HABARI

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

MATUKIO

MICHEZO

SIASA

» »Unlabelled » ASKARI WAFUKUZWA KAZI KWA KUKUTWA NA JINO LA TEMBO


 JESHI la Polisi limewafukuza kazi askari wawili wa Kituo cha Polisi cha Mugumu mkoani Mara, baada ya kukamatwa na jino moja la tembo lenye uzito wa kilo 3.5. Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mara, Ferdinand Mtui, aliwataja askari hao kuwa ni D/CPL Isack (43) mwenye namba E.9069 na D/C Sixbert Amos (25) mwenye namba F.5580 kwa kushirikiana na John Sogita maarufu Masese ambaye ni mkazi wa eneo la Bomani mjini Mugumu, walipatikana na nyara hiyo katika eneo la Kisima cha Mafuta cha EAFCO kilichopo wilayani Serengeti.

Alisema askari hao walikamatwa Oktoba 25, mwaka huu, saa nne usiku na askari wa wanyamapori wakitumia Toyota Caldina lenye namba za usajili T 269 BRN mali ya askari Amos.

Alisema kukamatwa kwa jino hilo kumetokana na operesheni okoa maliasili, iliyoendeshwa na askari hao na chanzo cha kukamatwa kwa watuhumiwa hao ni harakati za kutafuta mteja wa kulinunua.

Alisema askari hao wameshitakiwa kijeshi na wamefukuzwa kazi Novemba 7, mwaka huu na wanatarajiwa kufikishwa mahakamani wakati wowote.

RAI

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments: