HABARI

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

MATUKIO

MICHEZO

SIASA

» »Unlabelled » Maranda, Farijala wafungwa kesi nyingine Epa

 
Rajabu Maranda (Fulana ya Blue) na Farijala Hussein

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam, imewahukumu kutumikia kifungo jela miaka tisa wafanyabiashara watatu; Farijala Hussein, Rajabu Maranda na Ajai Somani na kuwaamuru wafanyakazi watatu wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), kulipa fidia ya Sh. milioni 15 baada ya kupatikana na hatia ya wizi wa fedha kwenye Akaunti ya Madeni ya Nje (Epa) ndani ya BoT na kuisababishia benki hiyo hasara.
Pia imewaamuru wafanyabiashara hao kurejesha Sh. 1,099,400,000.10 na wakishindwa mali zao zitaifishwe, huku wafanyakazi hao wa BoT wakihukumiwa kwenda jela miaka mitatu kila mmoja iwapo watashindwa kulipa faini ya Sh. milioni 5 kila mmoja baada ya kupatiakana na hatia ya kosa la sita la kuisababishia BoT hasara.
Watumishi wa BoT waliohukumiwa hukumu hiyo, ni Imani Mwakosya, Ester Komu na Sofia Lalika.
Hukumu hiyo ilisomwa jana na jopo la mahakimu watatu wakiongozwa na Mwenyekiti, Samwel Karua, Beatrice Mutungi na Illivin Mgeta waliosikiliza kesi hiyo.
Akisoma hukumu hiyo kwa niaba ya jopo hilo, Hakimu Mgeta alisema mshtakiwa wa kwanza, Farijala atatumikia kifungo cha miaka mitatu kwa kosa la pili, miaka miwili kwa kosa la tatu.
Pia alisema Fariajala, Maranda na Somani watatumikia kifungo cha miaka miwili kwa kosa la nne.
Hakimu Mgeta alisema mbali na kifungo hicho, Farijala anaamriwa kurejesha Sh. 82,956,400, ambazo ushahidi umethibitisha kuwa aliiba.
“Pia mshtakiwa wa pili Maranda anaamriwa kurejesha Sh. milioni 616.4 na mshtakiwa wa tatu Somani Sh. milioni 400, ambazo ushahidi wa Jamhuri umethibitisha kuwa waliiba fedha hizo … endapo washtakiwa wote watatu wakishindwa kurejesha fedha hizo mali zao zitaifishwe,” alisema.
Alisema mahakama imekubaliana na hoja za wakili wa utetezi Majura Magafu, kwamba, mshtakiwa wa nne Mwakosya, wa tano Komu na wa sita Lalika waliamini kazi waliyoifanya ilikuwa sahihi, hivyo walikuwa wakitekeleza majukumu yao wasiamriwe kurejesha fedha zinazodaiwa kuchotwa BoT.
Washatkiwa hao walifikishwa mahakamani hapo Novemba 4, 2008, wakikabiliwa na mashtaka sita, likiwamo la kughushi na wizi wa Sh. bilioni 3.8.
Hata hivyo, upande wa Jamhuri umeweza kutoa ushahidi wa kuwatia hatiani washtakiwa katika shtaka la pili la kughushi, hati za kuhamisha mali kwa jina la Kampuni ya Mwibare Farm ya Tanzania na Lakshmi Textile Mills Ltd ya Mumbai.
Katika shtaka la tatu na la nne, walidaiwa kuiba Sh. bilioni 3, 868, 805, 737. 13, mali ya BoT.
Katika shtaka la sita, walidaiwa kuwa Desemba 7, 2005 wakiwa waajiriwa wa BoT, kupitia nyadhifa zao, walizembea kazini na kuisababishia serikali hasara ya kiasi hicho cha fedha.
 
CHANZO: NIPASHE

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments: