HABARI

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

MATUKIO

MICHEZO

SIASA

NACTE YAFUTA LESENI YA VYUO VYA UFUNDI 26

Ndugu wasomaji wetu tunaomba support yenu kwa kutangaza nasi hapa kwenye hii blog kwa bei nafuu ili tuweze kuendelea kutoa habari bila tatizo lolote. Wasiliana nasi kupitia namba +255713363965 / +255755274953. Tunashukuru kwa ushirikiano wenu.



·      Nacte  yafuta leseni ya vyuo vya ufundi 26
·        20 vyasimamishiwa programu zisizosajiliwa na baraza hilo
·        2 vyasimamishwa kwa kutokuwa na usajili
            
Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE) limevifungia vyuo vya ufundi 26 kutokana na makosa mbalimbali, ikiwamo kushindwa kuzingatia masharti yaliyowekwa na kutoa mafunzo ambayo hayajathibitishwa.

    Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam, Kaimu Katibu mtendaji wa NACTE,    Dkt.Adolf Rutayuga, alisema kuwa wamekuwa wakifuatilia vyuo vya ufundi ili kutathmini kama vinafuata viwango vya ubora wa kitaaluma vilivyowekwa na NACTE katika kutoa mafunzo. 

“Kama ilivyoelezwa katika sheria za Usajili na Kanuni za leseni, kutozingatia  matakwa yoyoye yaliyowekwa na NACTE ni kosa kisheria. Kanuni zinasema kuwa hatua kali zinawezakuchukuliwa kwa kila kosa. Kulingana na matokeo  ya ufuatiliaji uliofanywa na timu maalumu, Baraza lina uwezo wa kuchukua hatua dhidi ya taasisi au vyuo vinavyoshindwa kutekeleza kanuni zilizowekwa,” alisema.

Alisema kuwa baada ya kufanya utafiti wao, wamebaini vyuo 26 vilishindwa kuzingatia masharti yaliyowekwa na NACTE katika cheti cha usajili, huku vyuo 20 vikitoa mafunzo ambayo hayajathibitishwa chini ya idara isiyotambulika,wakati vyuo viwili vikiwa na vituo vya satellite/Kampasi ambavyo navyo havijathibitishwa na chombo husika.

“Baraza linaufahamisha umma kwamba limechukua hatua mbalimbali kwa vyuo vya ufundi 48 kutokana na makosa mbalimbali, yaliyofanywa na vyuo hivyo ambapo limesitisha vyeti vilivyotolewa kwa vyuo 20 ambavyo vimeshindwa kuzingatia masharti yaliyowekwa kwenye Cheti cha Usajili.
“Uamuzi huu umefanywa kwa mujibu wa Kanuni ya 20 ya Usajili wa Vyuo vya Ufundi ya mwaka 2001,” alisema.

Rutayuga alisema kwamba vyuo vilivyofutiwa usajili kutokana na kosa la kutoa mafunzo ambayo hayajathibitishwa chini ya idara isiyotambulika ni 26.“Vyuo vya ufundi vinatakiwa kupata kwa idhini ya Baraza kabla ya kuanza kutoa mafunzo yoyote. Idhini hiyo inahusu uthibitisho wa mtaala kwa ajili mafunzo yaliyokusudiwa na utambuzi wa idara iliyopangwa kutoa mafunzo hayo,” alisema. 

Juu ya vyuo vyenye vituo vya setelite, kampasi, Dkt.Adolf Rutayuga alisema kuwa Baraza linahitaji mafunzo kutolewa katika vituo vilivyosajiliwa/kampasi za vyuo vikuu baada ya kuthibitishwa kwamba vinastahili kutoa mafunzo. 

“Hata hivyo, taasisi mbili zimebainika kutoa mafunzo katika vituo vya satellite/vyuo vikuu ambavyo havijasajiliwa na Baraza na hivyo kuadhibiwa. Vyuo hivyo navyo vimefutiwa leseni,” alisema Rutayuga.

NACTE ni bodi iliyoanzishwa kisheria chini ya Sheria ya Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi, kifungu cha 129, kusimamia na kuratibu utoaji wa elimu ya ufundi na mafunzo nchini Tanzania.  Chini ya sheria hiyo, ili kufikia na kudumisha hali ya mtoa mafunzo, vyuo vyote vinatakiwa viwe vimesajiliwa, vibali na kuwa mitaala iliyopitishwa na baraza. Vyuo haviruhusiwi kuanza kutoa kuanza kutoa huduma yoyote ya mafunzo bila idhini ya baraza.

Jedwali 1: Vyuo vya Ufundi vilivyofutiwa usajili
S/N
CHUO
1
Institute of Management and Development Studies – Iringa
2
Green Hill Institute – Mbeya
3
Institute of Business and Social Studies – Mbeya
4
Loyal College of Africa – Mbeya
5
Mbeya Training College – Mbeya
6
Mbengwenya College of Business and Information Technology –Mbinga
7
New Focus College – Mbeya
8
Shukrani International College of Business and Administration –  Mbeya
9
Majority Teachers College – Mbeya
10
Rukwa College of Health Sciences – Sumbawanga
11
MAM Institute of Education – Mbeya
12
Belvedere Business and Technology College – Mwanza
13
Geita Medical Laboratory Sciences and Nursing Training College – Geita
14
Global Community College – Geita
15
Muleba Academy Institute – Muleba
16
St. Bernard Health Training Institute – Katoro, Geita
17
Victoria Institute of Tourism and Hotel Management – Mwanza
18
Gisan Institute of Health Sciences – Mwanza
19
Dar es Salaam Institute of Business Management – Dar es Salaam
20
SAMFELIS College of Business Studies – Dar es Salaam
21
Ellys Institute of Technology – Bunda, Mara
22
Tanzania Institute of Chartered Secretaries and Administrators – Arusha
23
Emmanuel Community College – Kibaha
24
Modern Commercial Institute – Dar es Salaam
25
Marian College of Law – Dar es Salaam
Jedwali 2: Vyuo vya Ufundi vinavyotoa mafunzo ambayo hayajathibitishwa
S/N
CHUO
MAFUNZO
1
MISO Teachers College – Mafinga
Competence Building Network (CBN) - a Certificate in Early Childhood Education
2
Tusaale Teachers College - Mafinga
Competence Building Network (CBN) - a Certificate in Early Childhood Education
3
The St. Joseph’s College Institute of Business and Management (SJCIBM) – Morogoro

4
The Golden Training Institute – Dar es Salaam






5
Nkrumah Mkoka Teachers College – Kongwa, Dodoma

6
National Institute of Agriculture (Chuo cha Kilimo cha Taifa) – Arusha

7
Musoma Utalii Training College – Musoma

8
Mwanza Polytechnic Institute – Mwanza

9
Mwanza Polytechnic Institute – Maswa

10
Ruter Institute of Financial Management – Mwanza

11
Dar es Salaam Institute of Journalism and Mass Communication – Mwanza

12
Dar es Salaam Institute of Journalism and Mass Communication – Geita

13
Dar es Salaam Institute of Journalism and Mass Communication – Bukoba

14
Singni International Training Institute – Bukoba

15
Dar es Salaam Institute of Journalism and Mass Communication – Kahama

16
Dar es Salaam Institute of Journalism and Mass Communication – Simiyu

17
Richrise Teachers College – Geita

18
Twiga Training Institute – Musoma

19
Zoom Polytechnic Institute – Bukoba

20
St. Thomas Training College – Shinyanga

Jedwali 3: Vyuo vya Ufundi vyenye Vituo vya Satellite / Kampasi
S/N
CHUO
1
MISO Teachers College – Mafinga
2
Rungemba Teachers College – Mafinga

VYUO 175 NCHINI VYAPEWA NOTISI YA KUSHUSHWA HADHI

Ndugu wasomaji wetu tunaomba support yenu kwa kutangaza nasi hapa kwenye hii blog kwa bei nafuu ili tuweze kuendelea kutoa habari bila tatizo lolote. Wasiliana nasi kupitia namba +255713363965 / +255755274953. Tunashukuru kwa ushirikiano wenu.


Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE), Mhandisi Steven Mlote(kushoto)akisisitiza jambo kwa waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam,wakati wa kutoa tamko la baraza hilo kuvifutia Usajili baadhi ya vyuo na vyuo 175 vimepewa notisi ya kushushwa hadhi,5 vyafutiwa Usajili na 41 vimetakiwa kujisajili mara moja,ikiwa katika jitihada za kuboresha elimu ya ufundi nchini,ikiwa katika jitihada za kuboresha elimu ya ufundi nchini,Katikati Kaimu wa baraza hilo Dkt. Adolf Rutayuga na Mkurugenzi wa Udhibiti,Ufuatiliaji na Tathimini Bi. Agness Ponera

Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE) limetangaza kuwa vyuo 5 vimefungwa kuendesha mafunzo na kufutwa kwenye rejista ya vyuo vya ufundi nchini.
Pia Baraza limetangaza kuwa vyuo 41 vinavyotoa elimu ya ufundi bila kusajiliwa kwa mujibu wa sheria vimepewa muda wa wiki mbili na kutakiwa vijisajili mara moja kwenye Baraza hilo kabla ya kuchukuliwa hatua kali za kisheria.

Vilevile, vibali vya usajili wa vyuo 112 vya kutoa elimu ya ufundi vimefikia ukomo hivyo vinapaswa kutekeleza masharti ya Usajili; wakati vyuo 57 vimefikia ukomo wa ithibati, hivyo inapaswa kutekeleza masharti ya ithibati, imetangazwa jana.

Akiongea katika mkutano na waandishi wa habari, Mwenyekiti wa Baraza (NACTE), Mhandisi Steven Mlote, amesema Baraza limetoa muda wa mwezi mmoja kwa vyuo 112 kutekeleza masharti ya usajili na vyuo 52 kutekeleza masharti ya ithibati kwa mujibu wa sheria za uendeshaji vyuo vya ufundi nchini, na vyuo vitakavyoshindwa kutekeleza agizo hili vitafungiwa mara moja.


Mhandisi Mlote pia alitoa onyo akisema “vyuo 41 vinavyotoa elimu ya ufundi bila kusajiliwa kwa mujibu wa sheria nimevipa muda wa wiki mbili na navitaka vijisajili mara moja kwenye Baraza kabla ya kuchukuliwa hatua kali za kisheria”.

Mhandisi Mlote alivitaja vyuo vyote vyenye matatizo kama ifuatavyo:










TAARIFA KWA UMMA KUHUSU KUFUNGULIWA KWA MFUMO WA UDAHILI WA PAMOJA (CAS) UNAORATIBIWA NA NACTE NA KUTANGAZWA KWA MAJINA YA WAOMBAJI UDAHILI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KOZI ZA CHETI NA DIPLOMA

Ndugu wasomaji wetu tunaomba support yenu kwa kutangaza nasi hapa kwenye hii blog kwa bei nafuu ili tuweze kuendelea kutoa habari bila tatizo lolote. Wasiliana nasi kupitia namba +255713363965 / +255755274953. Tunashukuru kwa ushirikiano wenu.


Baraza linapenda kutoa taarifa kuwa Mfumo wa Udahili wa Pamoja (CAS) umefunguliwa tena kuanzia tarehe 22 Julai 2016 ili kujaza nafasi za udahili zilizo wazi baada ya Baraza kuchagua waombaji udahili waliowasilisha maombi yao kuanzia tarehe 4 Machi 2016 hadi tarehe 3 Juni 2016. 
Mwisho wa kuwasilisha maombi ni  tarehe 5 Agosti 2016 saa sita usiku.

Waombaji wapya na baadhi ya waombaji walioshindwa kukamilisha maombi yao kupitia mtandao ilipofika tarehe 3 Juni 2016, wanaarifiwa kuanza kuwasilisha maombi ya udahili kupitia Mfumo wa Udahili wa Pamoja (CAS) ili kujaza nafasi zilizo wazi. Waombaji wanahimizwa kutumia muda huu wa nyongeza ili kuwasilisha maombi.


Baraza linapenda pia kuwaarifu waombaji udahili na umma kwa ujumla kuwa vikao vya Kamati za kuidhinisha majina ya waombaji udahili kupitia Mfumo wa Udahili wa Pamoja (CAS) vilipitisha orodha ya majina  ya wenye sifa za udahili kulingana na nafasi za udahili kwa kila kozi zitolewazo na vyuo husika kati ya tarehe 18 Julai 2016 na 21 Julai 2016. 
Majina ya waombaji waliochaguliwa kwa kila kozi itolewayo na chuo husika yamekabidhiwa vyuoni kupitia Mfumo wa Udahili wa Pamoja (CAS). 

Waombaji waliochaguliwa nao wamearifiwa kupitia kurasa (profile) zao binafsi au kwa KUBOFYA HAPA. Waombaji ambao hawakuchaguliwa wamejulishwa sababu zilizowafanya wasichaguliwe kupitia kurasa (profile) zao pia. 


Kwa waombaji wa Shahada ya Kwanza waliowasilisha maombi yao kupitia NACTE, Baraza linapenda kuwaarifu kuwa, mashauriano kati ya NACTE na Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU) yanaendelea kufanyika ili kufanikisha udahili wa waombaji wa kozi za Shahada ya Kwanza kama Serikali ilivyoagiza.


Imetolewa na

Ofisi ya Katibu Mtendaji

NACTE

Tarehe: 22 Julai, 2016