Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA), Septemba 8, 2026, imeendesha Warsha ya Mafunzo kuhusu Uandaaji wa Hesabu kwa kuzingatia Viwango vya Kimataifa vya Uhasibu kwa Sekta ya Umma (IPSAS), mkoani Morogoro.
Akizungumza wakati wa ufunguzi wa warsha hiyo, Mkurugenzi Mtendaji wa NBAA, CPA Prof. Siasa I. Mzenzi, amesema Tanzania imepiga hatua kubwa katika utekelezaji wa IPSAS, hatua ambayo imeiwezesha nchi kujenga uwezo na kupata uzoefu unaoweza kuwa mfano kwa mataifa mengine.
CPA Prof. Siasa amesema Tanzania kwa sasa imevuka hatua ya msingi ya kujenga uwezo katika eneo la IPSAS, tofauti na baadhi ya nchi ambazo bado zinaendelea kutafuta namna ya kuimarisha uwezo wa wataalamu wao katika utekelezaji wa viwango hivyo. Amesema mafanikio hayo yameifanya Tanzania kuwa na nafasi ya kushirikisha uzoefu wake na nchi nyingine.
“Tumefanikiwa sana kwenye IPSAS, mkazo huo kwa sasa tunauelekeza pia kwenye Sustainability Reporting na tayari tumeshatoa Technical Pronouncement No. 1 ya mwaka 2024 ambayo inazitaka taasisi kuanza kutoa taarifa za Sustainability.
CPA Prof. Siasa amesisitiza umuhimu wa Taasisi za Umma kutumia mafanikio yaliyopatikana katika utekelezaji wa IPSAS kama msingi wa kuimarisha utoaji wa taarifa za uendelevu, akieleza kuwa maeneo hayo yanapaswa kwenda sambamba katika kukuza uwazi, uwajibikaji na uendelevu wa taasisi za umma.
Katika hatua nyingine, amewahamasisha washiriki wa warsha hiyo kuweka kipaumbele katika uandaaji na uwasilishaji bora wa vitabu vya hesabu kwa ajili ya "Best Presented Financial Statements Awards", akieleza kuwa idadi ya washindi itaongezwa kutoka watatu hadi watano.
Warsha hii ya IPSAS inalenga kuwawezesha washiriki kuongeza uelewa na ujuzi kuhusu matumizi sahihi ya IPSAS katika uandaaji wa taarifa za fedha za sekta ya umma, pamoja na kuimarisha weledi wa wataalamu katika eneo la Uhasibu na Ukaguzi wa hesabu.
Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA) CPA Prof. Siasa I. Mzenzi akizungumza wakati wa ufunguzi wa warsha ya Mafunzo kuhusu Uandaaji wa Hesabu kwa kuzingatia Viwango vya Kimataifa vya Uhasibu kwa Sekta ya Umma (IPSAS), mkoani Morogoro.
Mkurugenzi wa Huduma za Viwango vya Kiuhasibu, Utafiti na Huduma za Ufundi wa NBAA, Angyelile Tende akizungumza kwenye warsha ya Mafunzo kuhusu Uandaaji wa Hesabu kwa kuzingatia Viwango vya Kimataifa vya Uhasibu kwa Sekta ya Umma (IPSAS), mkoani Morogoro.
Baadhi ya washiriki pamoja na watumishi wa NBAA wakifuatlia ufunguzi wa warsha ya Mafunzo kuhusu Uandaaji wa Hesabu kwa kuzingatia Viwango vya Kimataifa vya Uhasibu kwa Sekta ya Umma (IPSAS), mkoani Morogoro.
Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA) CPA Prof. Siasa I. Mzenzi katikati waliokaa) akiwa kwenye picha ya pamoja na baadhi ya washiriki pamoja na watumishi wa NBAA kwenye warsha ya Mafunzo kuhusu Uandaaji wa Hesabu kwa kuzingatia Viwango vya Kimataifa vya Uhasibu kwa Sekta ya Umma (IPSAS)


















.jpeg)

.jpeg)

.jpeg)


























