NANE (8) MBARONI KWA MAKOSA MBALIMBALI YA UHALIFU MKOANI DODOMA.

 Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi DAVID MISIME - SACP

Na: Sylvester Onesmo wa Jeshi la Polisi Dodoma
Jeshi la Polisi Mkoa wa Dodoma linawashikilia watu nane kwa makosa mbalimbali ya uhalifu kufuatia msako uliofanyika tarehe 01/04/2014 maeneo mbalimbali ya Mkoa wa Dodoma.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi DAVID MISIME - SACP amesema tukio la kwanza alikamatwa SIMON S/O MTUNDU, miaka 51, Kabila Mhehe, mkulima na mkazi wa kijiji cha Kisisi Kata ya Kimagiyi Tarafa na Wilaya ya Mpwapwa, akimiliki silaha aina ya Gobore lenye Namba MP. 00202182 kinyume cha sheria za umiliki wa silaha.

Kamanda MISIME amesema tukio jingine alikamatwa CHISEMI S/O ROBERT, miaka 34, kabila Mgogo, mkazi wa kijiji cha Kiboriani Wilaya ya Mpwapwa na wenzake wawili wakimiliki shamba la bhangi ekari moja na nusu (1.5) kinyume cha sheria. Shamba hilo limefyekwa na kuteketezwa kwa moto. 

ENDELEA KUSOMA HABARI HII KWA KUBOFYA HAPA CHINI


Aidha katika Wilaya ya Chemba Mkoani humo alikamatwa MUSSA S/O ALLY MADEBE, mwenye miaka 20, mkulima wa Kijiji na Kata ya Songolo Tarafa ya Goima na wenzake watatu wakiwa na misokoto nane ya Bhangi,  watuhumiwa watafikishwa mahakamani mara upelelezi utakapokamilika na msako bado unaendelea.

Kamanda MISIME amewashukuru wananchi hawa wanaoshirikiana na Jeshi la Polisi kwa kutoa taarifa na kushirikiana na Polisi katika misako.

No comments

Powered by Blogger.