HABARI

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

MATUKIO

MICHEZO

SIASA

Ecobank Tanzania Yatoa Elimu ya Huduma za Kifedha Maonesho ya Sabasaba


Ecobank Tanzania imeendelea kutoa elimu kwa wananchi kuhusu huduma mbalimbali za kifedha kupitia ushiriki wake katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Sabasaba yanayoendelea katika Viwanja vya Julius Nyerere, Dar es Salaam, ambapo banda lake linapatikana katika Kijiji cha Bima kinachosimamiwa na Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania (TIRA).

Akizungumza katika maonesho hayo, mwakilishi wa Ecobank amesema benki hiyo inatoa huduma mbalimbali za kifedha zinazolenga kukidhi mahitaji ya watu binafsi, wafanyabiashara na taasisi, huku ikiwapa wateja suluhisho la huduma za benki kwa urahisi na ufanisi.

Ameeleza kuwa miongoni mwa huduma zinazotolewa ni "Saving Account", ambayo haina makato ya kila mwezi na humruhusu mteja kuweka na kutoa fedha wakati wowote kulingana na mahitaji yake.

Aidha, amesema Ecobank inatoa "Current Account", inayomwezesha mteja kupata huduma ya "Overdraft", inayomruhusu kutumia fedha zinazozidi salio lililopo kwenye akaunti kwa muda wa hadi siku 14, kwa kuzingatia masharti ya benki.

Vilevile, benki hiyo inatoa mikopo ya muda mfupi na muda mrefu kwa makundi mbalimbali yakiwemo watumishi wa umma, wafanyabiashara na watu binafsi, pamoja na mikopo ya ujenzi na ununuzi wa nyumba.

Mbali na huduma za benki, Ecobank pia inatoa huduma mbalimbali za bima zikiwemo bima ya nyumba, magari na afya, kwa kushirikiana na wadau wake wa sekta ya bima, ikiwa ni sehemu ya kuwapatia wateja huduma za kifedha zilizounganishwa katika eneo moja.

Ecobank imewahimiza wananchi wanaotembelea Maonesho ya Sabasaba kutembelea banda lake lililopo Kijiji cha Bima (TIRA) ili kupata elimu zaidi kuhusu huduma za benki na bima, kufungua akaunti, kupata ushauri wa kifedha na kufahamu fursa mbalimbali zinazotolewa na benki hiyo.
Mkuu wa kitengo cha Wateja Binafsi na Biashara kutoka Ecobank Tanzania, Joyce Ndyetabura akimsikiliza mfanyakazi wa Ecobank Tanzania walipokuwa wanatoa huduma katika maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Sabasaba yanayoendelea jijini Dar es Salaam ambapo banda lake linapatikana katika Kijiji cha Bima kinachosimamiwa na Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania (TIRA).
Watumishi wa Ecobank Tanzania wakitoa elimu katika maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Sabasaba yanayoendelea jijini Dar es Salaam.

Mkuu wa Kitengo cha Biashara kwa Wateja Wakubwa (Commercial Banking) Joyce Ndyetabura akiwa kwenye picha ya pamamo na watumishi wa Ecobank Tanzania katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Sabasaba yanayoendelea katika Viwanja vya Julius Nyerere, Dar es Salaam, ambapo banda lake linapatikana katika Kijiji cha Bima kinachosimamiwa na Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania (TIRA).

VIONGOZI MBALIMBALI WATEMBELEA BANDA LA NBAA MAONESHO YA SABASABA


Waziri wa Fedha Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb) (kushoto), akisikiliza maelezo kutoka kwa mfanyakazi wa NBAA alipotembelea banda la Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA) lililopo katika jengo la Wizara ya Fedha katika Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba), yenye Kaulimbiu ya "Maonesho ya Biashara ya Kimataifa Sabasaba ni Fahari ya Tanzania.
Waziri wa Fedha Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb) (kushoto) akipokea zawadi alipotembelea banda la Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA) lililopo katika jengo la Wizara ya Fedha katika Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba)
Spika wa Bunge Mstaafu, Bi. Anne Makinda (kushoto) akisaini kitabu alipotembelea banda la NBAA lililopo katika jengo la Wizara ya Fedha katika Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba)
Spika wa Bunge Mstaafu, Bi. Anne Makinda (kushoto) akizungumza na watumishi wa Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA) alipotembelea banda la Bodi hiyo lililopo katika jengo la Wizara ya Fedha katika Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba)
Mwenyekiti wa Baraza la Uongozi wa Chuo, CPA Dkt. Mwamini Tulli akisikiliza maelezo kutoka kwa mfanyakazi wa NBAA alipotembelea banda la Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA) lililopo katika jengo la Wizara ya Fedha katika Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba)
Mwenyekiti wa Baraza la Uongozi wa Chuo, CPA Dkt. Mwamini Tulli akisaini kitabu alipotembelea banda la NBAA lililopo katika jengo la Wizara ya Fedha katika Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba)
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma (PPRA), Bw. Dennis Simba akisaini kitabu alipotembelea banda la NBAA lililopo katika jengo la Wizara ya Fedha katika Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba)
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma (PPRA), Bw. Dennis Simba akiwa kwenye picha ya pamoja na watumishi wa NBAA alipotembele banda la Bodi hiyo lililopo katika jengo la Wizara ya Fedha katika Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba).
Maonesho yakiendelea katika banda la NBAA
Mkurugenzi wa Huduma za Shirika katika Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA) CPA Kulwa Emmanuel Malendeja akiwa kwenye picha ya pamoja na watumishi wa Bodi hiyo kwenye Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba).

RAIS WA MSUMBIJI AWASILI NCHINI KWA ZIARA YA KIKAZI YA SIKU TATU



Rais wa Jamhuri ya Msumbiji Mheshimiwa Daniel Francisco Chapo amewasili nchini kuanza ziara ya kikazi ya siku tatu, kuanzia Julai 2 -4 , 2026.

Katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam Mheshimiwa Rais Daniel Francisco Chapo alipokelewa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Dkt. Mahmoud Thabit Kombo (Mb) ambaye aliambatana na viongozi wengine waandamizi wa Serikali.

Akiwa nchini, Mheshimiwa Rais Chapo atafanya mazungumzo rasmi na mwenyeji wake Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Ikulu, jijini Dar es Salaam.

Aidha, Mheshimiwa Rais Chapo atafungua rasmi Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam; atamtembelea Mama Maria Nyerere kwa lengo la kumsalimia na ataweka jiwe la msingi la ujenzi wa Ubalozi wa Msumbiji jijini Dar es Salaam.

Itakumbukwa kuwa, ziara hii ni ya tatu kwa Mheshimiwa Chapo kufanyika hapa nchini tangu alipoingia madarakani mwaka 2024 jambo lililoakisi dhamira ya viongozi wa nchi hizi mbili ya kuendelea kuimarisha mahusiano ya kirafiki na ushirikiano wa uhusiano wa kindugu kati ya Tanzania na inatarajiwa kufungua fursa mpya za ushirikiano wa karibu yaliyojengwa juu ya historia ya ujirani mwema na mshikamano wa muda mrefu.




































NBAA YASHIRIKI MAONESHO YA 50 YA KIMATAIFA YA BIASHARA YA SABASABA 2026


Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA) inashiriki Maonesho ya Kimataifa ya Biashara ya 50 yanayoendelea kwenye Viwanja vya Sabasaba jijini Dar es Salaam, ikiwa ni jitihada za kuonyesha huduma mbalimbali zinazotolewa na Bodi hiyo pamoja na kutoa elimu kwa wananchi.

Banda la NBAA lipo ndani ya jengo la Wizara ya Fedha linawahudumia wananchi kwa kutoa maelekezo ya usajili wa mitihani katika ngazi mbalimbali za Taaluma ya Uhasibu, pamoja na kutoa maelekezo kuhusu ulipaji wa ada na huduma nyingine muhimu.

Katika kipindi hiki cha Sabasaba Bodi imewasogezea wananchi huduma karibu kwa kutoa huduma zote kama vile usajili wa watahiniwa wa mitihani ya Bodi, usajili wa wanachama wa ngazi mbalimbali, usajili wa Makampuni, usajili wa kozi mbalimbali zinazoendeshwa na Bodi.

Aidha, NBAA kwa sasa inatumia mifumo ya kidijitali kutoa huduma zake, ambapo wananchi wanaweza kufikia huduma hizo kupitia tovuti rasmi ya Bodi ambayo ni www.nbaa.go.tz.

Maonesho haya ya Sabasaba ni fursa kubwa kwa Bodi ya NBAA kuwasiliana moja kwa moja na wananchi na wadau mbalimbali wa taaluma ya uhasibu na ukaguzi, ili kuboresha utoaji wa huduma na kuelimisha kuhusu umuhimu wa taaluma hiyo katika maendeleo ya taifa.
Wafanyakazi wa Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA) wakiwa kwenye picha ya pamoja katika banda la Bodi hiyo lililopo ndani ya jengo la Wizara ya Fedha.
Huduma zikiendelea kwenye banda la NBAA

TCAA Yavutia Viongozi wa Serikali Maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma


Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi, Prof. Godius W. Kahyarara akisaini kitabu katika banda la Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) kwenye maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayofanyika katika viwanja vya Chinangali Park, jijini Dodoma.
Meneja wa TCAA Kituo cha Dodoma Aswile Kamendu akitoa maelezo kwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi, Prof. Godius W. Kahyarara aliyefika katika banda la Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) kwenye maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayofanyika katika viwanja vya Chinangali Park, jijini Dodoma.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi, Prof. Godius W. Kahyarara akipokea zawadi kutoka kwa Meneja wa TCAA Kituo cha Dodoma Aswile Kamendu alipotembelea banda la Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) kwenye maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayofanyika katika viwanja vya Chinangali Park, jijini Dodoma.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi, Prof. Godius W. Kahyarara akizungumza jambo katika banda la Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) kwenye maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayofanyika katika viwanja vya Chinangali Park, jijini Dodoma.
Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Juma Mkomi akisaini kitabu katika banda la Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) kwenye maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayofanyika katika viwanja vya Chinangali Park, jijini Dodoma.

Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Juma Mkomi akiwa kwenye picha ya pamoja na Watumishi wa TCAA alipotembelea katika banda la Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) kwenye maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayofanyika katika viwanja vya Chinangali Park, jijini Dodoma.
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA), Dkt. Habibu J. Suluo akisaini kitabu katika banda la Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) kwenye maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayofanyika katika viwanja vya Chinangali Park, jijini Dodoma.

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA), Dkt. Habibu J. Suluo akizungumza jambo alipotembelea banda la Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) kwenye maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayofanyika katika viwanja vya Chinangali Park, jijini Dodoma.

Mkuu wa Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima (TEWW), Prof. Philipo Sanga akisaini kitabu katika banda la Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) kwenye maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayofanyika katika viwanja vya Chinangali Park, jijini Dodoma.

Afisa Rasilimali Watu TCAA Lucy Ngowo (wa pili kulia) akikabidhi zawadi kwa Mkuu wa Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima (TEWW), Prof. Philipo Sanga alipotembelea banda la Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) kwenye maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayofanyika katika viwanja vya Chinangali Park, jijini Dodoma.


Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi, Prof. Godius Kahyarara, Juni 22, 2026 alitembelea banda la Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) katika Maonesho ya Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma, yanayofanyika katika viwanja vya Chinangali Park, jijini Dodoma.

Akiwa katika banda hilo, Prof. Kahyarara alipokewa na Meneja wa TCAA Kituo cha Dodoma, Aswile Kamendu, ambaye alimueleza juhudi mbalimbali zinazotekelezwa na Mamlaka katika kuimarisha sekta ya usafiri wa anga nchini, ikiwemo maboresho ya miundombinu ya anga, kuimarisha usalama wa safari za anga pamoja na kuhimiza matumizi ya teknolojia za kisasa katika utoaji wa huduma.

Akizungumza mara baada ya kutembelea banda hilo, Prof. Kahyarara alisema: “Serikali inaendelea kuwekeza katika kuimarisha sekta ya usafiri wa anga kwa kuhakikisha miundombinu inaboreshwa, usalama unaimarishwa na teknolojia za kisasa zinatumika ili kuongeza ufanisi wa huduma. Hatua hizi ni muhimu katika kuchochea maendeleo ya uchumi na kuimarisha ushindani wa nchi yetu kikanda na kimataifa.”

Mbali na Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi, wageni wengine waliotembelea banda la TCAA ni pamoja na Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Juma Mkomi, Mkuu wa Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima (TEWW), Prof. Philipo Sanga, na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA), Dkt. Habibu J. Suluo, na kupata maelezo kuhusu majukumu ya Mamlaka, mafanikio yaliyopatikana pamoja na mikakati inayotekelezwa katika kuimarisha usalama, ufanisi na maendeleo ya sekta ya usafiri wa anga nchini.

Kupitia ushiriki wake katika maonesho hayo, TCAA inatumia fursa hiyo kuwahamasisha vijana na wadau wa sekta ya usafiri wa anga kuchangamkia fursa za mafunzo zinazotolewa na Chuo cha Usafiri wa Anga Tanzania (CATC), chuo kinachomilikiwa na TCAA. Mafunzo yanayotolewa chuoni hapo yanalenga kukabiliana na changamoto ya upungufu wa wataalamu wa ndani katika sekta ya usafiri wa anga kwa kuzalisha wataalamu wa kutosha na wenye viwango vinavyokubalika kimataifa.

Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma mwaka huu yanaongozwa na kaulimbiu isemayo “Kuchochea Uwajibikaji Jumuishi kwa Huduma Endelevu”, ikisisitiza umuhimu wa matumizi ya teknolojia katika kuboresha huduma kwa wananchi na kuimarisha uwajibikaji katika utumishi wa umma.

Wiki ya Utumishi wa Umma huadhimishwa kila mwaka kwa lengo la kutambua mchango wa watumishi wa umma katika maendeleo ya taifa, ambapo maadhimisho ya mwaka huu yanatarajiwa kufikia kilele chake Juni 23, 2026.