HABARI

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

MATUKIO

MICHEZO

SIASA

» »Unlabelled » TANGAZO LA UZINDUZI WA TAWI LA YANGA MKOANI DODOMA

Na mwandishi wetu, Dodoma
WANACHAMA wapenzi na mashabiki wa timu kongwe ya mpira wa miguu nchini Yanga Afrika tawi la Dodoma waliopo ndani na nje ya mkoa wa Dodoma wametakiwa kufika kwenye mkutano wa kujadili masuala ya uzinduzi wa tawi hilo.
Wito huo umetolewa na katibu msaidizi wa tawi hilo mkoani Dodoma John Banda, ambapo aliwataka wanachama hao kuhudhuria mkutano huo kwa ajili ya maandalizi ya uzinduzi wa tawi utakaofanyika mapema mwaka huu.
Katibu huyo msaidizi aliweka wazi kwamba pamoja na mambo mengine watajadili namna ya ufunguzi wa ofisi ya tawi hilo iliyopo mapinduzi klabu barabara ya Bahi (Bahi Road) Dodoma ambayo iko tayari kwa ajili ya matumizi.
Banda alisema mkutano huo utafanyika jumapili  tarehe 15/9/2013 kuanzia saa nne asubuhi katika ukumbi wa mapinduzi klabu na kuwataka watu wote kuzingatia muda kwani kwa kuanza mapema ni sababu ya kumaliza mapema ili kwenda kwenye shughuli mbalimbali ikiwepo ufuatiliaji wa ligi za Ulaya zinazoendelea.

 ENDELEA KUSOMA HABARI HII KWA  KUBOFYA HAPA CHINI
 
Aliongeza kuwa Dodoma ni katikati ya nchi hivyo kuwataka wanachama mashabiki pamoja na wapenzi wa timu hiyo kufika bila kukosa katika mkutano huo ili kupanga mambo ambayo yanaweza kuwa mfano wa kuigwa na matawi mengine kote nchini.
Alitaabaisha kuwa wanatarajia kuwa viongozi wakuu wa kitaifa wa klabu hiyo kufika mjini Dodoma na kulizindua tawi hilo mapema baada ya mipango ya maandalizi ya shughuli hiyo kukamilika
“Tunatarajia kuwaonesha wanachama wapenzi na mashabiki wa Yanga Tawi la Dodoma ofisi yao ili kuwarahishia kujua maendeleo ya klabu yao kwa ujumla ili tuweze kupanga kwa pamoja tofauti na kuzungumzia mitaani mawazo mazuri yaliyopo kwa mashabiki wa timu bila kufanyiwa kazi”, alisema Banda.

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments: