HABARI

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

MATUKIO

MICHEZO

SIASA

» »Unlabelled » MADUKA YA UCHUMI SUPERMARKET YAFUNGWA NCHINI TANZANIA NA UGANDA

Ndugu wasomaji wetu tunaomba support yenu kwa kutangaza nasi hapa kwenye hii blog kwa bei nafuu ili tuweze kuendelea kutoa habari bila tatizo lolote. Wasiliana nasi kupitia namba +255713363965 / +255755274953. Tunashukuru kwa ushirikiano wenu.



Uongozi wa Uchumi Supermarket umetangaza kufunga shughuli zake katika maduka yake yaliyopo Tanzania na Uganda ili kutoa nafasi ya kuzuia mtikisiko wa kifedha unaoikumba kampuni hiyo.
Ofisa Mtendaji Mkuu wa Uchumi, Dk Julius Kipng'etich, amesema Bodi imeamua kufunga vitengo vya kikanda ili kuimarisha shughuli zake nchini Kenya baada ya kupata hasara katika maduka yake ya Uganda na Tanzania.
"Maduka yetu ya Uganda na Tanzania huchangia asilimia 25 tu ya gharama za uendeshaji. Matawi hayo mawili hayajapata faida yoyote kwa zaidi ya miaka mitano iliyopita jambo linaloyumbisha shughuli zetu," amesema Dk Julius
"Tuna uhakika kwamba tunaweza kuigeuza Uchumi kwa kulenga asilimia 95 ya biashara ambazo zinaleta fedha kwa wanahisa ambao wana matumaini kwamba tutafanikisha hili ndani ya muda mfupi," ameongeza Dk Kipng'etich.
Kwa upande wa Tanzania, juzi wafanyakazi zaidi ya 400 waligoma kwa kujifungia ndani ya ofisi zao kwa zaidi ya saa 20 wakitaka kujua hatma yao kwenye makao makuu ya duka hilo yaliyopo katika jengo la Quality Center jijini Dar es salaam.
Wafanyakazi hao walikubaliana na uongozi wa Uchumi Supermarket kuwa leo wangeendelea na majukumu yao kama kawaida huku wakisubiri hatma yao siku ya Ijumaa lakini walikuta ofisi zimefungwa bila ya kupewa taarifa yoyote rasmi.

Chanzo:  Mwananchi.

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments: