Katika Gazeti la Business Times toleo nambari 1248 la Ijumaa, tarehe 10 Agosti 2012, ziliandikwa habari zenye kichwa cha habari chenye maana kuwa “Operesheni za NBC zawekwa chini ya usimamizi wa Benki Kuu”. Katika habari hiyo ilielezwa kuwa Benki Kuu imechukua hatua hiyo kufuatia ripoti za tuhuma kadhaa zihusuzo udhaifu katika uendeshaji wa benki na utawala bora.
Benki
Kuu inapenda kuchukua fursa hii kuueleza umma kuwa haijaweka
operesheni/shughuli za NBC chini yake. Benki hiyo inajiendesha yenyewe
kwa kufuata utaratibu wa Sheria za Makampuni, 2002, Sheria ya Mabenki na
Taasisi za Fedha 2006 na miongozo itolewayo na Benki Kuu kama zilivyo
benki zingine. Wateja wa NBC na Umma kwa ujumla wanashauriwa kuendelea
kufanya biashara na benki hii kama kawaida.
IMETOLEWA NA BENKI KUU YA TANZANIA11AUGUST 2012




No comments:
Post a Comment