HABARI

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

MATUKIO

MICHEZO

SIASA

» »Unlabelled » Wizi wa ajabu na wa kutisha wazuka Dar, kuweni macho sana


Dear Colleagues,
 Naomba niwasimulie yaliyonipata jana ili na ninyi mchukue tahadhari mapema!
 Jioni baada ya kutoka kazini nilielekea nyumbani  Tabata Kinyerezi moja kwa moja na nilipitia njia zifuatazo.Nilipita Fire,Magomeni,Round about ya Kigogo,Tabata-Dampo, moja kwa moja hadi Tabata Segerea then Kinyerezi.Nilipofika njia ya kuingia kwangu,pembeni kuna Bar inaitwa Fantastic na ina Kigorofa,basi nikamkuta jamaa yangu mmoja nilyekuwa na mazungumzo naye then nikapark gari then nikashuka na kuongea naye nikiwa nimesimama umbali kidogo kama hatua kumi na tano na nilikopark gari langu-Noah!Baada ya mazumgumzo ya hardly dk 5 nikarudi kwenye gari ili niingie home,hamadi nikakuta tayari kioo cha gari cha kulia nyuma ya kiti cha dreva umeshavunjwa na wamechukua lap top yangu binafsi, iliyokuwa ndani ya begi na kulikuwa na documents nyingine nyingi na ziliakuwa original docs-vyeti vya shule na kadi za benki!
Ila upande wa pili wa barabara kulikuwa na waendesha pikipiki wenge tu sasa nikaanza kuwauliza je walimwona nani akiingia kwa gari langu,sikupata majibu hata kidogo!Katika kufutailialia na nikaenda polisi,walinieleza kuwa kuna wimbi la vijana ambao hutumia magari ya kifahari na pikipiki ambao kazi yao ndo hiyo tuu!na walijaribu kufutailia zaidi na ikaonekana kuwa hawa watu wanapenda kufuatilia watu nyuma na hata kama kuanzia mjini hadi katika vitongoji vyetu!Hii ni story ya kweli na imenitokea jana jioni ndugu zangu.
Sasa lengo la kuwasimulieni kisa chote hiki ili nanyi mchukue tahadhari!hata kama mtu unashuka kwenda kuchimba dawa,shuka na all your belongings especially your computer na vitu vyote muhimu ndugu zangu.Usipuuzie kwani yaliyonikuta jana sijalala hata kidogo maana Hasara niliyopata ni kubwa isiyopimika ndugu zangu.Katika kundelea na uchunguzi wamebaini kuwa maeneo ya tabata ni hatari sana kwa sasa na hawa wahuni wanatumia gari aina ya Rav 4 nyeusi,na wakati mwingine wanatembea na Toyota OPA.Ndugu zangu nawasihi sana ikiwezekana acha laptop nyumbani  beba external disc au flash disc maana kwenye gari sio tena shehemu nzuri ya kuhifadhia docs zako.
 Hayo ndo yaliyonipa jana na sina jinsi nabaki tu mdomo wazi! Samahanini kama nitakuwa nimewaboa but nawaokoa na ninyi ndugu zangu. Mtu yoyote atakayeona karatasi zime tupwa mahali tafadhali jaribu kuangalia maana na kama ni zangu nitashukuru nikizipata.
Asante Cayus

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments: