HABARI

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

MATUKIO

MICHEZO

SIASA

MAHAFALI YA 48 YA BODI YA NBAA YAFANA


Wahitimu wa Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu (NBAA) wakiwa kwenye maadamano ya kitaaluma wakati wa mahafali ya 48 ya Bodi hiyo yaliyofanyika katika hoteli ya APC Bunju, Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA), CPA. Prof. Sylvia S. Temu akipokea maadamano ya kitaaluma pamoja na viongozi wa Bodi pamoja na wajumbe wa Bodi hiyo wakati wa mahafali ya 48 ya Bodi hiyo.

Mwenyekiti wa Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA), CPA. Prof. Sylvia S. Temu akizungumza kuhusu namna Bodi hiyo ilivyofanikisha kuongeza idadi ya wahitimu kwa mwaka huu wakati wa mahafali ya 48 ya NBAA.

Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA), CPA Pius A. Maneno akisoma hotuba yake kuhusu mafanikio yaliyopatikana kwenye kipindi chake cha uongoziwake wakati wa mahafali ya 48 ya Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA).
Baadhi ya Wahitimu pamoja na wageni waalikwa wakifuatilia hotuba ya mgeni rasmi Mwenyekiti wa Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA), CPA. Prof. Sylvia S. Temu  kwenye mahafali ya 48 ya Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA).
Wahitimu wa ngazi ya CPA wakisoma viapo vyao wakati wa mahafali ya 48 ya Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA).
Mwenyekiti wa Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA), CPA. Prof. Sylvia S. Temu akiwatunuku wahitimu kwenye mahafali ya 48 ya Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA).
Wahitimu wakishangilia mara baada ya kutunukiwa CPA wakati wa mahafali ya 48 ya Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA)
Mwenyekiti wa Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA), CPA. Prof. Sylvia S. Temu akitoa vyeti kwa wahitimu waliofanya vizuri kwenye mitihani ya Bodi wakati wa mahafali ya 48.
Mwenyekiti wa Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA), CPA. Prof. Sylvia S. Temu akiwa kwenye picha ya pamoja na baadhi ya wafanyakazi wa Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu (NBAA) wakati wa mahafali ya 48 ya Bodi hiyo.

Ecobank Group Yaweka Rekodi ya Ongezeko la Mikopo kwa Biashara za Wanawake Afrika




Ecobank Group imetangaza ukuaji mkubwa wa mikopo, likilenga kuimarisha ujasiriamali wa wanawake barani Afrika. Ecobank imerekodi ongezeko kubwa la asilimia 194 katika utoaji wa mikopo kwa biashara zinazoongozwa na wanawake, likifikia dola za Marekani milioni 780 mwaka 2025 kutoka dola milioni 265 mwaka 2024. Hatua hii inaashiria mafanikio ya juhudi za benki hiyo katika kukuza usawa wa kijinsia na kuimarisha uchumi wa ndani barani Afrika.

Taarifa hiyo ilitolewa wakati wa uzinduzi wa Ripoti ya Programu ya Jinsia ya Ecobank, ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya International Women’s Day 2026.

Wataalamu wa uchumi wanaeleza kuwa wanawake wajasiriamali wana mchango mkubwa katika kukuza ajira, kusaidia familia na kuimarisha minyororo ya thamani ya ndani. Hata hivyo, biashara nyingi zinazoongozwa na wanawake bado zinakabiliwa na changamoto ya upatikanaji wa mitaji, huku pengo la ufadhili likikadiriwa kufikia dola bilioni 42 barani Afrika.

Ili kukabiliana na changamoto hiyo, Ecobank imeendelea kuwekeza katika mipango maalum inayolenga wanawake kwa kutoa mikopo rafiki, mafunzo ya biashara, ushauri na fursa za kuunganishwa na masoko ya kikanda. Lengo ni kuwasaidia wanawake kukuza biashara endelevu na zenye ushindani.

Moja ya mipango hiyo ni programu ya Ellevate, iliyoanzishwa mwaka 2020 kusaidia biashara za wanawake zilizoathiriwa na janga la COVID-19. Programu hiyo sasa imekua na kuwa moja ya miradi mikubwa zaidi barani Afrika, ikihudumia zaidi ya wanawake wajasiriamali 103,000 katika nchi 26. Zaidi ya wanawake 21,000 wamejiunga na mpango huo mwaka 2025 pekee, huku zaidi ya 24,000 wakinufaika na mafunzo na ushauri wa kibiashara.

Aidha, Ecobank imezindua programu ya MAMA inayolenga kuwasaidia wanawake wanaofanya biashara katika sekta isiyo rasmi, kwa kuwapatia mikopo nafuu na kuwasaidia kuingia katika mfumo rasmi wa kifedha. Mpango huo tayari umewafikia zaidi ya wanawake 10,000, huku zaidi ya 2,000 wakipata mikopo yenye thamani ya zaidi ya dola milioni 1.8.

Katika juhudi za kuongeza upatikanaji wa mtaji, Ecobank pia ilizindua hati fungani maalum ya jinsia nchini Côte d’Ivoire mwaka 2025, iliyokusanya zaidi ya faranga za CFA bilioni 11 ndani ya saa 48. Fedha hizo zinatarajiwa kusaidia kutoa mikopo kwa zaidi ya biashara 1,200 ndogo na za kati zinazomilikiwa na wanawake.

Akizungumza kuhusu mafanikio hayo, Mkurugenzi Mtendaji Mkuu wa Kundi la Ecobank, Jeremy Awori alisema wanawake wajasiriamali ni mhimili muhimu wa ukuaji wa uchumi wa Afrika, lakini bado wanakumbana na changamoto za upatikanaji wa fedha.

“Ecobank inaendelea kushughulikia changamoto hiyo kwa kuunganisha mitaji, ujuzi na fursa za masoko kupitia mtandao wake wa bara zima. Ongezeko hili linaonyesha wazi mahitaji makubwa ya huduma hizi na mafanikio ya programu zetu,” alisema.

Kwa siku zijazo, Ecobank inapanga kupanua zaidi programu ya Ellevate katika masoko yote inayofanya kazi, kuimarisha huduma zisizo za kifedha kama zana za kidijitali, pamoja na kuanzisha bidhaa mpya zitakazolenga wanawake ili kuongeza ushiriki wao katika uchumi wa Afrika.

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu Yakagua Maendeleo ya Ujenzi wa Chuo cha Usafiri wa Anga (CATC)

 


Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) imetembelewa na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu kwa lengo la kukagua eneo la mradi wa ujenzi na kujionea maendeleo ya ujenzi wa Majengo ya Kisasa ya Chuo cha Usafiri wa Anga (CATC) yaliyopo Banana–Ukonga, jijini Dar es Salaam.

Ziara hiyo ya kikazi iliongozwa na Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, Mhe. Selemani Kakoso, ambapo wajumbe wa Kamati walipata fursa ya kukagua hatua mbalimbali za utekelezaji wa mradi na kujionea hali ya maendeleo ya ujenzi unaoendelea.

Katika ziara hiyo, Kamati ilipongeza jitihada za TCAA katika kusimamia utekelezaji wa mradi huo na kuisisitiza Mamlaka kuendelea kumsimamia kikamilifu mkandarasi anayetekeleza ujenzi ili kuhakikisha mradi unakamilika kwa wakati na kwa kuzingatia viwango vilivyokubalika.

Kwa upande wake, Waziri wa Uchukuzi, Mhe. Prof. Makame Mbarawa, alisema kuwa Serikali ya Awamu ya Sita inaendelea kuwekeza katika sekta ya usafiri wa anga kupitia ujenzi, ukarabati na upanuzi wa miundombinu ya anga pamoja na kuimarisha mifumo ya usimamizi, akibainisha kuwa rasilimali watu yenye ujuzi wa hali ya juu ni msingi wa ukuaji na usalama wa sekta hiyo.

Akizungumza kwa niaba ya TCAA, Mkurugenzi Mkuu wa TCAA, Salim Msangi alibainisha kuwa CATC ina upekee wa kimkakati kwa kuwa ni miongoni mwa vyuo tisa barani Afrika vinavyotambuliwa katika kutoa mafunzo ya usalama wa usafiri wa anga, hali inayoliweka Taifa katika nafasi muhimu ya kikanda na kimataifa katika ukuzaji wa utaalamu wa anga.

“Mradi huu unaimarisha nafasi ya CATC kama kitovu cha ubora wa mafunzo ya usalama wa anga barani Afrika na ni uwekezaji wa moja kwa moja katika usalama na maendeleo endelevu ya sekta ya usafiri wa anga nchini,” alisema.
Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu wakitembelea na kukagua maendeleo ya ujenzi wa mradi wa ujenzi wa Chuo cha Usafiri wa Anga (CATC) unaendelea katika eneo la Banana, jijini Dar es Salaam.
 Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu ikiongozwa na Mwenyekiti wake, Selemani Kakoso na Menejimenti ya TCAA ikiongozwa na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA), Bw. Salim Msangi wakisiliza maelezo kuhusu ujenzi wa mradi wa Chuo cha Usafiri wa Anga (CATC) yaliyokuwa yanatolewa na Meneja mradi wa Chuo cha CATC, Mhandisi Stephen Mwakasasa.
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, Selemani Kakoso akizungumza mara baada ya kutembelea na kukagua maendeleo ya ujenzi wa mradi wa ujenzi wa Chuo cha Usafiri wa Anga (CATC) unaendelea katika eneo la Banana, jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Uchukuzi Mhe. Prof. Makame Mbarawa akizumgumza kuhusu namna wizara inavyosimamia mradi wa Ujenzi wa Chuo cha Usafiri wa Anga (CATC) kinachojengwa katika eneo la Banana, jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) Salim Msangi akizungumza kuhusu maendelea ya mradi wa Ujenzi wa Chuo cha Usafiri wa Anga (CATC) kinachojengwa katika eneo la Banana, jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu pamoja na watumishi wa TCAA wakiwa kwenye kikao mara baada ya kamati hiyo kutembelea na kukagua maendeleo ya ujenzi wa mradi wa ujenzi wa Chuo cha Usafiri wa Anga (CATC) unaendelea katika eneo la Banana, jijini Dar es Salaam.
Ujenzi ukiendelea