HABARI

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

MATUKIO

MICHEZO

SIASA

» » » NAJUTA KUMSALITI MUME WANGU SEHEMU YA SITINI NA MOJA(61)

Ndugu wasomaji wetu tunaomba support yenu kwa kutangaza nasi hapa kwenye hii blog kwa bei nafuu ili tuweze kuendelea kutoa habari bila tatizo lolote. Wasiliana nasi kupitia namba +255713363965 / +255755274953. Tunashukuru kwa ushirikiano wenu.



Baada ya wiki moja kupita taarifa zilimfikia Peter kuwa Jackline alikuwa akiishi peke yake na ana mtoto mdogo. Mbali na hayo mdaku huyo alitoa taarifa kuwa Jackline hakuwahi kuonekana na mwanaume yoyote isipokuwa mwanamke ambaye alimtambua kama dada yake ambaye hufika mara chache tu na kuondoka.
Kwa mdaku aliyemtuma kumchunguza Tinonko, alikuwa na taarifa kuwa bado Tinonko alikuwa ni tajiri sana huko Morogoro lakini alikuwa akijificha na kutotaka kujulikana. Pia mbali na hayo, cha muhimu kilikuwa ni kwamba Tinonko naye hakuwahi kuonekana na mwanamke yoyote zaidi alikuwa akiishi peke yake tu.
Hilo likamfurahisha Peter akajua kwa vyovyote Tinonko kama angeachana na Jackline, lazima angekuwa na mwingine mpaka sasa kwa kuwa ilikuwa imepita takribani miezi tisa, hivyo suala la yeye kubakia peke yake ilikuwa inamaanisha kuwa bado anampenda Jackline.
Peter akaona lazima autumie udhaifu huo ili kujipatia fedha tena kwa kuwa Jackline ana mtoto wa Tinonko, hiyo ilikuwa nzuri kwa upande wake. Peter akacheka na kuanza kupanga mikakati ya kuwateka Jackline na mwanaye.

UKITAKA KUSOMA STORY YA LEO ILIYOKAMILIKA NITAFUTE WHATSAPP KWA NAMBA HII 0713363965 UTATUMIWA.

ITAENDELEA JUMAPILI

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments: