HABARI

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

MATUKIO

MICHEZO

SIASA

» »Unlabelled » MBUNGE LUKUVI AWAPASHA WALANGUZI WA MPUNGA PAWAGA NA IDODI

MBUNGE wa jimbo la Ismani wilaya ya Iringa mkoani Iringa Wiliam Lukuvi amesema kuwa mbinu ya wafanyabiashara wakubwa wa mpunga kuendelea kuwaibia wakulima wa Pawaga na Idodi dawa yake ipo jikoni baada ya kuanzisha mpango kabambe wa kufunga mashine kukoboa mpunga na kuuuza mchele badala ya mpunga.


Lukuvi ambaye pia ni waziri wa nchi ofisi ya waziri mkuu ( sera na uratibu wa bunge) alitoa kauli hiyo Leo Mara baada ya kukagua mfereji wa mradi wa umwagiliaji katika kijiji cha Magozi kata ya Ilolompya ambao utajengwa kwa zaidi ya shilingi bilioni 2.

Alisema kuwa wakulima wa mpunga katika eneo hilo wamekuwa wakilanguliwa mazao Yao ya mpunga na wafanyabiashara hao wakubwa ambao wamekuwa wakinunua mpunga kwa bei ambazo wanapenda wao na sio bei inayomkomboa mkulima .

Lukuvi alisema mfereji huo ambao unajenga unataraji kumwagilia 600 hivyo katika tarafa hiyo ya Pawaga ambayo wananchi wake wanategemea kilimo cha umwagiliaji watapiga hatua kubwa katika kilimo hicho.

Alisema kwa kipindi kirefu kata hiyo ya Pawaga ilikuwa ikikabiliwa na tatizo la njaa ila baada ya serikali kuanzisha mradi huo wa kilimo cha umwagiliaji wananchi wameanza kuondokana na tatizo hilo la njaa na sasa hata maisha Yao kiuchumi yameanza kuboresheka kwa kuongeza ujenzi wa nyumba za bati tofauti na a wali ambapo nyumba za bati hazikuwepo.

Aidha alisema kuwa mbali ya mradi kujengwa kwa kipindi tofauti tofauti serikali kwa bajeti yake ya mwaka 2012/2013 serikali imetenga zaidi ya shilingi milioni 600 kwa ajili ya mradi huo.

Lukuvi alisema kuwa katika tarafa hiyo ya Pawaga kuna mfereji miwili mikubwa ya umwagiliaji ukiwemo mfereji wa Mlenga na huo wa kijiji cha Magozi unaoendelea kujengwa.

Hata hivyo alisema ujenzi huo wa mifereji ya umwagiliaji katika tarafa hiyo imesababisha mapinduzi makubwa ya uchumi kwa wananchi na hivyo kuwataka wananchi kuongeza kasi ya uzalishaji.

Lukuvi alisema katika miaka miwili hii kabla ya uchaguzi mkuu mwaka 2015 anatarajia kuona tarafa hiyo inakuwa na umeme wa uhakika na kuwa njia hiyo itawawezesha kujikomboa kiuchumi zaidi.

Pia alisema upo mkakati wa kujenga Maghara ya kuhifadhia chakula katika tarafa hiyo pamoja na mashine za kukoboa mpunga na kuwataka wafanyabiashara wa mashine za mpunga waliopo mjini Iringa kufika kuwekeza katika tarafa hiyo kwa kujenga mashine .

wakati huo huo Mbunge Lukuvi ametangaza ofa maalum kwa wapiga kura wake ambao wanataka kujenga nyumba za kisasa kuwa ofisi yake itajitolea kununua bati Kiwandani na kuzifikisha hadi mjini Iringa na huko watanunua bati hizo kwa bei ya Kiwandani kwa kuanzia bati 10 na kuendelea.
MWISHO

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments: