PROF.LIPUMBA ALAANI WATU WAWILI KUJERUHIWA NA VIJANA WALIO FICHA SURA ZAO MAKUNDUCHI ZANZIBAR.

Ndugu wasomaji wetu tunaomba support yenu kwa kutangaza nasi hapa kwenye hii blog kwa bei nafuu ili tuweze kuendelea kutoa habari bila tatizo lolote. Wasiliana nasi kupitia namba +255713363965 / +255755274953. Tunashukuru kwa ushirikiano wenu.

Picha kutoka Maktaba

Kufuatia watu wawili waliojeruhiwa na watu waliokuwa wamejigunika nyuso zao huko katika mtaa wa Makunduchi Zanzibar waliokuwa wakienda kujiandikisha katika daftari la wapiga kura, mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF) Mhe Prof.Ibrahimu Lipumba ametoa tamko la kulaani kitendo hicho.
Akiwahutubia wananchi katika viwanja vya sabasaba wilayani Buhigwe mkoani kigoma mwenyekiti huyo Mhe.Lipumba amesema kitendo hicho si cha kuvunilia. 
 
Aidha Mhe.Lipumba amemtaka rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania kama amiri jeshi mkuu kuhakikisha amani na usalama vinaendelea kuwepo wakati tukielekea katika uchaguzi mkuu ujao.

No comments

Powered by Blogger.