
Anaitwa Shilole na Skwadi lake wakilishambulia jukwaa vilivyo usiku wa jana kwenye tamasha la Serengeti Fiesta 2013
Mmoja wa Wasanii mahiri katika anga ya muziki wa kizazi kipya,Ommy Dimpoz akiwaimbisha mashabiki wake usiku wa leo kwenye uwanja wa Samora,ambapo tamasha la Serengeti fiesta linafanyika usiku huu.
Moja
ya kikundi mahiri kutoka jijini Dar,chenye maskani yake
Kinondoni,KINOKO wakionesha umahiri wao wa kucheza moja ya wimbo wa
Michael Jackson,mbele ya wakazi wa Iringa wakati tamasha la Serengeti
fiesta likiendelea usiku wa leo ndani ya uwanja wa Samora.
ENDELEA KUTIZAMATUKIO HILI KWA KUBOFYA HAPA CHINI
Msanii
aliyewahi kuiwakilisha vyema shindano la BSS, Walter Chilambo akiimba
jukwaani usiku wa leo, wakati tamasha la Serengeti Fiesta 2013 likiendelea
kwenye uwanja wa Samora.

Mmoja ya wasanii wa kike wanaokuja kwa kasi kwenye anga ya muziki wa Bongofleva,Neylee akiimba kwa hisia jukwaani usiku wa leo

Sehemu ya umati wa watu wakifuatilia tamasha la Serengeti Fiesta usiku wa leo ndani ya uwanja wa Samora.
Mzee wa mahaba kutoka Manzabay,Cassim Mganga akiwaimbisha mashabiki
wake jukwaani usiku wa leo mbele ya maelfu ya wakazi wa Iringa na vitongoji
vyake kwenye tamasha la Serengeti Fiesta 2013.

Anaitwa
Linah,moja ya wasanii wanaofanya vyema kwenye anga ya muziki wa
Bongofleva akiimba kwa hisia jukwaani,huku shangwe za mashabiki zikivuma
kila kona ya uwanja.
Anajiita Rais wa Manzese,kutoka kundi la Tip Top Connections,Madee akiwaimbisha mashabiki wake wimbo wa Nani kaiba yangu usiku wa leo kwenye tamasha la serengeti fiesta 2013,linalofanyika ndani ya uwanja wa Samora mkoani Iringa.
Mmoja wa madansa machachari sana kutoka THT,aitwaye Msami akiwa amebebwa juu na mashabiki baada ya kuonesha umahiri wake wa kuyarudi mangoma jukwaani.
Wasanii wanaokuja juu katika anga ya muziki wa kizazi kipya-hip hop.Stamina na Young Killer wakilishambulia jukwaa kwa pamoja huku mayowe yakiwa yametawala kila kona ya uwanja.
Pichani ni sehemu ya wakazi wa Mkoa Iringa na vitongoji vyake wakiwa
wamejitokeza kwa wingi usiku wa leo kwenye tamasha la Serengeti Fiesta 2013
linaloendelea kufanyika hivi sasa katika uwanja wa Samora.
HABARI NA JIACHIE BLOG
Anajiita Rais wa Manzese,kutoka kundi la Tip Top Connections,Madee akiwaimbisha mashabiki wake wimbo wa Nani kaiba yangu usiku wa leo kwenye tamasha la serengeti fiesta 2013,linalofanyika ndani ya uwanja wa Samora mkoani Iringa.
Mmoja wa madansa machachari sana kutoka THT,aitwaye Msami akiwa amebebwa juu na mashabiki baada ya kuonesha umahiri wake wa kuyarudi mangoma jukwaani.
Wasanii wanaokuja juu katika anga ya muziki wa kizazi kipya-hip hop.Stamina na Young Killer wakilishambulia jukwaa kwa pamoja huku mayowe yakiwa yametawala kila kona ya uwanja.

HABARI NA JIACHIE BLOG











No comments:
Post a Comment