HABARI

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

MATUKIO

MICHEZO

SIASA

» »Unlabelled » THE TANZANITE WAREJEA BAADA YA KUWAFUNGA MSUMBIJI BAO 5- 1

Baadhi ya wachezaji wa timu ya taifa ya wanawake chini ya umri wa miaka 20 ‘The Tanzanite’ wakiwasili jana kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam, wakitokea Msumbiji katika mechi ya marudiano ya kufuzu fainali za Dunia za wanawake ambako Tanzanite iliichapa Msumbiji mabao 5-1. 


 Kaimu Katibu Mkuu wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Boniface Wambura akipeana mkono na wachezaji wa Tanzanite mara baada ya timu hiyo kuwasili jijini Dar es Salaam ikitokea Msumbiji.

 ENDELEA KUTIZAMA TUKIO HILI KWA KUBOFYA HAPA CHINI


 Wachezaji The Tanzanite wakiwapungia mikono mashabi waliofika kuwapokea kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam jana, wakitokea Msumbiji.
 Nahodha wa The Tanzanite, Fatuma Issa akizungumza na waandishi wa habari.
 Hapa ilikuwa ni furaha baada ya ndugu kukutana
 Kocha Mkuu wa The Tanzanite, Rogasin Kaijage akizungumza na vyombo vya habari baada ya kuwasili nchini
 Mchezaji wa The Tanzanite, Anastazia Anthony akiwa na kaka yake Nickodem Anthony baada ya kuwasili nchini wakitokwa Msumbiji

 Kaimu Katibu Mkuu wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Boniface Wambura akizungumza na vyombo vya habari baada ya timu ya Tanzanite kuwasili jijini Dar es Salaam ikitokea Msumbiji.
 Baadhi ya wazazi wakiwa na watoto wao baada ya kuwasili jijini Dar es Salam wakitokea Msumbiji.
 Wachezaji wa timu ya taifa ya wananwake chini ya umri wa miaka 20 'Tanzanite' wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kuwasili kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere wakitokea Msumbiji katika mchezo wa kufuzu fainali za kombe la Dunia la wanawake dhidi ya Msumbiji, ambako Tanzania ilishinda 5-1.
 Baadhi ya wachezaji wa timu ya taifa ya wanawake chini ya umri wa miaka 20 ‘The Tanzanite’ wakipanda basi baada ya kuwasili leo kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam, wakitokea Msumbiji.

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments: