BREAKING NEWS: NDEGE YA ALGERIA ILIYOKUWA NA 116 YAANGUKA


Ndege ya shirika la Air Algerie la Algeria iliyokuwa ikitoka nchini Burkina Faso kwenda Algiers na kuripotiwa kupotea kwenye radar mapema leo, imethibitishwa kuwa imeanguka.

Msako wa kutafuta mabaki ya ndege hiyo unaendelea na ilikuwa na abiria zaidi ya 100 na wafanyakazi 6.
Awali mamlaka inayohusika na uchunguzi wa anga ilisema ilipoteza mawasiliano na ndege hiyo saa 0155 GMT, au dakika 50 baada ya kupaa. Hiyo ina maana kuwa ndege hiyo imepotea kwa saa kadhaa kabla ya habari hiyo kujulikana.
Ndege hiyo ilikuwa ikitoka Ouagadougou, mji mkuu wa Burkina Faso.
;;

No comments

Powered by Blogger.