Ndugu wasomaji wetu tunaomba support yenu kwa kutangaza nasi hapa kwenye hii blog kwa bei nafuu ili tuweze kuendelea kutoa habari bila tatizo lolote. Wasiliana nasi kupitia namba +255713363965 / +255755274953. Tunashukuru kwa ushirikiano wenu.
Baadhi ya vitu walivyokamatwa navyo watu hao wanaopiga Ramli chonganishi ambao wameshikiliwa na jeshi la mkoani Dodoma .
Na. Sylvester Onesmo wa Jeshi la Polisi Dodoma.
Jeshi la Polisi Mkoa wa Dodoma linawashikilia watu saba kwa kosa la kujihusisha na upigaji Ramli chonganishi na imani za ushirikina. Katika msako maalum uliofanyika kuanzia tarehe 09/03/2015 Wilaya ya Chamwino Mkoa wa Dodoma.
Akithibitisha tukio hilo Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi DAVID A. MISIME – SACP aliwataja watu waliokamatwa pamoja na Nyara za Serikali wanazotumia kupiga Ramli chonganishi kuwa ni:
1. Daud Mnyetumbi, Mwenye umri wa miaka 70, mkulima wa Chanhumba – Ilolo, Kata ya Handali, alikamatwa akiwa na Ngozi moja ya fisi, Ngozi moja ya kenge, Kipande cha Mkia wa Twiga, Pembe ya Digidigi na Kioo.
2. Ernest Togoya, mwenye umri wa miaka sabini (70), Mkulima wa Chanhumba kitongiji cha Sasajila, Kata ya Handali. Alikamatwa akiwa na; Ngozi moja ya nyoka aina ya Swila, Jino moja la Ngiri, Pembe ya ng’ombe, vipande viwili vya ngozi ya ngo’ombe (viatu vya ramli na ndoto za kichawi).
ENDELEA KUSOMA HABARI HII KWA KUBOFYA HAPA CHINI
3. Antony Kasuga, Mwenye umri wa miaka arobaini na saba (47), Mkulima wa Chanhumba - Ilolo, Kata ya Handali. Amekamatwa akiwana na; Ngozi moja ya Mbweha, Ngozi tatu za nyoka, mbili za aina ya swira na moja ya Chatu, Mkia wa Fisi, Jino moja la Ngili, Gamba la Kakakuona, Ngozi ya Fungo na vipande viwili vya ngozi ya ng’ombe (viatu vya ramli na ndoto za kichawi).
4. Robarti Talibo, Mwenye umri wa miaka hamsini na nne (54), Mkulima wa Kata ya Handali kijiji cha Malechela. Amekamatwa akiwa na Ngozi moja ya Mbweha, Mkia wa Ng’ombe na Vioo viwili.
5. Malima Matungwe, Mwenye umri wa miaka sitini na mbili (62), Mkulima wa Kata ya Mvumi kijijij cha Malechela. Amekamatwa akiwa na Ngozi ya Nyoka aina ya Swira mbili, Ngozi ya Kenge na Mkia wa Nyumbu.
6. Mtemi Sumile, Mwenye umri wa miaka sabini na tano (75), Mkulima wa Kata ya Mvumi Mission kijiji cha Chihembe. Amekamatwa aikiwa na; Vipande vya ngozi ya ng’ombe (viatu vya ramli na ndoto za kichawi) pamoja na Kioo kimoja.
7. Lusinde Mchete, Mwenye umri wa miaka tisini (90), Mkulima wa Kata ya Mvumi Mission Kitongoji cha Jamhuri. Amekamatwa akiwa na; Mwiko wa kupigia ramli, Pembe la Ng’ombe na vipande viwili vya ngozi ya ngombe vya ramli na ndoto za kichawi.
Kamanda MISIME amesema uchunguzi zaidi unaendelea na Watuhumiwa watafikishwa Mahakamani mara utakapokamilika kwa makosa ya Kupatikana na nyara za Serikali na Kijihusisha na upigaji ramli chonganishi.
Aidha Kamanda MISIME ametoa wito kwa wananchi kuondokana na tabia ya baadhi ya watu kujihusisha na imani za kishirikina na kupiga ramli kwani ndizo baade hupelekea watu wenye ualbino kuuawa na kukatwa viungo; Pia vikongwa kuuawa kwa imani kwaba wanazuia mvua isinyeshe au wanaloga watu.
Kila mmoja atambue kuwa unachomfanyia mwingine kwa imani potofu za kiushirikina na kiuchonganishi kinaweza kesho au kwa siku za baadae kikakupata wewe au mtu wa familia yako; Tunatakiwa wote kuanzia ngazi ya familia kupeana elimu na kupiga vita mabo hayo.
No comments:
Post a Comment