HABARI

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

MATUKIO

MICHEZO

SIASA

Rais Samia ashiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali kuhusu Uvumbuzi wa Nishati ya Nyuklia barani Afrika (NEISA), Kigali nchini Rwanda


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza katika Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali kuhusu Uvumbuzi wa Nishati ya Nyuklia barani Afrika (NEISA), Kigali nchini Rwanda tarehe 19 Mei, 2026. Mkutano huo wa Kimataifa unawakutanisha pia wataalamu wa nishati, wawekezaji na mashirika ya kimataifa, ambapo utajadili matumizi ya nishati ya nyuklia kwa maendeleo ya Bara la Afrika. Mkutano huo pia unalenga kujadili namna bora ya kuongeza upatikanaji wa nishati ya umeme Afrika, kupunguza uchafuzi wa mazingira, kusaidia maendeleo ya viwanda, kukuza ubunifu wa teknolojia za nishati ya nyuklia pamoja na kuvutia wawekezaji katika miradi ya nishati tarehe, 19 Mei, 2026.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha ya pamoja na Viongozi mbalimbali walioshiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali kuhusu Uvumbuzi wa Nishati ya Nyuklia barani Afrika (NEISA), Kigali nchini Rwanda tarehe 19 Mei, 2026. Mkutano huo wa Kimataifa unawakutanisha pia wataalamu wa nishati, wawekezaji na mashirika ya kimataifa, ambapo utajadili matumizi ya nishati ya nyuklia kwa maendeleo ya Bara la Afrika. Mkutano huo pia unalenga kujadili namna bora ya kuongeza upatikanaji wa nishati ya umeme Afrika, kupunguza uchafuzi wa mazingira, kusaidia maendeleo ya viwanda, kukuza ubunifu wa teknolojia za nishati ya nyuklia pamoja na kuvutia wawekezaji katika miradi ya nishati, tarehe 19 Mei, 2026.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akitembelea maonyesho wakati wa Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali kuhusu Uvumbuzi wa Nishati ya Nyuklia barani Afrika (NEISA), Kigali nchini Rwanda tarehe 19 Mei, 2026. Mkutano huo wa Kimataifa unawakutanisha pia wataalamu wa nishati, wawekezaji na mashirika ya kimataifa, ambapo utajadili matumizi ya nishati ya nyuklia kwa maendeleo ya Bara la Afrika. Mkutano huo pia unalenga kujadili namna bora ya kuongeza upatikanaji wa nishati ya umeme Afrika, kupunguza uchafuzi wa mazingira, kusaidia maendeleo ya viwanda, kukuza ubunifu wa teknolojia za nishati ya nyuklia pamoja na kuvutia wawekezaji katika miradi ya nishati, tarehe 19 Mei, 2026.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan pamoja na Viongozi mbalimbali wakishiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali kuhusu Uvumbuzi wa Nishati ya Nyuklia barani Afrika (NEISA), Kigali nchini Rwanda tarehe 19 Mei, 2026. Mkutano huo wa Kimataifa unawakutanisha pia wataalamu wa nishati, wawekezaji na mashirika ya kimataifa, ambapo utajadili matumizi ya nishati ya nyuklia kwa maendeleo ya Bara la Afrika. Mkutano huo pia unalenga kujadili namna bora ya kuongeza upatikanaji wa nishati ya umeme Afrika, kupunguza uchafuzi wa mazingira, kusaidia maendeleo ya viwanda, kukuza ubunifu wa teknolojia za nishati ya nyuklia pamoja na kuvutia wawekezaji katika miradi ya nishati.

Rais Dkt. Samia Aelekea Rwanda Kushiriki Mkutano wa Nishati ya Nyuklia Afrika




Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiagana na viongozi mbalimbali kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) Jijini Dar es Salaam kabla ya kuondoka nchini, kuelekea Kigali, Rwanda kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali kuhusu Uvumbuzi wa Nishati ya Nyuklia barani Afrika (NEISA) tarehe 19 Mei, 2026. Mkutano huo wa Kimataifa unawakutanisha pia wataalamu wa nishati, wawekezaji na mashirika ya kimataifa, ambapo utajadili matumizi ya nishati ya nyuklia kwa maendeleo ya Bara la Afrika. Mkutano huo pia unalenga kujadili namna bora ya kuongeza upatikanaji wa nishati ya umeme Afrika, kupunguza uchafuzi wa mazingira, kusaidia maendeleo ya viwanda, kukuza ubunifu wa teknolojia za nishati ya nyuklia pamoja na kuvutia wawekezaji katika miradi ya nishati.

Baraza la Mawaziri la EAC kukutana kwa Dharura jijini Arusha


Maandalizi ya Mkutano wa 60 wa Dharura wa Baraza la Mawaziri la Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), unaotarajiwa kufanyika tarehe 22 Mei 2026, yameanza rasmi kupitia vikao vya ngazi ya wataalamu vinavyoendelea kuanzia tarehe 18 hadi 20 Mei 2026 katika Makao Makuu ya Jumuiya hiyo jijini Arusha.

Kikao hicho cha wataalamu kimepokea na kujadilia taarifa ya Kamati ya Fedha na Utawala kuhusu masuala ya fedha ya Jumuiya, na rasimu ya bajeti ya Sekretarieti ya EAC pamoja na taasisi zake kwa mwaka wa fedha 2026/2027. Mapendekezo yatakayopitishwa katika ngazi hiyo yatawasilishwa kwa Makatibu Wakuu watakaokutana tarehe 21 Mei, 2026 kabla ya kuwasilishwa katika Mkutano wa Baraza la Mawaziri utakaofanyika tarehe 22 Mei, 2026.

Vilevile, mkutano huo wa siku tano kuanzia tarehe 18 hadi 22 Mei, 2026 unalenga kuweka mikakati ya pamoja ya utekelezaji wa maelekezo na maamuzi yaliyotolewa na Mkutano wa 25 wa Wakuu wa Nchi za EAC, hususan katika maeneo ya mipango na fedha

Baraza la Mawaziri la EAC ni chombo kikuu cha maamuzi na kusimamia shughuli za Jumuiya, katika hatua hii ya maandalizi ya bajeti, Baraza hilo lina jukumu la kupokea, kuchambua, kufanya marekebisho na kuidhinisha makadirio ya mapato na matumizi ya Sekretarieti ya EAC kabla ya kuwasilishwa katika Bunge la Afrika Mashariki (EALA) kwa ajili ya kujadiliwa na kupitishwa rasmi.

Ujumbe wa Tanzania katika mkutano huo unajumuisha wajumbe kutoka Wizara ya Fedha, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora pamoja na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, ukionaongozwa na Mkurugenzi wa Sera na Mipango kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Justin Kisoka.






Rais Samia Akutana na Mkurugenzi wa Miradi Benki ya Dunia Afrika


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye mazungumzo na aliyekuwa Mkurugenzi Mkazi wa Benki ya Dunia anayesimamia nchi za Malawi, Tanzania, Zambia na Zimbabwe, Bw. Nathan Belete, Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 18 Mei, 2026. Bw. Belete ambaye kwa sasa ni Mkurugenzi wa Miradi wa Benki ya Dunia Kanda ya Afrika, alifika Ikulu kwa ajili ya kumuaga Mhe. Rais Dkt. Samia mara baada ya kuhudumu katika nafasi yake ya awali kwa kipindi cha miaka minne. Pia aliambatana na mrithi wake Mkurugenzi Mkazi wa Benki hiyo anayesimamia nchi za Malawi, Tanzania, Zambia na Zimbabwe Bw. Firas Raad.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na aliyekuwa Mkurugenzi Mkazi wa Benki ya Dunia anayesimamia nchi za Malawi, Tanzania, Zambia na Zimbabwe, Bw. Nathan Belete ambaye kwa sasa ni Mkurugenzi wa Miradi ya Benki hiyo, Kanda ya Afrika, Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 18 Mei, 2026.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na aliyekuwa Mkurugenzi Mkazi wa Benki ya Dunia anayesimamia nchi za Malawi, Tanzania, Zambia na Zimbabwe, Bw. Nathan Belete ambaye kwa sasa ni Mkurugenzi wa Miradi wa Benki hiyo, Kanda ya Afrika, pamoja na Mkurugenzi Mkazi wa Benki ya Dunia anayesimamia nchi za Malawi, Tanzania, Zambia na Zimbabwe Bw. Firas Raad mara baada ya mazungumzo yao, Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 18 Mei, 2026.

NBAA Yatoa Mafunzo kwa Watumishi wa NAOT


Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA) imetoa mafunzo maalumu kwa watumishi 101 wa Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi (NAOT) kwa lengo la kuimarisha ujuzi wa kitaaluma, kuongeza ufanisi katika utendaji kazi pamoja na kuendana na mabadiliko ya kimataifa katika Taaluma ya Uhasibu na Ukaguzi.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo, Mkurugenzi Mtendaji wa NBAA, CPA Prof. Siasa Issa Mzenzi ameishukuru NAOT kwa kuendelea kushirikiana na NBAA katika kuwawezesha Wahasibu na Wakaguzi kupitia mafunzo mbalimbali ya kitaaluma, hususan mafunzo maalumu yaliyoandaliwa kwa watumishi wa ofisi hiyo.

Prof. Mzenzi amesema tangu alipoanza rasmi majukumu yake tarehe 30 Machi mwaka huu, amepokea salamu nyingi za pongezi kutoka kwa wadau mbalimbali wa Taaluma ya Uhasibu na Ukaguzi, jambo ambalo limempa hamasa ya kuendelea kuisukuma mbele Taaluma hiyo kupitia kaulimbiu ya “Moving the Profession Forward”.

Aidha, amempongeza aliyekuwa Mkurugenzi Mtendaji wa NBAA, CPA Pius A. Maneno, kwa mchango wake mkubwa wa zaidi ya miaka 20 katika kuimarisha Taaluma ya Uhasibu na Ukaguzi nchini. Amesema mafanikio mengi yanayoonekana leo katika Taaluma hiyo yametokana na uongozi na juhudi zake katika kipindi chote cha utumishi wake.

Katika hatua nyingine, Prof. Mzenzi amesisitiza umuhimu wa kuendelea kuimarisha ushirikiano kati ya NBAA na NAOT katika maeneo mbalimbali ikiwemo mafunzo, utawala bora pamoja na matumizi ya Viwango vya Kimataifa vya Uhasibu wa Sekta ya Umma (IPSAS).

Amesema Tanzania imeendelea kuwa mfano bora barani Afrika katika utekelezaji wa viwango vya IPSAS, huku nchi nyingi za Afrika zikiiangalia Tanzania kama kitovu cha kujifunza uzoefu na mafanikio katika utekelezaji wa viwango hivyo. Ameeleza kuwa mafanikio hayo yametokana na juhudi kubwa zinazofanywa na NAOT katika kuhakikisha Taasisi za umma zinaandaa taarifa za fedha zinazokidhi viwango vya kimataifa.

Sambamba na hilo, amewataka Wahasibu na Wakaguzi kujiandaa na mabadiliko mapya ya Taaluma, hususan katika eneo la Sustainability Reporting, akisema kuwa mfumo huo sasa ni sehemu muhimu ya taarifa za kifedha duniani. Ameongeza kuwa Serikali kupitia Wizara ya Fedha tayari imeanza kutoa mwongozo na ramani ya utekelezaji wa mfumo huo nchini.

Naye mwakilishi wa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Charles E. Kichere, amesema faida kubwa ya mafunzo hayo ni ushirikiano uliopo kati ya NBAA na NAOT katika kuandaa muundo wa mafunzo unaoendana na hali halisi pamoja na changamoto zinazojitokeza katika utekelezaji wa majukumu ya Ukaguzi wa hesabu za Serikali.

“Tumekuwa na muundo maalumu wa ratiba ya mafunzo haya ili kuhakikisha yanakuwa yenye tija na yanakidhi mahitaji halisi ya washiriki. Kabla ya kuanza rasmi kwa mafunzo, tulipata fursa ya kushirikiana kwa karibu katika kuandaa mada mbalimbali, jambo lililowezesha kuwepo kwa majadiliano yanayoakisi mazingira halisi ya kazi pamoja na changamoto zinazokabili Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Serikali,” amesema.

Aidha, amesema ushirikiano huo umewezesha NBAA kutoa nafasi kwa wakufunzi wa ndani pamoja na wakufunzi kutoka NAOT kushiriki katika kuendesha mafunzo hayo, hatua ambayo imeongeza ubora wa mafunzo na kuimarisha ushirikiano wa kitaaluma kati ya Taasisi hizo mbili.

Vilevile, amewapongeza watumishi wa NAOT kwa ushiriki wao mzuri katika mafunzo hayo, akieleza kuwa ushiriki huo ni ishara ya dhamira ya kuendelea kujifunza na kuongeza ufanisi katika utendaji wa kazi.

Mafunzo hayo yanatarajiwa kuongeza ujuzi wa kitaaluma kwa washiriki na kuimarisha uwezo wao katika kutekeleza majukumu ya Ukaguzi na usimamizi wa fedha za umma kwa ufanisi zaidi.
Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA), CPA Prof. Siasa Issa Mzenzi akizungumza na watumishi wa Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi (NAOT) alipokuwa anafungua mafunzo ya siku mbili yaliyofanyika katika Ukumbi wa Hoteli ya APC, Bunju jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa Huduma za Utafiti, Viwango na Uhasibu wa NBAA, CPA Angyelile Tende akizungumza kuhusu namna wanavyoshirikiana na Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi (NAOT) katika utoaji wa Mafunzo kwa watumishi wao wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya Siku mbili yaliyofanyika katika Ukumbi wa Hoteli ya APC, Bunju jijini Dar es Salaam.

Mkufunzi wa Mafunzo hayo, CPA. Dkt. Neema Kiure Mssusa akiendelea kutoa mada kwa watumishi wa Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi (NAOT)
Watumishi wa Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi (NAOT) wakifuatilia hotuba ya mgeni rasmi Mkurugenzi Mtendaji wa NBAA, CPA Prof. Siasa Issa Mzenzi wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya Siku mbili kwa watumishi hao.
Mkurugenzi Mtendaji wa NBAA, CPA Prof. Siasa Issa Mzenzi akiwa kwenye picha ya pamoja na Watumishi wa Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi (NAOT), watoa mada pamoja na baadhi ya watumishi wa NBAA.

ECOBANK TANZANIA YADHAMINI TUZO ZA BMT 2025, WAZIRI MKUU APONGEZA MCHANGO WA SEKTA BINAFSI KUKUZA MICHEZO



Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba ameongoza zoezi la utoaji wa Tuzo za Baraza la Michezo la Taifa (BMT) zilizotolewa kwa wanamichezo na timu zilizofanya vizuri mwaka 2025, katika hafla iliyolenga kutambua mchango na mafanikio ya wadau wa michezo nchini.

Akizungumza katika hafla hiyo ambapo alikuwa mgeni rasmi, Dkt. Nchemba alitoa pongezi na shukrani za dhati kwa Ecobank Tanzania kwa mchango wake mkubwa wa kudhamini hafla hiyo muhimu ya michezo nchini.

Dkt. Nchemba alisema ushirikiano kati ya Serikali na sekta binafsi unaendelea kuwa chachu ya maendeleo ya michezo nchini, huku akiipongeza Ecobank Tanzania kwa kuonyesha dhamira ya kweli katika kuunga mkono vipaji vya wanamichezo wa Tanzania. Alibainisha kuwa udhamini huo umeongeza hadhi ya Tuzo hizo na kutoa motisha kwa wanamichezo kuendelea kufanya vizuri katika mashindano ya kitaifa na kimataifa.

Aidha, Waziri Mkuu alisema katika kipindi kifupi yameshuhudiwa mafanikio makubwa katika sekta ya michezo, yakiwamo kuanzishwa kwa Mfuko wa Maendeleo ya Michezo unaopata asilimia tano ya mapato ya michezo ya kubashiri, hatua ambayo imewezesha timu na wanamichezo kushiriki mashindano mengi zaidi kwa ubora wa hali ya juu. Alisisitiza kuwa mchango wa wadau kama Ecobank Tanzania unaendelea kusaidia juhudi za Serikali katika kuinua sekta ya michezo na kuibua vipaji vya vijana nchini.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Ecobank Tanzania, Dkt. Charles Asiedu alisema benki hiyo inajivunia kuunga mkono juhudi za Serikali katika kutambua na kuinua vipaji vya michezo mbalimbali hapa nchini kupitia Tuzo za Baraza la Michezo la Taifa (BMT) tukio linaloadhimisha ubora, kujituma na mafanikio makubwa ya mashujaa wa michezo wa Tanzania.

Dkt. Asiedu alisema kupitia Tuzo hizo maalumu, Ecobank imedhamini kipengele cha Tuzo ya Mwamuzi Bora wa Kiume wa Mwaka, kinacholenga kutambua na kuhamasisha vipaji vinavyochipukia katika sekta ya michezo nchini. Alieleza kuwa benki hiyo itaendelea kushirikiana na wadau mbalimbali kuhakikisha vijana wenye vipaji wanapata motisha na mazingira bora ya kufikia mafanikio yao.

" Ecobank Group ni benki kubwa yenye mtandao mpana zaidi barani Afrika, ikiwa na uwepo katika nchi zaidi ya 33. Nchini Tanzania, Ecobank inatoa huduma mbalimbali za kibenki kwa wateja binafsi pamoja na wafanyabiashara wadogo, wa kati na wakubwa." Alisema Dkt. Asiedu

Benki hiyo imeendelea kuwakaribisha wananchi kutumia huduma zake kupitia matawi, mawakala pamoja na ATM zilizopo Dar es Salaam, Arusha na Mwanza ili kupata huduma bora na za kisasa za kibenki. Sambamba na hilo, Ecobank pia inatoa huduma za kibenki kiganjani kupitia Ecobank Mobile, ambapo wateja wanaweza kupata huduma mbalimbali ikiwamo kufungua akaunti, kulipia bili, kupata huduma ya salary advance kwa waajiriwa pamoja na mikopo kwa watumishi wa umma.

Kwa pamoja, Serikali na wadau wa sekta binafsi wanaendelea kuibua vipaji, kuhamasisha jamii na kuwezesha kizazi kijacho kupitia michezo.
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba akizungumza na viongozi pamoja na wageni  mbalimbali wakati wa utoaji wa Tuzo za BMT 2025 zililizofanyika katika ukumbi wa The Super Dome, Masaki jijini Dar es Salaam
Mkurugenzi Mtendaji wa Ecobank Tanzania, Dkt. Charles Asiedu akimtangaza mshindi Tuzo ya Mwamuzi Bora wa Kiume wa Mwaka katika Tuzo za BMT 2025 zilizotolewa katika ukumbi wa The Super Dome, Masaki jijini Dar es Salaam
Mkurugenzi Mtendaji wa Ecobank Tanzania, Dkt. Charles Asiedu(kulia) akimkabidhi Tuzo ya Mwamuzi Bora wa Kiume wa Mwaka, Shabani Mahobonya (kushoto) kwenye Tuzo za BMT 2025 zilizotolewa katika ukumbi wa The Super Dome, Masaki jijini Dar es Salaam
Wafanyakazi wa Ecobank Tanzania wakiongozwa na Mkurugenzi Mtendaji, Dkt. Charles Asiedu(wa kwanza kushoto) wakiwa kwenye hafla ya utoaji wa Tuzo za BMT 2025.
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba pamoja na viongozi wengine wakiwa kwenye picha ya pamoja na wadhamini wa Tuzo za BMT 2025.
Wafanyakazi wa Ecobank Tanzania wakiwa kwenye picha ya pamoja katika Tuzo za BMT 2025


WATUMISHI WA NBAA WASHIRIKI MAADHIMISHO YA MEI MOSI 2026 DAR ES SALAAM


Watumishi wa Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA) wameshiriki katika maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani (Mei Mosi) mwaka 2026, yaliyofanyika kimkoa katika Wilaya ya Ilala, katika Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.

Mgeni rasmi katika maadhimisho hayo alikuwa Mhe. Albert Chalamila, Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, ambaye alisisitiza umuhimu wa wafanyakazi kutambua nafasi yao katika kujenga taswira ya serikali. Alieleza kuwa mfanyakazi mmoja anaweza kuchangia serikali kupendwa au kuchukiwa, hivyo aliwahimiza wafanyakazi wote kuendelea kutekeleza majukumu yao kwa uaminifu, weledi na kujituma, akibainisha kuwa serikali inawajali na kuthamini mchango wao.

Maadhimisho hayo ya Siku ya Wafanyakazi Duniani (Mei Mosi) yameambatana na kaulimbiu isemayo: “Kazi zenye Staha ni Nguzo Imara kwa Maendeleo Endelevu katika Utekelezaji wa Dira ya Taifa 2050.”

Ushiriki wa watumishi wa NBAA katika maadhimisho hayo unaonesha dhamira ya taasisi hiyo kuendelea kuunga mkono juhudi za serikali katika kukuza utamaduni wa kazi, uwajibikaji na maendeleo endelevu nchini.
Baadhi ya Watumishi wa Bodi ya Taifa ya wahasibu na wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA) wakipita mbele ya Jukwaa kuu huku wakiwa na bango lenye ujumbe kuhusiana Wafanyakazi wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani yaliyofanyika katika Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya Watumishi wa Bodi ya Taifa ya wahasibu na wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA) wakiwa kwenye picha ya pamoja wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani yaliyofanyika katika Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.