HABARI

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

MATUKIO

MICHEZO

SIASA

» »Unlabelled » BUYERN MUNICH WATWAA KOMBE LA UEFA CHAMPIONS LEAGUE KWA KUICHAPA BORUSSIA DORTMUND 2-1

 Dimba la Wembley dakika chache kabla ya kuanza kwa mtifuano wa fainali ya Mabingwa Ulaya kati ya Bayern Munich na Borussia Dortmund zote za Ujerumani.
Kansela wa Ujerumani, Angela Merkel (wa pili kulia), akiimba wimbo wa taifa kabla ya kuanza kwa mtanange huo wa fainali kwenye Uwanja wa Wembley jana usiku.
 Mshambuliaji wa Timu ya Buyern Munich, Arjen Robben, (katikati)  Thomas Mueller (kushoto) na  Franck Ribery, wakishangilia kwa pamoja bao la Robben, alilifunga kipindi cha pili wakati wa mchezo wa Fainali wa Ligi ya Mabingwa kati yao na Borussia Dortmund, uliochezwa usiku huu kwenye Uwanja wa Wembley. Katika mchezo huo Buyern wameibuka na ushindi wa mabao 2-1 na kutwaa Kombe hilo.
Kipa wa Bayern, Manuel Neuer, akizuia shuti la mchezaji wa Dortmund, Robert Lewandowski (kushoto)  
 Mchezaji wa Bayern, Bastian Schweinsteiger, Kulia) akiruka na mpira wakati wa mchezo wa Fainali wa Ligi ya Mbingwa kati ya Borussia Dortmund na Bayern Munich uliochezwa kwenye Uwanja wa  Wembley London, usiku huu. Katika mchezo huo Bayern wameibuka na ushindi wa mabao 2-1, na kutwaa Kombe hilo.
Mshambuliaji wa Buyern Munich, Mario Mandzukic, (kulia) akifunga bao.
  Arjen Robben akidhibitiwa na wachezaji wa Borussia Dortmund's Neven Subotic na Lukasz Piszczek (kulia)
 Arjen Robben (kushoto) na Mario Mandzukic, wakishangilia.
 Mchezaji wa Buyern Munich, Franck Ribery (kulia) akiruka kwanja................
Arjen Robben (katikati) akimchambua Kipa wa Dortmund, Roman Weidenfeller na kufunga bao la pili, wakati wa Fainali hiyo.
  Wachezaji wa Bayern Munich wakishangilia baada ya filimbi ya mwisho.
 Nahodha wa FC Bayern Munich ya Ujerumani, Phillip Lahm akiwa ameshikilia taji la Ligi ya Mabingwa Ulaya, walilolitwaa jana usiku baada ya kuichapa Borussia Dortmund pia ya Ujerumani kwa mabao 2-1 katika fainali iliyopigwa kwenye dimba la Wembley jijini London.
 Wachezaji wa Bayern Munich wakiendelea kushangilia ubingwa huo.

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments: