO

SIASA

WAZIRI DKT. BASHIRU AIAGIZA BODI MPYA YA TAFICO KUIGEUZA TAFICO KUWA INJINI YA UCHUMI SEKTA YA UVUVI


Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa, ameitaka Bodi mpya ya pili ya Shirika la Uvuvi Tanzania (TAFICO) kuhakikisha uwekezaji mkubwa uliofanywa na Serikali katika sekta ya uvuvi unatafsiriwa kuwa uzalishaji wa kibiashara, mapato na mchango mkubwa zaidi katika uchumi wa Taifa.

Akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa bodi hiyo iliyofanyika Julai 13, 2026, katika Ofisi za Makao Makuu ya TAFICO, Ras Mkwavi, Kigamboni jijini Dar es Salaam, Waziri Dkt. Bashiru alisema Bodi hiyo inaanza kazi katika kipindi muhimu ambacho Serikali imeweka msisitizo mkubwa katika kukuza uchumi wa buluu kupitia uwekezaji wa kimkakati kwenye sekta ya uvuvi ikiwa ni utekelezaji wa Dira ya Taifa 2050.

"Mnaanza kazi wakati ambao msingi wa uwekezaji umeanza kujengwa. Hivyo jukumu lenu ni kuhakikisha uwekezaji huo unazaa matokeo chanya ya kibiashara na ya maendeleo kwa Taifa," alisema Dkt. Bashiru.

Katika maelekezo yake, Waziri aliitaka Bodi kusimamia kwa karibu ukamilishaji wa miradi ya kimkakati ikiwemo uendeshaji wa meli ya uvuvi wa bahari kuu kwa utaratibu wa ubia (PPP), kuharakisha mabadiliko ya TAFICO kutoka hatua ya maandalizi kwenda uzalishaji halisi wa kibiashara, kupitia upya mpango mkakati na maandiko ya uwekezaji, kuimarisha upatikanaji wa rasilimali fedha, kujenga rasilimali watu yenye uwezo, kufanya maboresho ya muundo wa Shirika, kuendeleza ushirikiano na sekta binafsi pamoja na kuhakikisha uwazi, uwajibikaji na usimamizi wa mali zote za Shirika.

Akizungumza kwa niaba ya Bodi ya Wakurugenzi, Mwenyekiti wa Bodi ya TAFICO Prof. Yunus Daud Mgaya, aliishukuru Serikali kwa kuiamini Bodi hiyo kuiongoza TAFICO katika kipindi cha miaka mitatu, akiahidi kuwa Bodi itafanya kazi kwa weledi, uwajibikaji na ushirikiano wa karibu na Wizara pamoja na Menejimenti ili kuhakikisha maelekezo yaliyotolewa na Waziri yanatekelezwa kikamilifu

Awali akizungumza kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo anayeshughulikia sekta ya uvuvi, Prof. Mohammed Sheikh, alisema sekta ya uvuvi inaendelea kuwa miongoni mwa sekta zenye mchango mkubwa katika maendeleo ya uchumi wa Taifa, huku Serikali ikiendelea kuwekeza katika miradi ya kimkakati ikiwemo Bandari ya Uvuvi ya Kilwa Masoko na kuimarisha Shirika la Uvuvi Tanzania (TAFICO) ili liwe chombo kikuu cha kuendesha uvuvi wa kibiashara nchini.

Kwa upande wake, Afisa Mtendaji Mkuu wa TAFICO, CPA Shaibu Matessa, alisema Shirika limeingia katika hatua mpya ya maendeleo ambapo linaendelea kutekeleza miradi mbalimbali ya kimkakati inayolenga kuifanya TAFICO kuwa taasisi ya kisasa ya kibiashara katika sekta ya uvuvi.

Uzinduzi wa Bodi ya Pili ya Wakurugenzi wa TAFICO unatarajiwa kuwa chachu ya kuimarisha usimamizi wa uwekezaji wa Serikali katika sekta ya uvuvi na kuhakikisha Shirika linafikia dhamira ya kuwa nguzo ya utekelezaji wa ajenda ya uchumi wa buluu kupitia uzalishaji, biashara na uendelezaji wa rasilimali za uvuvi kwa manufaa ya Taifa.

Sanjari na tukio hilo, Waziri Dkt. Bashiru amezindua maandalizi ya Kongamano la Kimataifa la Ukuzaji Viumbemaji Duniani (WA26T) na Ukuzaji Viumbemaji Afrika (AFRAQ26), ambapo Tanzania itakuwa mwenyeji wa Kongamano hilo litakalofanyika Desemba,2026 Jijini Dar es salaam.
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa (kulia), akimkabidhi nyaraka za Utendaji kazi Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya TAFICO Prof. Yunus Daud Mgaya, katika Hafla ya Uzinduzi wa Bodi hiyo iliyofanyika Julai 13, 2026, katika Ofisi za Makao Makuu ya TAFICO, Ras Mkwavi, Kigamboni jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Dkt. Bashiru Ally Kakurwa kizungumza wakati akizindua Bodi ya pili ya Wakurugenzi ya TAFICO, katika hafla ya uzinduzi iliyofanyika Julai 13, 2026, katika Ofisi za Makao Makuu ya TAFICO, Ras Mkwavi, Kigamboni jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya TAFICO Prof. Yunus Daud Mgaya akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi wa Bodi mpya ya pili ya Shirika la Uvuvi Tanzania (TAFICO) uliyofanyika, katika Ofisi za Makao Makuu ya TAFICO, Ras Mkwavi, Kigamboni jijini Dar es Salaam.
Afisa Mtendaji Mkuu wa Shirika la Uvuvi Tanzania (TAFICO) CPA Shaibu Matessa, akizungumza wakati wa uzinduzi wa Bodi ya pili ya Wakurugenzi ya TAFICO, katika hafla ya uzinduzi iliyofanyika Julai 13, 2026, katika Ofisi za Makao Makuu ya TAFICO, Ras Mkwavi, Kigamboni jijini Dar es Salaam.
Mkutano ukiendelea
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa (walioketi katikati), akiwa kwenye picha ya pamoja na wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi ya TAFICO, katika Hafla ya Uzinduzi wa Bodi hiyo iliyofanyika Julai 13, 2026, katika Ofisi za Makao Makuu ya TAFICO, Ras Mkwavi, Kigamboni jijini Dar es Salaam.

MKURUGENZI MTENDAJI WA NBAA ATEMBELEA MAONESHO YA SABASABA

MKURUGENZI MTENDAJI WA NBAA ATEMBELEA MAONESHO YA SABASABA

Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA), CPA Prof. Siasa Issa Mzenzi akizungumza na watumishi wa NBAA alipotembelea banda la Bodi hiyo katika jengo la Wizara ya Fedha katika Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA), CPA Prof. Siasa Issa Mzenzi akiwa kwenye picha ya pamoja na watumishi wa  NBAA alipotembelea banda la Bodi hiyo katika jengo la Wizara ya Fedha katika Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA), CPA Prof. Siasa Issa Mzenzi akisalimiana na Afisa Habari Mwandamizi wa Wizara ya Fedha, Bw. Ramadhan Kissimba alipowasili  katika Banda la NBAA katika jengo la Wizara ya Fedha katika Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA), CPA Prof. Siasa Issa Mzenzi akizungumza na watumishi wa  Wizara ya Fedha alipotembelea banda hilo katika  jengo la Wizara ya Fedha katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara.
Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA), CPA Prof. Siasa Issa Mzenzi akisaini kitabu cha wageni alipotembelea banda la Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA)  ndani ya jengo la Wizara ya Fedha katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara.
Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA), CPA Prof. Siasa Issa Mzenzi akipata maelezo kutoka kwa Mkuu wa Kitengo cha Ushirikiano wa Kimataifa, Uhusiano na Masoko wa IAA, Sarah Goroi kuhusu kazi mbalimbali zinazofanywa na  IAA alipotembelea banda la Chuo cha Uhasibu Arusha (IAA) katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Sabasaba yanayoendelea katika Viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere, Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA), CPA Prof. Siasa Issa Mzenzi akisaini kitabu cha wageni alipotembelea banda la Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM) ndani ya jengo la Wizara ya Fedha katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara.
Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA), CPA Prof. Siasa Issa Mzenzi akipokea zawadi alipotembelea Banda la SELF Microfinance Fund katika Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA), CPA Prof. Siasa Issa Mzenzi akupata maelezo kutoka kwa Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano na Masoko cha TIA, Bi. Lilian Rugaitika alipotembelea banda la Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA)  ndani ya jengo la Wizara ya Fedha katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara.
Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA), CPA Prof. Siasa Issa Mzenzi akisaini kitabu cha wageni alipotembelea banda la Chuo cha Mipango ndani ya jengo la Wizara ya Fedha katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara.
Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA), CPA Prof. Siasa Issa Mzenzi akupata maelezo kutoka kwa Afisa Uhusiano na Elimu kwa Umma wa CMSA, Stella Anastazi alipotembelea banda la Mamlaka ya Masoko ya Mitaji na Dhamana (CMSA) lililopo ndani ya jengo la Wizara ya Fedha katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara.
Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA), CPA Prof. Siasa Issa Mzenzi (kushoto) akupata maelezo kutoka kwa  Mkuu wa Masoko na Mauzo wa APC Michael Mwakifuna(kulia) alipotembelea banda la "APC Hotel and Conference "
Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA), CPA Prof. Siasa Issa Mzenzi akiwa kwenye picha ya pamoja na watumisho wa "APC Hotel and Conference " 

Ecobank Tanzania Yatoa Elimu ya Huduma za Kifedha Maonesho ya Sabasaba


Ecobank Tanzania imeendelea kutoa elimu kwa wananchi kuhusu huduma mbalimbali za kifedha kupitia ushiriki wake katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Sabasaba yanayoendelea katika Viwanja vya Julius Nyerere, Dar es Salaam, ambapo banda lake linapatikana katika Kijiji cha Bima kinachosimamiwa na Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania (TIRA).

Akizungumza katika maonesho hayo, mwakilishi wa Ecobank amesema benki hiyo inatoa huduma mbalimbali za kifedha zinazolenga kukidhi mahitaji ya watu binafsi, wafanyabiashara na taasisi, huku ikiwapa wateja suluhisho la huduma za benki kwa urahisi na ufanisi.

Ameeleza kuwa miongoni mwa huduma zinazotolewa ni "Saving Account", ambayo haina makato ya kila mwezi na humruhusu mteja kuweka na kutoa fedha wakati wowote kulingana na mahitaji yake.

Aidha, amesema Ecobank inatoa "Current Account", inayomwezesha mteja kupata huduma ya "Overdraft", inayomruhusu kutumia fedha zinazozidi salio lililopo kwenye akaunti kwa muda wa hadi siku 14, kwa kuzingatia masharti ya benki.

Vilevile, benki hiyo inatoa mikopo ya muda mfupi na muda mrefu kwa makundi mbalimbali yakiwemo watumishi wa umma, wafanyabiashara na watu binafsi, pamoja na mikopo ya ujenzi na ununuzi wa nyumba.

Mbali na huduma za benki, Ecobank pia inatoa huduma mbalimbali za bima zikiwemo bima ya nyumba, magari na afya, kwa kushirikiana na wadau wake wa sekta ya bima, ikiwa ni sehemu ya kuwapatia wateja huduma za kifedha zilizounganishwa katika eneo moja.

Ecobank imewahimiza wananchi wanaotembelea Maonesho ya Sabasaba kutembelea banda lake lililopo Kijiji cha Bima (TIRA) ili kupata elimu zaidi kuhusu huduma za benki na bima, kufungua akaunti, kupata ushauri wa kifedha na kufahamu fursa mbalimbali zinazotolewa na benki hiyo.
Mkuu wa kitengo cha Wateja Binafsi na Biashara kutoka Ecobank Tanzania, Joyce Ndyetabura akimsikiliza mfanyakazi wa Ecobank Tanzania walipokuwa wanatoa huduma katika maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Sabasaba yanayoendelea jijini Dar es Salaam ambapo banda lake linapatikana katika Kijiji cha Bima kinachosimamiwa na Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania (TIRA).
Watumishi wa Ecobank Tanzania wakitoa elimu katika maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Sabasaba yanayoendelea jijini Dar es Salaam.

Mkuu wa Kitengo cha Biashara kwa Wateja Wakubwa (Commercial Banking) Joyce Ndyetabura akiwa kwenye picha ya pamamo na watumishi wa Ecobank Tanzania katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Sabasaba yanayoendelea katika Viwanja vya Julius Nyerere, Dar es Salaam, ambapo banda lake linapatikana katika Kijiji cha Bima kinachosimamiwa na Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania (TIRA).

VIONGOZI MBALIMBALI WATEMBELEA BANDA LA NBAA MAONESHO YA SABASABA


Waziri wa Fedha Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb) (kushoto), akisikiliza maelezo kutoka kwa mfanyakazi wa NBAA alipotembelea banda la Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA) lililopo katika jengo la Wizara ya Fedha katika Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba), yenye Kaulimbiu ya "Maonesho ya Biashara ya Kimataifa Sabasaba ni Fahari ya Tanzania.
Waziri wa Fedha Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb) (kushoto) akipokea zawadi alipotembelea banda la Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA) lililopo katika jengo la Wizara ya Fedha katika Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba)
Spika wa Bunge Mstaafu, Bi. Anne Makinda (kushoto) akisaini kitabu alipotembelea banda la NBAA lililopo katika jengo la Wizara ya Fedha katika Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba)
Spika wa Bunge Mstaafu, Bi. Anne Makinda (kushoto) akizungumza na watumishi wa Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA) alipotembelea banda la Bodi hiyo lililopo katika jengo la Wizara ya Fedha katika Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba)
Naibu Waziri wa Fedha Mhe. Laurent Deogratius Luswetula (kushoto) akizungumza na Mwenyekiti wa Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA), CPA. Profesa Sylvia Temu (kulia) alipotembelea banda la Bodi hiyo hiyo lililopo katika jengo la Wizara ya Fedha katika Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba)
Mwenyekiti wa Baraza la Uongozi wa Chuo, CPA Dkt. Mwamini Tulli akisikiliza maelezo kutoka kwa mfanyakazi wa NBAA alipotembelea banda la Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA) lililopo katika jengo la Wizara ya Fedha katika Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba)
Mwenyekiti wa Baraza la Uongozi wa Chuo, CPA Dkt. Mwamini Tulli akisaini kitabu alipotembelea banda la NBAA lililopo katika jengo la Wizara ya Fedha katika Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba)
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma (PPRA), Bw. Dennis Simba akisaini kitabu alipotembelea banda la NBAA lililopo katika jengo la Wizara ya Fedha katika Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba)
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma (PPRA), Bw. Dennis Simba akiwa kwenye picha ya pamoja na watumishi wa NBAA alipotembele banda la Bodi hiyo lililopo katika jengo la Wizara ya Fedha katika Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba).
Maonesho yakiendelea katika banda la NBAA
Mkurugenzi wa Huduma za Shirika katika Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA) CPA Kulwa Emmanuel Malendeja akiwa kwenye picha ya pamoja na watumishi wa Bodi hiyo kwenye Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba).

RAIS WA MSUMBIJI AWASILI NCHINI KWA ZIARA YA KIKAZI YA SIKU TATU



Rais wa Jamhuri ya Msumbiji Mheshimiwa Daniel Francisco Chapo amewasili nchini kuanza ziara ya kikazi ya siku tatu, kuanzia Julai 2 -4 , 2026.

Katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam Mheshimiwa Rais Daniel Francisco Chapo alipokelewa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Dkt. Mahmoud Thabit Kombo (Mb) ambaye aliambatana na viongozi wengine waandamizi wa Serikali.

Akiwa nchini, Mheshimiwa Rais Chapo atafanya mazungumzo rasmi na mwenyeji wake Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Ikulu, jijini Dar es Salaam.

Aidha, Mheshimiwa Rais Chapo atafungua rasmi Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam; atamtembelea Mama Maria Nyerere kwa lengo la kumsalimia na ataweka jiwe la msingi la ujenzi wa Ubalozi wa Msumbiji jijini Dar es Salaam.

Itakumbukwa kuwa, ziara hii ni ya tatu kwa Mheshimiwa Chapo kufanyika hapa nchini tangu alipoingia madarakani mwaka 2024 jambo lililoakisi dhamira ya viongozi wa nchi hizi mbili ya kuendelea kuimarisha mahusiano ya kirafiki na ushirikiano wa uhusiano wa kindugu kati ya Tanzania na inatarajiwa kufungua fursa mpya za ushirikiano wa karibu yaliyojengwa juu ya historia ya ujirani mwema na mshikamano wa muda mrefu.