HABARI

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

MATUKIO

MICHEZO

SIASA

» » IDADI YA VIFO TETEMEKO LA ARDHI NCHINI ITALIA YAONGEZEKA HADI WATU 247

Ndugu wasomaji wetu tunaomba support yenu kwa kutangaza nasi hapa kwenye hii blog kwa bei nafuu ili tuweze kuendelea kutoa habari bila tatizo lolote. Wasiliana nasi kupitia namba +255713363965 / +255755274953. Tunashukuru kwa ushirikiano wenu.


 Idadi ya watu waliofariki kwenye tetemeko la ardhi lililotokea nchini Italia Jumatano hii imeongezeka na kufikia watu 247.
 Tetemeko hilo linalokadiriwa kuwa na nguvu ya 6.2 katika vipimo vya Ritcher limesababisha madhara makubwa kwenye miji ya Umbria, Amatrice, Accumoli na Pescara del Tronto kwa watu kufukiwa kwenye vifusi.
 Wakati maafisa wa uokoaji wakiendelea na juhudi za kuwaokoa watu walionusurika kwenye tukio hilo walitatizwa na mitetemeko mingine iliyotokea ghafla na kutikisa majumba yaliyosalia yakiwa bado wima.
Maeneo yaliyokumbwa zaidi na uharibifu huo ni Accumoli na Pescara del Tronto huku tetemeko hilo likitajwa kuanzia kwenye Norcia, kilomita 170 kaskazini magharibi mwa mji mkuu Roma.

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments: