HABARI

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

MATUKIO

MICHEZO

SIASA

WABUNGE WA VITI MAALUMU CCM MKOA WA DAR, WAFANYA ZIARA KUHAMASISHA WANACHAMA NA KUIMARISHA UHAI WA CHAMA

Kiongozi wa Wabunge wa Viti Maalumu, Mkoa wa Dar es Salaam, na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Angela kairuki, akizungumza na Viongozi na Wanachama wa UWT (CCM) wakati wa ziara ya wabunge hao katika Wilaya ya Kinondoni kwa lengo la kuhamasisha wanachama juu ya uchaguzi wa Jumuiya hiyo na Uhai wa Chama. Mkutano huo ulifanyika leo mchana kwenye Ukumbi wa Ndugumbi uliopo Magomeni Barafu jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Mbunge wa Viti Maalum CCM, Ikupa Alex. Picha Zote na Muhidin Sufiani (MAFOTO) 
Baadhi ya Wanachama wa CCM Kina mama wakifurahia moja ya kauli ya mgeni rasmi.
Wanachama wakimsikiliza kwa makini mgeni rasmi wakati wa mkutano huo.
Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Kinondoni, Masunga, akizungumza machache kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi kuhutubia.
Wanachama wa CCM wakifurahi na kucheza na mgeni rasmi
Wanachama wa CCM wakifurahi na kucheza na mgeni rasmi
Wanachama wa CCM wakifurahi na kucheza na mgeni rasmi
Ilikuwa ni furaha kwenda mbele.
Wanachama wakishangilia
Mgeni rsmi Angela Kairuki akiagana na wanachama waliokuwepo ukumbini humo baada ya kumaliza mkutano huo.
Kiongozi wa Wabunge wa Viti Maalumu, Mkoa wa Dar es Salaam, na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Angela kairuki, akizungumza jambo na mmoja wa wanachama aliyekuwa akimueleza baadhi ya Kero za mtaani kwake baada ya kumaliza kuwahutubia Viongozi na Wanachama wa UWT (CCM) wakati wa ziara ya wabunge hao katika Wilaya ya Kinondoni kwa lengo la kuhamasisha wanachama juu ya uchaguzi wa Jumuiya hiyo na Uhai wa Chama katika mkutano uliofanyika leo mchana kwenye Ukumbi wa Ndugumbi uliopo Magomeni Barafu jijini Dar es Salaam.
Mgeni rsmi Angela Kairuki akiagana na wanachama waliokuwepo ukumbini humo baada ya kumaliza mkutano huo.

BULEMBO AFUNGA KAZI WILAYA YA MISENYI NA BUKOBA MJINI MKOANI KAGERA

 Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM, Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Tanzania Alhaj Abdallah Bulembo akiwasili ukumbini kuendesha kikao cha Wajumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Wilaya ya Misenyi, Mabalozi, viongozi wa Jumuia za CCM na watendaji wa Serikali katika Wilaya hiyo mkoani Kagera, leo
Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Alhaj Abdallah Bulembo akisaini kitabu cha wageni baada ya kuwaili ukumbini
                         Wajumbe wakiwa ukumbini tayari kumsikiliza Alhaj Bulembo
Katibu wa Jumuia ya Wazazi Tanzana, Wilaya ya Misenyi Rehema Mtawala akimkabidhi zawadi maalum Mjumbe wa kamati Kuu ya CCM, Mwenyekiti wa Jumuia ya Wazazi Alhaj Abdallah Bulembo kabla ya kikao kuanza
Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM, Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Alhaj Abdallah Bulembo akionyesha zawadi hiyo maalum baada ya kukabidhiwa. Zawadi hiyo ina maneno ya kumpongeza kwa kuteuliwa kuwa Mbunge.
 Mwenyekiti wa CCM wa CCM Wilaya ya Misenyi mkoani Kagera, Haji Seruhu akifungua kikao hicho
 Katibu wa CCM Wilaya ya Misenyi mkoani Kagera Mwajuma Mboha, akieleza maneno ya utangulizi katika kikao hicho

 Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Alhaj Abdallah Bulembo akifurahia jambo na Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Misenyi Haji Seruhu, wakati wanapita taarifa iliyosomwa na Katibu wa CCM wa Wilaya hiyo
 Wajumbe wakihamasika kwenye kikao hicho
Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Alhaj Abdallah Bulembo akisisitiza jambo wakati wa kikao hicho
Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Alhaj Abdallah Bulembo akizungumza na wajumbe wakati wa kikao hicho
 Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Alhaj Abdallah Bulembo akitulia kumsikiliza kwa makini mshairi Mansur Athan wakati akighani shairi mwishoni mwa kikao hicho
Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Alhaj Abdallah Bulembo akipokea zawadi ya Mbuzi aliyopewa na Jumuiya ya Wazazi Wilaya ya Misenyi wakati wa kikao hicho leo.
Mwenyekiti wa UVCCM mkoa wa Kagera Yahya Kateme (kushoto) akibadilishana mawazo na Vijana wa wa CCM nje ya ukumbi baada ya kikao
Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Ajhaj Abdallah Bulembo akiendelea kuwasikiliza nje ya ukumbi badhi ya wadau waliotaka ufafanuzi wa baadhi ya mambo baada ya kikao hicho
 Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM akiwafafanulia jambo nje ya ukumbi baadhi ya wadau
Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Alhaj abdallah Bulembo akiendelea kuwasikiliza wadau hata baada ya kupanda gari lake tayari kwa kuondoka

Baada ya wadau kuridhika wakamuaga kwa furaha na kumtakia safari njema kwenda Wilaya ya Bukoba mjini
 Safari ya Alhaj Bulembo kutoka Misenyi kwenda Wilaya ya Bukoba mjini ilipitia kwenye daraja hili la Mto Kagera, eneo la Kyaka.
 Mwenyekiti wa UVCCM mkoa wa Kagera Yahya Kateme akizungumza na vijana waendesha bodaboda aliowakuta Bukoba Mjini, baada ya msafara wa Alhaj Abdallah Bulembo kuwasili
 Mwenyekiti huyo wa UVCCM akapiga picha ya pamoja na vijana wa green Guard wa Bukoba mjini
 Baada ya kuwasili tu Bukoba Mjini, Mjumbe wa kamati Kuu ya CCM Alhaj Abdallah Bulembo alieanda ofisini kwa Mkuu wa mkoa wa Kagera Meja Jenerali Mstaafu Salim Mustafa Kijuu na kuwa na mazungumzo naye kwa muda. Pichani, wakiwa katika picha ya pamoja baada ya mazungumzo hayo. Wengine kushoto ni Katibu wa CCM mkoa wa Kagera Lahel Ndegeleki na Mwenyekiti wa CCM mkoa huo Costansia Buhiye
Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Alhaj Abdallah Bulembo akimweleza jambo Mkuu huyo wa mkoa kabla ya kuondoka
Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Alhaj Abdallah Bulembo akiwasalimia vijana wa green Guard nje ya Ofisi ya Mkuu wa mkoa.
 Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Alhaj Abdallah Bulembo akimwelekeza jambo Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Bukoba mjini Yusuf Ngaiza wakati wa kikao cha Wajumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM wilaya hiyo, Mabalozi, viongozi wa Jumuiya na Watendaji wa serikali, leo
Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Bukoba Mjini mkoani Kagera Yusuf Ngaiza akifungua kikao hicho
                                                       Wajumbe wakiwa ukumbini katika kikao hicho
Mjumbe wa kamati Kuu ya CCM, Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Alhaj Abdallah Bulembo akizungumza na wajumbe wakati wa kikao hicho Bukoba mjini mkoani Kagera, leo. PICHA; BASHIR NKOROMO

Wahujumu uchumi walitaka kumhonga Rais Magufuli Bilioni 300

Ikiwa imepita siku mbili tangu Rais John Magufuli kueleza kuwa kwa sasa nchi iko katika vita ya uchumi na kwamba ana majina ya watu waliotaka kuingilia na kuharibu uchunguzi wa Kamati Maalumu aliyoiunda ili kuchunguza thamani na viwango vya madini vilivyomo kwenye mchanga wenye madini (Makinikia) katika makontena 277 yaliyozuiliwa kusafirishwa nje ya nchi, ili kupoteza ushahidi. 

Katibu wa Itikadi na Uenezi CCM, Humphrey Polepole Mei 25, 2017 aliibuka na kudai kuwa kuna wahujumu uchumi walitaka kumhonga kiasi cha Bilioni 300 Rais Magufuli, ili kusitisha zoezi la uchunguzi huo, huku akihoji masilahi wanayopata watu wanaofanya biashara ya kusafirisha makinikia hayo nje ya nchi.

“Vita ziko za aina nyingi, ziko zile tunazopigana kwa silaha mtu na mtu, na nchi na nchi, lakini sasa ziko vita za kiuchumi, ni mbaya zaidi zinalenga kuturudisha nyuma.Wahujumu uchumi hawapigani na rais, bali wanapigana na maisha ya wananchi wa Tanzania, tukiwa wamoja tutashinda vita hii, wako watu wanaipinga vita hii yenye dhamira njema, huu si wakati wa kutofautiana ni wakati wa kusimama kumshinda adui,” alisema.

Polepole aliyasema hayo, wakati akitoa wito kwa wananchi, kumuunga mkono Rais Magufuli katika kipindi hiki kigumu kwani nchi iko katika vita mbaya ya uchumi ambayo wahujumu uchumi wamelenga kupigana na maisha ya watanzania na kurudisha nyuma maendeleo ya Taifa.

“Kuna watu walitaka kumhonga rais bilioni 300 ili kusitisha uchunguzi. Walitaka kuhonga bilioni 300 kwa ajili ya kusitisha uchunguzi huo, hivi wao wanapata fedha kiasi gani? Lakini rais akawatolea nje, akasema subirini uchunguzi ukamilike. Tusiamame naye na hakika tutashinda na historia itaandikwa kwamba tulisimama katika kulinda urithi wetu,” amesema.

Katika hatua nyingine, Polepole aliwajibu baadhi ya wanansiasa wanaoikosoa CCM kutokana na viongozi wake waliopita kutunga na kupitisha sheria za madini ambazo zinatetea masilahi ya wawekezaji kuliko nchi, kwa kusema kuwa viongozi walioko sasa ni tofauti na waliopita, na kwamba serikali iliyoko madaraka itarekebisha sheria hizo.

“Tumehujumiwa sana, tumedhurumiwa sana mali za watanzania ambazo tumezirithi kutoka kwa mababu zetu na tuna dhamana ya kuhakikisha zinawafikia watoto wa watoto wetu,” alisema.

NAIBU KATIBU MKUU CCM BARA RODRICK MPOGOLO AMALIZA KWA KISHINDO ZIARA YA KUIMARISHA CHAMA JIMBO LA UBUNGO NA KIBAMBA

Mwenyekiti wa Kamati ya Siasa Wilaya ya Kinondoni na Mwenyekiti wa CCM Kata ya Mzimuni, ambaye pia ni Mwenyekiti wa zamani wa Klabu ya Simba, Hassan Dalali (kulia) akicheza muziki na Katibu Mwenezi wa Kinondoni, Mwinyimku Sangaraza, wakifurahia hotuba ya Naibu Katibu MKuu Bara baada ya kuwahutubia katika Jimbo la Kibamba jijini Dar es Salaam, jana. Picha Zote na Muhidin Sufiani (MAFOTO).
Naibu Katibu Mkuu wa CCM Bara, Rodrick Mpogolo, akiteta jambo na Mkuu wa Wilaya ya Ubungo, Kisare Matiku Makori, katika Ukumbi wa CCM Manzese, wakati wa ziara yake ya kuimarisha Chama kwa kuzungumza na Wenyeviti, Makatibu na Wenezi wa Kata, Makatibu wa Jumuiya ya ngazi za Kata, Wenyeviti wa Mitaa na Mabalozi wa Jimbo hilo la Ubungo jijini Dar esSalaam , jana. 
Mkuu wa Wilaya ya Ubungo, Kisare Matiku Makori, akizungumza kutoa tathmini ya usalama wa kisiasa katika Wilaya yake mbele ya mgeni Rasmi Naibu Katibu Mkuu wa CCM Bara Rodrick Mpogolo, aliyekuwa katika ziara yake ya kuimarisha Chama katika Jimbo la Ubungo, jijini Dar es Salaam, jana. 
Msanii ambaye pia ni Katibu Mwenezi wa Kata ya Makurumla, Shukuru Mbundi, akitoa burudani ya kuimba mbele ya mgeni rasmi, Naibu Katibu Mkuu wa CCM Bara wakati wa mkutano wa kuimarisha Chama katika Jimbo la Ubungo jana.
Naibu Katibu Mkuu wa CCM Bara, Rodrick Mpogolo, akizungumza na Makatibu na Wenezi wa Kata, Makatibu wa Jumuiya ya ngazi za Kata, Wenyeviti wa Mitaa, Mabalozi na Wanachama wa CCM wa Jimbo la Ubungo, wakati akiwa katika ziara yake ya kuimarisha Chama Mkoa wa Dar es Salaam, jana katika Ukumbi wa CCM manzese jijini Dar Es Salaam. 
Naibu Katibu Mkuu wa CCM Bara, Rodrick Mpogolo, akiwatambulisha Wenyeviti wa Serikali ya Mtaa na Mabalozi wa Kata ya Manzese na kuwapa majukumu baada ya kuzungumza na Wenyeviti, Makatibu na Wenezi wa Kata, Makatibu wa Jumuiya ya ngazi za Kata, Wenyeviti wa Mitaa na Mabalozi wa Jimbo la Ubungo, wakati akiwa katika ziara yake ya kuimarisha Chama Mkoa wa Dar es Salaam, jana katika Ukumbi wa CCM manzese jijini Dar Es Salaam.

Mwenyekiti wa UWT Mkoa wa Dar es Salaam, Janeth Masaburi (kushoto) akisebeneka na baadhi ya wanachama wa CCM Kata ya Manzese wakati wa ziara ya Naibu Katibu Mkuu wa CCM Bara , Rodrick Mpogolo, jana. 
Naibu Katibu Mkuu wa CCM Bara, Rodrick Mpogolo, akizungumza na Wenyeviti, Makatibu na Wenezi wa Kata, Makatibu wa Jumuiya ya ngazi za Kata, Wenyeviti wa Mitaa na Mabalozi wa Jimbo la Kibamba, wakati akiwa katika ziara yake ya kuimarisha Chama Mkoa wa Dar es Salaam, katika Ukumbi wa Hoja Kata ya Salanga, jijini Dar es Salaam, jana.
Baadhi ya Viongozi wa Kata ya Salanga Jimbo la Kibamba, wakiwa bize kutunza kumbukumbu ya elimu iliyokuwa ikitolewa kwao na Naibu Katibu Mkuu jana.
Baadhi ya wanachama wa CCM Kata ya Salanga wakisimama na kuimba kumpongeza Naibu Katibu Mkuu wakati wa ziara hiyo.
Naibu Katibu Mkuu wa CCM Bara Rodrick Mpogolo, akiteta jambo na Mjumbe wa Kamati ya Siasa Kata ya Salanga, Euzedius Chilipwei, wakati akiwa katika ziarayake ya kuimarisha Chama Jimbo la KIbamba jana.
Naibu Katibu Mkuu CCM Bara, Rodrick Mpogolo, akijumuika na viongozi na wanachama wa CCM kufurahi kwa pamoja kucheza muziki baada ya kumaliza kuwahutubia katika ziara yake ya kuimarisha Chama kwenye Jimbo la Kibamba Kata ya Salanga jana.

Naibu Katibu Mkuu CCM Bara, Rodrick Mpogolo, akijumuika na viongozi na wanachama wa CCM kufurahi kwa pamoja kucheza muziki baada ya kumaliza kuwahutubia katika ziara yake ya kuimarisha Chama kwenye Jimbo la Kibamba Kata ya Salanga jana.
Mwenyekiti wa Kamati ya Siasa Wilaya ya Kinondoni na Mwenyekiti wa CCM Kata ya Mzimuni, 
ambaye pia ni Mwenyekiti wa zamani wa Klabu ya Simba, Hassan Dalali (kulia) akicheza muziki na Katibu Mwenezi wa Kinondoni, Mwinyimku Sangaraza, wakifurahia hotuba ya Naibu Katibu MKuu Bara baada ya kuwahutubia katika Jimbo la Kibamba jijini Dar es Salaam, jana.

Naibu Katibu akiondoka ukumbini
Akiagana na baadhi ya viongozi