HABARI

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

MATUKIO

MICHEZO

SIASA

» »Unlabelled » MABOMU NA RISASI ZARINDIMA KARIAKOO KUHUSU UVUNJWAJI WA NYUMBA

Askari wa Kikosi Cha kutuliza Ghasia FFU wakiweka ulinzi mkali eneo la Kariakoo baada ya kufunga mitaa ya Kongo na ile ya jirani kutokana na kuibuka vurugu zilizotokana na ugonvi wa nyumba ambayo kwa maelezo ya watu wa karibu nyumba hiyo ilikuwa na mgogoro kwa zaidi ya miaka 20 kati ya wamiliki na wapangaji kutokana na kutengeneza hati feki.
Mmoja wa majeruhi kwenye vurugu hizo akiondolewa eneo la soko la Kariakoo baada ya kuanguka chini kutokana na milipuko ya mabomu ya machozi yaliyokuwa yakitumiwa na askari polisi waliofika kutuliza ghasia katika eneo hilo, ambayo iliambatana na mawe yaliyokuwa yakirushwa na vijana waliokua wakitetea upande mmoja wa ugomvi huo.
Wananchi wakizungumza na waandishi wa habari kutoa maoni yao juu ya mgogoro huo.
Kikosi cha kampuni ya Yono Auction Mart iliyopewa tenda ya kusimamia ubomoaji wa nyumba hiyo chini ya ulinzi mkali wa polisi wakiendelea na kazi kwenye nyumba hiyo iliyopo mtaa wa Kongo.
Askari wa kikosi cha kutuliza ghasia (FFU) akifyatua bomu la machozi.
Vijana wakirusha mawe.
  Hali ikiwa tete eneo hilo.
 
Watu wakikimbia ovyo kusalimisha roho zao.
 
Askari kanzu wakilinda usalama eneo la tukio.
 
Umati wa watu na wafanyabishara walioshindwa kufanya biashara zao wakiangalia hali ya mambo.
 
Soko kuu la Kariakoo likiwa limefungwa kufuatia machafuko hayo.
MAENEO ya Kariakoo jijini Dar es Salaam leo yalikuwa hayakaliki kufuatia vijana waliokuwa wakipambana na polisi wakipinga uvunjwaji wa nyumba iliyokuwa ikimilikiwa  na swahiba wao aliyetajwa kwa jina la Shaban Hassan. Nyumba hiyo imekabidhiwa kwa  Samir Sadiq baada ya kushinda kesi Mahakama ya Ilala jijini.
(PICHA : RICHARD BUKOS / GPL) 

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments: