HABARI

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

MATUKIO

MICHEZO

SIASA

» »Unlabelled » Vurugu Dumila: Polisi watumia Nguvu, barabara yafungwa kwa muda

 374819 295267233917591 277925452 n1 VURUGU Morogoro: Wananchi wachoma moto magari, magesti house, na kufunga barabara
Kuna maandamano yamefanywa na wananchi eneo la Dumila. Chanzo ni mgogoro kati ya WAKULIMA na WAFUGAJI. Makazi ya wafugaji yamechomwa moto. Mpambano unaendelea wananchi wamebeba silaha za jadi wanaelekea kituo cha POLISI.Wananchi wakulima wanamtaka Mkuu wa Mkoa wa Morogoro (Joel Bendera) kufika kuwatatulia tatizo lao la kunyang'anywa maeneo yao na kuwapatia wafugaji. 

Wananchi hao wamegawanyika katika makundi kadhaa huku kila kundi likifunga barabara ya kuingia na kutoka eneo hilo la Dumila, ambapo wamezuia magari yote yanayopita eneo hilo kutoka Morogoro na kutoka Dodoma.  Tayari Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, ameomba udhuru kutoka katika Kikao cha wakuu wa mikoa, kilichokuwa kikiendelea mkoani Dodoma na yupo njiani akielekea eneo hilo kwa nia ya kukutana na wananchi hao ili kuwasikiliza na kutatua mgogoro huo
 Wafugaji wanapendelewa na mkuu wa wilaya na mapolisi kwa kuwa wanahonga sana.

Mgogoro wa eneo hilo na wilaya ya Kilosa kwa ujumla ni mkubwa sana na wa miaka mingi sana (Nilishawahi kufanya research huko 2003 kuhusu migogoro ya ardhi). Inashindikana kutatuliwa kwa kuwa wafugaji wana uwezo wa kuhonga wakati wakulima hawana uwezo wa kuhonga.


Kumbukeni mgogoro wa Msovero mwaka 2001 ambako watu zaidi ya 100 walikufa. Serikali ya CCM imekuwa ikumbatia hii migogoro bila kutafuta suluhisho la kudumu. Pia mapendekezo ya sheria ya ardhi ambayo yangemaliza kabisa migogoro hii ya wakulima na wafugaji yalikataliwa na wabunge wanaotokea maeneo ya wafugaji kwa kuwa ingewanyima haki ya kugeuza nchi nzima eneo la malisho.


Serikali ya CCM imeshindwa kuleta maendeleo na inashindwa hata kutatua migogoro ya ardhi. Shime watanzania tuikatae CCM.


JAMII FORUMS 

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments: