HABARI

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

MATUKIO

MICHEZO

SIASA

» »Unlabelled » BAYERN MUNICH WAMTAMBULISHA RASMI PEP GUARDIOLA KATIKA MKUTANO MZITO ALLIANZ ARENA

Guardiola aliungana na Matthias Sammer, Karl-Heinz Rummenigge na Uli Hoeness, Aisema sababu ya kwanza iliyomfanya akubali ofa ya kuifundisha Bayern ni wachezaji wa klabu hiyo na historia yake.
 Waliohudhuria mkutano huo wa kutambulishwa Guardiola bosi mpya Bayern
 Guardiola akiwa na kocha anayeondolewa Bayern, Jupp Heynckes.


Endelea kusoma habari hii kwa kubofya hapa chini



 Pep Guardiola anakuwa kocha wa mabingwa wapya wa Ulaya, Bayern Munich
 Kocha tayari anajisikia nyumbani katikati ya watu
Guardiola akizungumza
Mabingwa wa mataji matatu, Bayern Munich wamemtambulisha kocha wao mpya, Pep Guardiola leo katika Mkutano na Waandishi wa Habari, The Bavarians wakijiandaa kuendelea kutamba katika soka ya nyumbani na Ulaya.
Kocha huyo wa zamani wa Barcelona amesema yuko tayari kukabiliana na changamoto za kufundisha timu iliyofanya vizuri msimu uliopita chini ya Jupp Heynckes, ikishinda mataji ya Ligi Kuu ya nyumbani na makombe mawili, pamoja na Ligi ya Mabingwa Ulaya.
“Lazima nikubali mlinganisho,” alisema Guardiola, akiwa katika vazi nadhifu la suti ya vipande vitatu ya rangi ya kijivu akizungumza Kijerumani kwenye Mkutano uliofanyika ukumbi wa mikutano wa klabu, Allianz Arena.
“Lazima niwe tayari kuishi na hiyo. Nipo chini ya shinikizo, wazi, lakini nafahamu hili na nakubali changamoto hii bila woga na ndiyo maana mimi ni kocha,”alisema.
Guardiola, ambaye aliyeshinda mataji 14 katika miaka minne ya kuwa na Barcelona, usajili wake ni mkubwa Bayern na hasa ikizingatiwa anahamia timu iliyofanya vyema. Alitumia mwaka wake mzima baada ya kuacha kazi Hispania mwaka 2012, kwa kupumzika New York, Marekani.
“Kitu nachofikiria kwa sasa ni zawadi, baraka kuwa hapa na Bayern,”alisema kocha huyo Mspanyola, aliyesaini Mkataba wa miaka mitatu.

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments: