Mabaki ya nyumba za marehemu Ernest Mholela zilizobomolewa kabla ya
kumzika akiwa hai kutokana na kutuhumiwa kuwa mchawi. Picha na Stephano
Simbeye
KUTOKANA na tukio la watu wawili kuzikwa
wakiwa hai hivi karibuni Wilaya ya Mbozi, wazee mkoani Mbeya
wameiomba Serikali kuandaa utaratibu wa kutoa ulinzi hasa kwa watu
waliopo vijijini.
Wamesema matukio kama hayo yamewajengea woga na
kusababisha kuishi kwa hofu hali inayosababisha kushindwa kufanya kazi
zao za kila siku na kushiriki katika shuguli za kijamii vizuri.
Akizungumza na mwandishi wa gazeti hili kwa niaba
ya wazee hao, Abel Ambakisye alisema tukio hilo limekuwa tishio kwa
wazee hasa waishio vijijini na kuleta sifa mbaya ya Mkoa wa Mbeya kuwa
ni eneo lenye matukio mabaya.
“Suala hili ni kubwa na baya kwa mkoa wetu, kwani linatutisha sisi wazee kuona watoto na vijana wetu wanatufanyia vitendo vya kinyama kama hiki kilichotokea hivi karibuni cha kuwazika watu wawili wakiwa hai,” alisema.
“Suala hili ni kubwa na baya kwa mkoa wetu, kwani linatutisha sisi wazee kuona watoto na vijana wetu wanatufanyia vitendo vya kinyama kama hiki kilichotokea hivi karibuni cha kuwazika watu wawili wakiwa hai,” alisema.
Aliongeza kuwa “Huu ni unyama hivyo Serikali
kupitia polisi inapaswa kuhakikisha wanafanya uchunguzi wa kina na
kuandaa utaratibu maalumu wa kutupatia ulinzi ili tuweze kuishi kwa
amani”.
Alisema huko nyuma Mkoa wa Mbeya ulisikika kwa
kuwa na matukio ya uchunaji ngozi watu na upigaji nondo, kitendo ambacho
kilisababisha watu wengi kutoka nje ya Mkoa wa Mbeya kuuogopa mkoa huu.
“Lakini Serikali kupitia polisi walikomesha
vitendo hivyo, sasa havipo tena, nguvu hizo sasa zielekezwe katika
kupambana na matukio kama haya ya kuwazika watu wakiwa wazima”alisema.
“Tunaomba Serikali ya kijiji pia ihusike katika
kuvisaidia vyombo vyetu vya ulinzi na usalama, kuhakikisha wazee
wanakuwa na ulinzi ili waweze kuishi kwa amani na utulivu na kushiriki
katika shughuli mbalimbali za maendeleo ya jamii bila kubughudhiwa,”
alisema.
Aliongeza kuwa wazee wanatarajia kuonana na
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Diwani Athumani kwa ajili ya
kuwasilisha maombi yao na kujadiliana jinsi ya kukabiliana na tatizo
hilo na kuangalia mbinu za kufanya ili kulikomesha.
Ambakisye alisema wananchi wa Mkoa Mbeya
wanahitaji kufanya mikakati mbalimbali ya kuleta maendeleo, lakini
vitendo kama hivi vinarudisha nyuma jitihada hizo.
“Kwani hata wawezekezaji wataogopa kuja hapa
mkoani kwetu kuwekeza, kwa kuwa sifa kubwa inayotangazika mkoani kwetu
ni vitendo vya kinyama na hivyo kujenga hofu miongoni mwa wawekezaji,”
alisema.
MWANANCHI
MWANANCHI
No comments:
Post a Comment