HABARI

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

MATUKIO

MICHEZO

SIASA

SPIKA WA BUNGE ATEMBELEWA NA MCHUNGAJI ANTHONY LUSEKELO LEO MJINI DODOMA.

 Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (kushoto) akisalimiana na Mchungaji Anthony Lusekelo (kulia) alipomtembelea leo katika ukumbi wa Spika Mjini Dodoma.
 Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (katikati) akizungumza jambo wakati alipotembelewa na ugeni kutoka Kanisa la Maombezi (GRC) ulioongozwa na Mchungaji Anthony Lusekelo (wa pili kulia) katika kikao kilichofanyika leo katika ukumbi wa Spika Mjini Dodoma.
 Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (wa pili kulia) akimsikiliza Mchungaji Anthony Lusekelo (kulia) kutoka Kanisa la Maombezi (GRC) pale alipomtembelea leo katika ukumbi wa Spika Mjini Dodoma.
Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (wa pili kushoto)akimsikiliza Mbunge wa Viti Maalum, Mheshimiwa Anna Lupembe (aliesimama)akizungumza jambo pale ugeni kutoka kanisa la Maombezi (GRC)ukiongozwa na Mchungaji, Anthony Lusekelo (wa pili kulia)ulipomtembelea leo katika ukumbi wa Spika Mjini Dodoma.
(PICHA NA OFISI YA BUNGE)
 Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (katikati) akipiga picha ya pamoja na ugeni kutoka Kanisa la Maombezi (GRC) ukiongozwa na Mchungaji Anthony Lusekelo (wa tatu kulia) baada ya kikao kilichofanyika leo katika ukumbi wa Spika Mjini Dodoma.

MZEE WA UPAKO AFUNGUKA KUHUSU SAKATA LA KUWATUKANA MAJIRANI ZAKE

Ndugu wasomaji wetu tunaomba support yenu kwa kutangaza nasi hapa kwenye hii blog kwa bei nafuu ili tuweze kuendelea kutoa habari bila tatizo lolote. Wasiliana nasi kupitia namba +255713363965 / +255755274953. Tunashukuru kwa ushirikiano wenu.


Siku tatu baada ya kudaiwa kumfanyia fujo jirani yake, Mchungaji wa Kanisa la Maombezi (GRC), Anthony Lusekelo maarufu Mzee wa Upako, amejibu tuhuma hizo akisema anaishi kana kwamba hana jirani.“...Tunaishi kama majambazi tu, hujui jirani yako ni nani,” amesema.

Lusekelo amesema Yesu ambaye ni  mwana wa Mungu alikubali kudhalilishwa na baadaye kufa bila hatia hivyo na yeye alikubali kula kiapo katika nafasi ya utumishi wake.

Amesema magazeti wa  mitandao ya kijamii hayawezi kumshusha kwa kuwa hayakumpasha ila Mungu pekee.

Katika mahubiri yake yaliyohudhuriwa na waumini wengi kama ilivyo kwa Jumapili nyingine za karibuni kanisani kwake, Ubungo Kibangu, mchungaji huyo aliingia kwa mapokezi ya wimbo wa kuabudu uitwao ‘Angalia Bwana’ kabla ya waumini kuanza kumtunza kwa sadaka kama ilivyo kawaida ya ibada zake.

Katika mahubiri hayo alisema haiogopi jela, bali anaogopa kuvunja sheria za nchi na wala alipokamatwa na Polisi haikumtisha wala kumvunja moyo, kwani viongozi wa dini wamekula kiapo hadi kufa. 


Aidha, alisema wapo waliosema kuwa Mzee wa Upako alikuwa anatukana, alidai kuwa matusi yake yote ni maandiko na anayetaka ufafanuzi wowote akipata nafasi amuulize yameandikwa katika vitabu gani li apate kuelewa.


Alisema mpumbavu sio tusi hayo ni maelezo na Yesu alitukanwa sana, na hata ushenzi si tusi lina maana pana ya kwamba huna hofu ya Mungu, mjinga ana dhambi ya mauti, inayomsubiri kwenda peponi.

Hata hivyo, aliwausia waumini wa kanisa hilo kuwa kamwe wasimtukane mtu kwa umbo ama rangi yake kwa kuwa hakupenda kuzaliwa hivyo na waishi hivyo kwa kutenda mema kwa kuwa ufalme wa Mungu watauona.

Alisema tangu kutokea kwa tukio amekuwa akipigiwa simu na watu ambao hakuwategemea huku waandishi wakimtaka kuzungumzia chochote wakiwamo waandishi wa habari ambao alisema walikuwamo ndani ya kanisa hilo jana.

Akifafanua kilichotokea siku hiyo, alieleza kuwa alitoka saa 11 alifajiri bila kufafanua alikuwa akitokea wapi, ndipo alipokutana na watu wawili akiwemo Mmasai na dada mmoja alipowauliza wanatokea wapi katika eneo hilo ambalo wakazi wengi wa huko hutoka na magari yao, ndipo ugomvi ulipoanzia.

“Hawa watu wa magazeti wanataka kuuza magazeti, barabara hiyo nimeijenga mimi hivyo nilikuwa na haki ya kuwauliza maana ni kibarabara... washenzi wakubwa wanaandika tu, halafu wanasema nimewatukana majirani kule hakuna jirani hajui wanaingia saa ngapi na wanatoka saa ngapi na hakuna hata habari za asubuhi. Kila mmoja anatumia gari lake,” alieleza Mzee wa Upako.

“Kwanza waliandika habari kwamba waumini hawatakuja kanisani badala yake wamejitokeza bila kukatishwa tamaa. Wakati mnajitokeza hapa mbele (kutoa sadaka), alipita mama mmoja amebeba mtoto, nilimwombea mwaka jana hapa kwamba atapata mtoto na leo amepata mtoto, sasa mbona magazeti yasiandike habari hizo?”

“Kwa nini wasiandike hayo mazuri ‘front page’ (ukurasa wa mbele)?, halafu mnaandika Mzee wa Upako matatani, matatani babu yako.”

“Najua na leo mmekuja mpo humu mnasubiri niseme, nasubiri mmalize kwanza nyinyi halafu na mimi ndiyo nitasema, baada ya mwezi mmoja najua mtakuwa mmemaliza,”alisema.

MCHUNGAJI ANTHONY LUSEKELO (MZEE WA UPAKO) ANADAIWA KUMFANYIA FUJO JIRANI YAKE HUKU AKIWA AMELEWA

Ndugu wasomaji wetu tunaomba support yenu kwa kutangaza nasi hapa kwenye hii blog kwa bei nafuu ili tuweze kuendelea kutoa habari bila tatizo lolote. Wasiliana nasi kupitia namba +255713363965 / +255755274953. Tunashukuru kwa ushirikiano wenu.


Mtu huyo anayedaiwa kuwa Mzee wa Upako, anaonekana amevalia shati la rangi ya bluu na suruali nyeusi, anasikika akimfokea mtu aliye ndani na kumuonya asikutane naye.
Katabazi aliithibitishia Mwananchi kuwa taarifa hiyo iliyosambaa kuhusu Mzee wa Upako ni yake na kwamba alimkuta mchungaji huyo asubuhi eneo la Kawe Beach anakoishi akiwa anawatolea maneno makali watu waliokuwa ndani ya uzio wa nyumba, akidai kuwa wanamdharau.
Alisema kwa mujibu wa watu saba aliowakuta kwenye eneo la tukio, mchungaji huyo alikuwa akirejea nyumbani kwake asubuhi hiyo akionekana kutokuwa katika hali ya kawaida.
Lakini kabla ya kufika nyumbani alisimamisha gari lake mbele ya geti la nyumba ya jirani yake na kuanza kuwatolea maneno hayo kwa madai kuwa wamekuwa wakimkebehi yeye kuwa hafai kuwa mchungaji kwa sababu ni mlevi.
“Nilimsihi sana hadi saa moja asubuhi nikimwomba anisikilize, aache kutukana, kutoka katika eneo la nyumba ya watu kwa sababu yeye ni mtumishi wa Mungu anajidhalilisha ,” alisema Katabazi.
Katabazi alisema mchungaji huyo hakumsikiliza.
Katabazi, ambaye alidai kuwa wakati huo Mzee wa Upako hakuonekana kuwa katika hali nzuri, alikubali kwenda nyumbani.
Hata hivyo, Katabazi alisema baada ya muda mfupi Mzee wa Upako alirudi kwenye nyumba hiyo na kuanza tena kutoa maneno hayo.
Katabazi alisema kwa kuwa kulikuwa kumeshapambazuka taarifa zilianza kusambaa, askari wa kituo cha polisi cha Kawe walifika eneo hilo na kumchukua.
Lakini Kamanda wa Polisi wa Kinondoni, Suzan Kaganda alisema hana taarifa za kukamatwa kwa Mzee wa Upako.
Wakati taarifa zinadai kuwa baadaye alichukuliwa na askari wa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Kamanda Simon Sirro hakutaka kuzungumzia suala hilo na kuahidi kutoa taarifa ya tukio hilo leo.
Mlinzi wa nyumba ambayo Mchungaji Lusekelo alikutwa akitoa maneno hayo alithibitisha kutokea kwa tukio hilo, akisema alifika asubuhi majira ya saa 11:00 na kuegesha gari barabarani kisha kuanza kufoka.
Baada ya kufoka mtu mmoja alitoka na kumuita kwa kutumia cheo cha mchungaji, lakini alijibiwa “mchungaji hukohuko”, na kuendelea kufoka, jambo lililofanya walinzi kupiga simu polisi.
Alisema polisi walifika muda mfupi baadaye na kutaka kujua sababu za mchungaji huyo kuitaarifu polisi kama ana matatizo na jirani yake, lakini akawa anatoa maelezo ambayo walishindwa kuyaelewa na hivyo kuondoka naye.

Mke wa mchungaji huyo, Happiness Ngasala aliiambia Mwananchi kuwa mchungaji huyo alikuwa nyumbani kwake.
“Mume wangu yupo nyumbani hapa. Hizo taarifa hazina ukweli wowote,” alisema.
Kuhusu madai ya kutoa maneno nayo, Ngasala alisema: “Hata huo waraka si wa kweli. Mchungaji hawezi kutoa maneno kama hayo.”
Ngasala, ambaye alithibitisha kwamba mume wake yupo nyumbani alipoombwa ampe Mzee wa Upako simu ili mwandishi azungume naye, alisema apigiwe kwenye simu yake.
Mwandishi alipomwambia kwamba mchungaji huyo amepigiwa simu yake lakini hajapokea, alisema mume wake hajakamatwa na kwamba kuna kinyozi alifika kwa ajili ya kumnyoa nywele, hivyo apigiwe baadaye.

CHANZO: MWANANCHI

MCHUNGAJI ANTHONY LUSEKELO ANENA MAZITO KUHUSU LOWASSA NA CCM

Ndugu wasomaji wetu tunaomba support yenu kwa kutangaza nasi hapa kwenye hii blog kwa bei nafuu ili tuweze kuendelea kutoa habari bila tatizo lolote. Wasiliana nasi kupitia namba +255713363965 / +255755274953. Tunashukuru kwa ushirikiano wenu.


Mchungaji wa Kanisa la Maombezi (GRC) la Ubungo jijini Dar es Salaam, Anthony Lusekelo maarufu ‘Mzee wa Upako’ amesema kitendo cha viongozi wa CCM kulitaja zaidi jina la Edward Lowassa katika Mkutano Mkuu Maalumu wa chama hicho ni ishara kuwa Waziri Mkuu huyo wa zamani ni tishio.

“Nani! Lowassa…. jina lake kutajwa sana katika vikao vya CCM. Hiyo inaashiria kuwa ni mtu tishio. Ndiyo ni tishio,” alisema Lusekelo jana katika mkutano wake na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam

Lusekelo ambaye hivi karibuni, Rais John Magufuli alishiriki ibada katika kanisa lake, alimzungumzia Lowassa baada ya kuulizwa swali juu ya mtazamo wake kuhusu Mkutano Maalumu wa CCM ambao jina la mgombea huyo wa urais kupitia Chadema na Ukawa lilitajwa na makada wengi wa chama hicho tawala. 

Alisema hilo lilidhihirika hata katika mchakato wa CCM kupata mgombea wake wa urais, kutokana na Lowassa kuungwa mkono kwa kiasi kikubwa. 

Alisema kitendo cha Waziri Mkuu huyo wa zamani kuzua mjadala katika Mkutano Mkuu wa chama hicho tawala sambamba na wimbi la makada wanaohama vyama vyao, si mambo yanayopaswa kuwa mjadala kwa sababu uchaguzi ulishapita. 

Huku akisema: “Sizungumzi haya kwa ajili ya kujipendekeza, sihitaji ukuu wa wilaya,” Lusekelo aliwataka viongozi kukataa kuendeleza uhasama wa kisiasa na chuki kwa maelezo kuwa mwaka huu uwe maalumu kuzika tofauti hizo, kufanya kazi kulijenga Taifa na kuhubiri amani na umoja. 

Katika mkutano huo, Lusekelo alipongeza kuimarika kwa vyama vya upinzani akaponda mvutano ulioibuka bungeni akisema kukosa uzoefu kwa Naibu Spika, Dk Tulia Ackson kulichangia huku akiunga mkono kauli ya Rais kuzuia shughuli za siasa na kubainisha jinsi Rasimu ya Katiba ya Tume ya Jaji Joseph Warioba, ilivyopendekeza kupunguzwa kwa madaraka ya Rais. 

Jumamosi iliyopita, katika Mkutano Mkuu wa CCM mjini Dodoma, uliomalizika kwa Rais Magufuli kuchaguliwa kuwa mwenyekiti, mzimu wa Lowassa ulitawala kutokana na kila aliyepewa nafasi ya kuzungumza ama kumtaja kwa jina au kwa mafumbo. 

Mwenyekiti wa CCM aliyemaliza muda wake, Jakaya Kikwete ndiye aliyeanza kuzungumzia hali ya mchakato wa chama hicho kupata mgombea wake wa urais, kuwa ulikuwa mgumu na majaribu makubwa na kwamba wazee walifanya kazi kunusuru hali hiyo.

Katika mchakato huo, CCM ilikata jina la Lowassa katika hatua za awali, jambo lililosababisha kiongozi huyo kuhama na kundi la wanaCCM na kujiunga na Chadema ambayo ilimteua kuwa mgombea wake wa urais. 

Hata hivyo, katika mkutano wake wa jana, Lusekelo alisema katika mchakato wa chama hicho tawala kupata mgombea wake wa urais kulikuwa na watu wenye majina makubwa, akiwamo Lowassa na aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Nje, Bernard Membe. 

“Niliwaambia CCM, Membe huwezi kumpuuza, Lowassa naye huwezi kumpuuza maana wanataka madaraka na kwa vyovyote lazima mtapata mtikisiko. Nikawaomba waahirishe suala la kupata Katiba Mpya maana wasingelimaliza na muda ulikuwa mfupi,” alisema na kuongeza: “Kama mwaka huu hautatumika kutibu majeraha yaliyotokea huko nyuma, tutaharibikiwa sana.” 

Alisema mchakato wowote wa uchaguzi na kura ya maoni ndani ya vyama huacha mpasuko na watu hutumia dini na ukabila kubaguana, hivyo lazima baada ya uchaguzi mambo hayo yamalizwe. 

“Tunapaswa kukumbuka kuwa wote ni Watanzania tusahau uchaguzi. Sasa ni wakati wa kuijenga nchi. Amani inatengenezwa, na Mungu huwapa hekima maana kujenga ni kazi na kubomoa ni rahisi, huu ni mwaka wa uponyaji na kurejesha Taifa pamoja,” alisema Lusekelo. 

Alisema kuanza kubagua watu kwa sababu walitoka CCM kwenda Chadema au kutoka Chadema kwenda chama tawala si jambo sahihi huku akitolea mfano mataifa yaliyovurugika kwa kuendekeza siasa za chuki na uhasama. 

Yaliyotokea bungeni 
Akizungumza yaliyotokea bungeni na kusababisha wabunge wa Ukawa kususia vikao vya Bunge vilivyoongozwa na Dk Tulia, Lusekelo alisema Mtanzania anayejua historia ya nchi yake hawezi kufumbia macho suala hilo. 

“Binafsi nawalaumu waliotoka (wabunge wa upinzani) na waliobaki (wabunge wa CCM). Kushindana si kuzuri. Mbatia (James Mbunge wa Vunjo na Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi) na wenzake wanapaswa kujua kuwa naibu spika ni mchanga katika siasa waende naye taratibu maana kapewa ubunge tu na kuwa naibu spika,” alisema. 

Huku akiponda uamuzi wa Serikali kufuta urushwaji wa matangazo ya moja kwa moja ya Bunge alisema: “Nashangaa wazee kama Salim (Ahmed Salim – Waziri Mkuu mstaafu), Pinda (Mizengo – Waziri Mkuu mstaafu) na Warioba. Sijui walishindwa nini kukaa na wabunge hawa ili kumaliza tofauti zao.”

Alisema si jambo jema kuongoza nchi kwa mabavu na kusisitiza kuwa hata uhuru ulipatikana kwa mazungumzo. 

Mchungaji huyo aliusifu utawala wa Rais Magufuli kuwa una kasi kubwa na kwamba licha ya wananchi kulia ukata, watacheka baada ya mwaka mmoja huku akiwananga wanaomponda Kikwete kuwa hawajui mazuri aliyoyafanya. 

Awapongeza wapinzani 
Akizungumzia nguvu ya vyama vya upinzani, Lusekelo alisema ushindani wa kisiasa umekuwa mkubwa kutokana na kuimarika kwa upinzani: “Chadema ya sasa si ile ya miaka ya 1990. Wanaongoza miji mikubwa na ukiona chama kina wabunge 40 usikipuuze. Hata nguvu ya mfalme ni watu.” 

Mikutano ya siasa
Kuhusu kauli ya Rais kusitisha shughuli za siasa hadi mwaka 2020, alisema jambo hilo linaweza kuonekana baya lakini lina unafuu mkubwa, kwamba Kenya wamelifanya na kufanikiwa kumaliza tofauti za kisiasa. 

“Hivi watu 10,000 wakiandamana na kusema Magufuli aliiba kura itakuwaje? Tuna askari wa kuwazuia! Nadhani wanasiasa wafanye kazi ya utawala katika vyama vyao. Tutulie kwanza tutibu majeraha. Hakuna jambo baya kama kuwaongoza watu wenye njaa maana hawana la kupoteza,” alisema. 

Hata hivyo, Lusekelo alisema Rasimu ya Katiba ilipendekeza Rais kupunguziwa madaraka na huenda madaraka makubwa aliyonayo Rais yakawa sababu ya nchi kuendelea kuwa na amani. 

“Kenya kuzuia maandamano ni ngumu sana lakini hapa kwetu hadi Zitto (Kabwe-Kiongozi wa ACT-Wazalendo) alizuiwa kufanya mkutano wa ndani. Kwetu rais ana madaraka makubwa sana,” alisema huku akiwataka polisi kutekeleza wajibu wao vyema, wakikumbuka kuwa nao ni binadamu.