Lema: Nimeaga familia yangu
MBUNGE wa Arusha
Mjini Godbless Lema, amesema tangu alipoamua kupigania haki za wananchi
alikwisha itaarifu familia yake kuwa iwe tayari kupokea mwili wake akiwa
amekufa.
Lema alisema maneno hayo jana jioni katika viwanja vya shule ya
Msingi Ngarenaro, wakati akihutubia maelfu ya wakazi wa Arusha katika
kile alichoita kutoa ufafanuzi wa tukio la yeye kuhusishwa na vurugu
zilizotokea katika Chuo cha Uhasibu wiki iliyopita."
Familia yangu, inafahamu na nilishaiarifu, kwa sababu napigania haki
za wananchi, wawe tayari kupokea maiti yangu na si mgonjwa mwenye
majereha," alisema.
Mbunge huyo, alitumia muda mwingi
kumshambulia kwa maneno makali Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Magesa Mulongo
kama ndiye tatizo kubwa la demokrasia mkoani hapa.
"Mulongo
akishirikiana na polisi, walijaribu kutengeneza kesi ya mauaji ya yule
kijana ti mimi nilihusika,lakini kwa sababu nilishaandaa mikanda ya
video nakuisambaza wakashindwa,
"Nilishajua nia yao,ndio maana
nikatengeneza ile video na kuisambaza kama sivyo wangenipa kesi ya
mauaji,nasema huu ni mpango wa Serikali kutaka kumpiga mchungaji wa
kondoo ili kondoo watawanyike"
Aliishutumu vikali ofisi ya Bunge kwa kushindwa kukemea utaratibu uliotumiwa na polisi kumkamata.
"Nimedhalilishwa
na kudhalilishwa kwangu ni ninyi mmedhalilishwa,kutukanwa mimi ni ninyi
mmetukanwa,hawakuja na kibali cha Spika, wamekuja kama wanavamia nyumba
ya mhalifu"
Lema alitumia mkutano huo, kuitaka Tume ya Taifa ya
Uchaguzi (NEC) kutangaza uchaguzi katika kata ya Sombetini, ili kuwapa
fursa wananchi kupata kiongozi wao.
"CCM kupitia tume iache uhuni
huu kwa hofu kuwa tukishinda tutaunda halmashauri ya jiji kwa kumtoa
meya aliyepo,nawaambia hatutakubali,ama tutafia barabarani au tutazuia
mahakamani,hii haikubaliki"
"Sheria inasema diwani asipohudhuria
vikao vitatu sio diwani tena (Alphonce Mawazo), aliyekuwa diwani
Sombetini kupitia CCM, alijiunga nasi tangu mwaka jana ,hawa watu hawako
makini hata kidogo"
Katika hatua nyingine, aliyewahi kuwa
Mwenyekiti wa Jumuia ya Vijana wa CCM Mkoa wa Arusha ambaye sasa ni kada
maarufu wa Chadema, James Millya amemfungulia mlango wa kutokea mbunge
wa Simanjiro, Christofa Sendeka (CCM).
Millya alidai mwaka 2015,
Simanjiro itakuwa jimbo la Chadema na Mungu akimweka hai na akipitishwa
na chama chake njia ni nyeupe kwake.
"Simanjiro ni
yetu,namtaarifu kuwa 2015 tutashinda kwa kishindo na si hapo tu lengo
letu la msingi ni kuchukua dola" alisema Millya.
MTANZANIA
Post a Comment