HABARI

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

MATUKIO

MICHEZO

SIASA

» »Unlabelled » UPDATES: ABIRIA 30 WANUSURIKA KATIKA AJALI YA KUZAMA KWA KIVUKO CHA MTO KILOMBERO

Ndugu wasomaji wetu tunaomba support yenu kwa kutangaza nasi hapa kwenye hii blog kwa bei nafuu ili tuweze kuendelea kutoa habari bila tatizo lolote. Wasiliana nasi kupitia namba +255713363965 / +255755274953. Tunashukuru kwa ushirikiano wenu.


Taarifa zilizotufikia zinasema kuwa Kivuko cha mto Kilombero mkoani Morogoro kimezama kikiwa na abiria zaidi ya 30 na magari 3. 
Mkuu wa wilaya ya Kilombero Bw Leph Gembe amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo na kusema kuwa, kuzama kwa kivuko hicho kulichangiwa na upepo mkali uliokuwa ukivuma wakati huo hivyo kupoteza uelekeo wake. 
Alisema ajali hiyo imetokea jana Majira ya saa 1 usiku wakati kivuko hicho kikitokea Ulanga. 
Mkuu huyo wa wilaya amesema taarifa alizopewa ni kwamba kivuko hicho kilikuwa na abiria 30 na wote waliokolewa baada ya kupewa majaketi ya usalama baada kivuko hicho kuanza kupoteza uelekeo kutokana na upepo mkali. 
Hata hivyo amesema kuna mashaka ya mtu mmoja kuwa alizama na wanaendelea kufuatilia kupata ukweli wake. 
Ameyataja magari yaliyozama kuwa ni pamoja na gari moja la CRDB, gari la kampuni ya mitiki, fuso moja pamoja na bajaji.
Muonekano wa Misingi ya Daraja la Mto huo, huku kivuko kilichozama kikionekana kulia.

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments: