Iphone 5S zitakazokuwa zikipatikana katika rangi tatu‘Die Hard
customers’ wa simu za iPhone wameamua kupanga foleni nje ya duka la
simu hizo jijini London, Uingereza na kuamua kuweka kambi ya muda kwa
kufunga matenti na kuhamishia makazi yao hapo huku wakisubiri siku rasmi
ya kuanzwa kuuzwa kwa toleo jipya la iPhone5S linalosubiriwa kwa hamu
kote ulimwenguni ambayo ni Ijumaa hii (September 20).
ENDELEA KUSOMA HABARI HII KWA KUBOFYA HAPA CHINI
Mmoja wa wateja hao ambaye hii ni siku pili kushinda na kulala hapo akisubiri kujipatia simu yake mara zitakapoanza kuuzwa, amesema mpaka sasa ameshakataa ofa ya £200 (515,000 Tsh) kwaajili ya kuuza nafasi yake kwenye foleni hiyo na kuwa na matarajio ofa inaweza kuja kufikia £1000(2,575,000)baadaye.
Vijana hao wawili ambao wameweka kambi jana usiku nje ya duka la Apple wamedai kuwa siku zote wao huwa miongoni mwa wateja wa kwanza kuzipata simu mpya za iPhone kila zinapotoka, hivyo wameamua kuweka kambi nje ya duka ili wahakikishe wawe wateja wa kwanza kuzinunua siku ya Ijumaa.






No comments:
Post a Comment